< תהילים 107 >
הדו ליהוה כי טוב כי לעולם חסדו׃ | 1 |
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
יאמרו גאולי יהוה אשר גאלם מיד צר׃ | 2 |
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
ומארצות קבצם ממזרח וממערב מצפון ומים׃ | 3 |
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
תעו במדבר בישימון דרך עיר מושב לא מצאו׃ | 4 |
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
רעבים גם צמאים נפשם בהם תתעטף׃ | 5 |
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
ויצעקו אל יהוה בצר להם ממצוקותיהם יצילם׃ | 6 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
וידריכם בדרך ישרה ללכת אל עיר מושב׃ | 7 |
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 8 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
כי השביע נפש שקקה ונפש רעבה מלא טוב׃ | 9 |
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
ישבי חשך וצלמות אסירי עני וברזל׃ | 10 |
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
כי המרו אמרי אל ועצת עליון נאצו׃ | 11 |
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
ויכנע בעמל לבם כשלו ואין עזר׃ | 12 |
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
ויזעקו אל יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם׃ | 13 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
יוציאם מחשך וצלמות ומוסרותיהם ינתק׃ | 14 |
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 15 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
כי שבר דלתות נחשת ובריחי ברזל גדע׃ | 16 |
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
אולים מדרך פשעם ומעונתיהם יתענו׃ | 17 |
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
כל אכל תתעב נפשם ויגיעו עד שערי מות׃ | 18 |
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
ויזעקו אל יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם׃ | 19 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
ישלח דברו וירפאם וימלט משחיתותם׃ | 20 |
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 21 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
ויזבחו זבחי תודה ויספרו מעשיו ברנה׃ | 22 |
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
יורדי הים באניות עשי מלאכה במים רבים׃ | 23 |
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
המה ראו מעשי יהוה ונפלאותיו במצולה׃ | 24 |
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
ויאמר ויעמד רוח סערה ותרומם גליו׃ | 25 |
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
יעלו שמים ירדו תהומות נפשם ברעה תתמוגג׃ | 26 |
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
יחוגו וינועו כשכור וכל חכמתם תתבלע׃ | 27 |
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
ויצעקו אל יהוה בצר להם וממצוקתיהם יוציאם׃ | 28 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
יקם סערה לדממה ויחשו גליהם׃ | 29 |
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
וישמחו כי ישתקו וינחם אל מחוז חפצם׃ | 30 |
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם׃ | 31 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
וירממוהו בקהל עם ובמושב זקנים יהללוהו׃ | 32 |
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
ישם נהרות למדבר ומצאי מים לצמאון׃ | 33 |
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
ארץ פרי למלחה מרעת ישבי בה׃ | 34 |
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
ישם מדבר לאגם מים וארץ ציה למצאי מים׃ | 35 |
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
ויושב שם רעבים ויכוננו עיר מושב׃ | 36 |
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
ויזרעו שדות ויטעו כרמים ויעשו פרי תבואה׃ | 37 |
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
ויברכם וירבו מאד ובהמתם לא ימעיט׃ | 38 |
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
וימעטו וישחו מעצר רעה ויגון׃ | 39 |
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
שפך בוז על נדיבים ויתעם בתהו לא דרך׃ | 40 |
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
וישגב אביון מעוני וישם כצאן משפחות׃ | 41 |
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
יראו ישרים וישמחו וכל עולה קפצה פיה׃ | 42 |
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
מי חכם וישמר אלה ויתבוננו חסדי יהוה׃ | 43 |
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.