< תהילים 107 >
הדו ליהוה כי טוב כי לעולם חסדו׃ | 1 |
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
יאמרו גאולי יהוה אשר גאלם מיד צר׃ | 2 |
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
ומארצות קבצם ממזרח וממערב מצפון ומים׃ | 3 |
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
תעו במדבר בישימון דרך עיר מושב לא מצאו׃ | 4 |
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
רעבים גם צמאים נפשם בהם תתעטף׃ | 5 |
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
ויצעקו אל יהוה בצר להם ממצוקותיהם יצילם׃ | 6 |
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
וידריכם בדרך ישרה ללכת אל עיר מושב׃ | 7 |
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 8 |
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
כי השביע נפש שקקה ונפש רעבה מלא טוב׃ | 9 |
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
ישבי חשך וצלמות אסירי עני וברזל׃ | 10 |
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
כי המרו אמרי אל ועצת עליון נאצו׃ | 11 |
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
ויכנע בעמל לבם כשלו ואין עזר׃ | 12 |
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
ויזעקו אל יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם׃ | 13 |
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
יוציאם מחשך וצלמות ומוסרותיהם ינתק׃ | 14 |
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 15 |
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
כי שבר דלתות נחשת ובריחי ברזל גדע׃ | 16 |
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
אולים מדרך פשעם ומעונתיהם יתענו׃ | 17 |
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
כל אכל תתעב נפשם ויגיעו עד שערי מות׃ | 18 |
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
ויזעקו אל יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם׃ | 19 |
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
ישלח דברו וירפאם וימלט משחיתותם׃ | 20 |
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 21 |
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
ויזבחו זבחי תודה ויספרו מעשיו ברנה׃ | 22 |
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
יורדי הים באניות עשי מלאכה במים רבים׃ | 23 |
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
המה ראו מעשי יהוה ונפלאותיו במצולה׃ | 24 |
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
ויאמר ויעמד רוח סערה ותרומם גליו׃ | 25 |
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
יעלו שמים ירדו תהומות נפשם ברעה תתמוגג׃ | 26 |
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
יחוגו וינועו כשכור וכל חכמתם תתבלע׃ | 27 |
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
ויצעקו אל יהוה בצר להם וממצוקתיהם יוציאם׃ | 28 |
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
יקם סערה לדממה ויחשו גליהם׃ | 29 |
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
וישמחו כי ישתקו וינחם אל מחוז חפצם׃ | 30 |
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 31 |
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
וירממוהו בקהל עם ובמושב זקנים יהללוהו׃ | 32 |
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
ישם נהרות למדבר ומצאי מים לצמאון׃ | 33 |
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
ארץ פרי למלחה מרעת ישבי בה׃ | 34 |
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
ישם מדבר לאגם מים וארץ ציה למצאי מים׃ | 35 |
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
ויושב שם רעבים ויכוננו עיר מושב׃ | 36 |
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
ויזרעו שדות ויטעו כרמים ויעשו פרי תבואה׃ | 37 |
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
ויברכם וירבו מאד ובהמתם לא ימעיט׃ | 38 |
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
וימעטו וישחו מעצר רעה ויגון׃ | 39 |
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
שפך בוז על נדיבים ויתעם בתהו לא דרך׃ | 40 |
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
וישגב אביון מעוני וישם כצאן משפחות׃ | 41 |
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
יראו ישרים וישמחו וכל עולה קפצה פיה׃ | 42 |
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
מי חכם וישמר אלה ויתבוננו חסדי יהוה׃ | 43 |
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.