< תהילים 107 >

הדו ליהוה כי טוב כי לעולם חסדו׃ 1
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
יאמרו גאולי יהוה אשר גאלם מיד צר׃ 2
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
ומארצות קבצם ממזרח וממערב מצפון ומים׃ 3
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
תעו במדבר בישימון דרך עיר מושב לא מצאו׃ 4
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
רעבים גם צמאים נפשם בהם תתעטף׃ 5
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
ויצעקו אל יהוה בצר להם ממצוקותיהם יצילם׃ 6
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
וידריכם בדרך ישרה ללכת אל עיר מושב׃ 7
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ 8
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
כי השביע נפש שקקה ונפש רעבה מלא טוב׃ 9
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
ישבי חשך וצלמות אסירי עני וברזל׃ 10
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
כי המרו אמרי אל ועצת עליון נאצו׃ 11
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
ויכנע בעמל לבם כשלו ואין עזר׃ 12
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
ויזעקו אל יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם׃ 13
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
יוציאם מחשך וצלמות ומוסרותיהם ינתק׃ 14
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ 15
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
כי שבר דלתות נחשת ובריחי ברזל גדע׃ 16
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
אולים מדרך פשעם ומעונתיהם יתענו׃ 17
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
כל אכל תתעב נפשם ויגיעו עד שערי מות׃ 18
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
ויזעקו אל יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם׃ 19
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
ישלח דברו וירפאם וימלט משחיתותם׃ 20
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ 21
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
ויזבחו זבחי תודה ויספרו מעשיו ברנה׃ 22
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
יורדי הים באניות עשי מלאכה במים רבים׃ 23
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
המה ראו מעשי יהוה ונפלאותיו במצולה׃ 24
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
ויאמר ויעמד רוח סערה ותרומם גליו׃ 25
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
יעלו שמים ירדו תהומות נפשם ברעה תתמוגג׃ 26
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
יחוגו וינועו כשכור וכל חכמתם תתבלע׃ 27
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
ויצעקו אל יהוה בצר להם וממצוקתיהם יוציאם׃ 28
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
יקם סערה לדממה ויחשו גליהם׃ 29
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
וישמחו כי ישתקו וינחם אל מחוז חפצם׃ 30
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ 31
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
וירממוהו בקהל עם ובמושב זקנים יהללוהו׃ 32
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
ישם נהרות למדבר ומצאי מים לצמאון׃ 33
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
ארץ פרי למלחה מרעת ישבי בה׃ 34
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
ישם מדבר לאגם מים וארץ ציה למצאי מים׃ 35
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
ויושב שם רעבים ויכוננו עיר מושב׃ 36
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
ויזרעו שדות ויטעו כרמים ויעשו פרי תבואה׃ 37
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
ויברכם וירבו מאד ובהמתם לא ימעיט׃ 38
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
וימעטו וישחו מעצר רעה ויגון׃ 39
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
שפך בוז על נדיבים ויתעם בתהו לא דרך׃ 40
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
וישגב אביון מעוני וישם כצאן משפחות׃ 41
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
יראו ישרים וישמחו וכל עולה קפצה פיה׃ 42
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
מי חכם וישמר אלה ויתבוננו חסדי יהוה׃ 43
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< תהילים 107 >