< תהילים 113 >

הללו יה הללו עבדי יהוה הללו את שם יהוה׃ 1
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
יהי שם יהוה מברך מעתה ועד עולם׃ 2
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
ממזרח שמש עד מבואו מהלל שם יהוה׃ 3
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
רם על כל גוים יהוה על השמים כבודו׃ 4
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
מי כיהוה אלהינו המגביהי לשבת׃ 5
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
המשפילי לראות בשמים ובארץ׃ 6
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
מקימי מעפר דל מאשפת ירים אביון׃ 7
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
להושיבי עם נדיבים עם נדיבי עמו׃ 8
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
מושיבי עקרת הבית אם הבנים שמחה הללו יה׃ 9
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< תהילים 113 >