< תהילים 113 >
הללו יה הללו עבדי יהוה הללו את שם יהוה׃ | 1 |
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
יהי שם יהוה מברך מעתה ועד עולם׃ | 2 |
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
ממזרח שמש עד מבואו מהלל שם יהוה׃ | 3 |
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
רם על כל גוים יהוה על השמים כבודו׃ | 4 |
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
מי כיהוה אלהינו המגביהי לשבת׃ | 5 |
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
המשפילי לראות בשמים ובארץ׃ | 6 |
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
מקימי מעפר דל מאשפת ירים אביון׃ | 7 |
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
להושיבי עם נדיבים עם נדיבי עמו׃ | 8 |
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
מושיבי עקרת הבית אם הבנים שמחה הללו יה׃ | 9 |
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.