< תהילים 105 >
הודו ליהוה קראו בשמו הודיעו בעמים עלילותיו׃ | 1 |
Mshukuruni Yahwe, liitieni jina lake; myafanye matendo yake yajulikane kati ya mataifa.
שירו לו זמרו לו שיחו בכל נפלאותיו׃ | 2 |
Mwimbieni yeye, mwimbieni sifa yeye; semeni matendo yake yote ya ajau.
התהללו בשם קדשו ישמח לב מבקשי יהוה׃ | 3 |
Mjivune katika utakatifu wa jina lake; moyo wao wamtafutao Yahwe ufurahi.
דרשו יהוה ועזו בקשו פניו תמיד׃ | 4 |
Mtafuteni Yahwe na nguvu zake; utafuteni uwepo wake siku zote.
זכרו נפלאותיו אשר עשה מפתיו ומשפטי פיו׃ | 5 |
Kumbukeni mambo ya ajabu aliyoyatenda,
זרע אברהם עבדו בני יעקב בחיריו׃ | 6 |
miujiza yake na amri zitokazo kinywani mwake, enyi kizazi cha Ibrahimu mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wachaguliwa wake.
הוא יהוה אלהינו בכל הארץ משפטיו׃ | 7 |
Yeye ni Yahwe, Mungu wetu. Amri zake ziko juu ya nchi yote.
זכר לעולם בריתו דבר צוה לאלף דור׃ | 8 |
Naye hulikumbuka agano lake milele, neno alilo amuru kwa ajili ya vizazi elfu.
אשר כרת את אברהם ושבועתו לישחק׃ | 9 |
Hulikumbuka agano alilolifanya na Ibrahimu na kiapo alicho mwapia Isaka.
ויעמידה ליעקב לחק לישראל ברית עולם׃ | 10 |
Hiki ndicho alicho mthibitishia Yakobo kama agano na kama agano la milele kwa Israeli.
לאמר לך אתן את ארץ כנען חבל נחלתכם׃ | 11 |
Alisema, “Nitakupa wewe ardhi ya Kanaani kama sehemu yako ya urithi.”
בהיותם מתי מספר כמעט וגרים בה׃ | 12 |
Alisema hili wakati tu walipokuwa wachache katika hesabu, yaani wachahe sana, nao walikuwa wageni katika nchi.
ויתהלכו מגוי אל גוי מממלכה אל עם אחר׃ | 13 |
Walienda taifa hadi taifa na kutoka ufalme moja kwenda mwingine.
לא הניח אדם לעשקם ויוכח עליהם מלכים׃ | 14 |
Hakuruhusu yeyote kuwaonea; aliwakemea wafalme kwa ajili yao.
אל תגעו במשיחי ולנביאי אל תרעו׃ | 15 |
Alisema, “Msiwaguze wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
ויקרא רעב על הארץ כל מטה לחם שבר׃ | 16 |
Aliita njaa katika nchi; akaondoa upatikanaji wa mkate wote.
שלח לפניהם איש לעבד נמכר יוסף׃ | 17 |
Akatuma mtu mbele yao; Yusufu aliuzwa kama mtumishi.
ענו בכבל רגליו ברזל באה נפשו׃ | 18 |
Miguu yake ilifungwa kwa pingu; alivishwa mnyororo wa chuma shingoni mwake,
עד עת בא דברו אמרת יהוה צרפתהו׃ | 19 |
mpaka wakati wa maneno yake ulipotimia, nalo neno la Yahwe lilimjaribu.
שלח מלך ויתירהו משל עמים ויפתחהו׃ | 20 |
Mfalme alituma watumishi kumfungua; mtawala wa watu alimuweka huru.
שמו אדון לביתו ומשל בכל קנינו׃ | 21 |
Alimuweka kuwa msimamizi wa nyumba yake kama mtawala wa mali zake zote
לאסר שריו בנפשו וזקניו יחכם׃ | 22 |
kuwaelekeza wakuu kama alivyopenda na kuwafundisha viongozi wake hekima.
ויבא ישראל מצרים ויעקב גר בארץ חם׃ | 23 |
Kisha Israeli iliingia Misri, na Yakobo aliishi kwa muda katika nchi ya Hamu.
ויפר את עמו מאד ויעצמהו מצריו׃ | 24 |
Yahwe aliwajalia watu wake wazae sana, na aliwafanya wenye nguvu kuliko adui zao.
הפך לבם לשנא עמו להתנכל בעבדיו׃ | 25 |
Alisababisha adui zao wawachukie watu wake, na kuwatendea visivyo watumishi wake.
שלח משה עבדו אהרן אשר בחר בו׃ | 26 |
Alimtuma Musa, mtumishi wake, na Haruni, ambaye alikwisha mchagua.
שמו בם דברי אתותיו ומפתים בארץ חם׃ | 27 |
Walifanya ishara zake kati ya Wamisri na maajabu yake katika ya nchi ya Hamu.
שלח חשך ויחשך ולא מרו את דבריו׃ | 28 |
Alituma giza na likaifanya nchi hiyo kuwa giza, lakini watu wake hawakutii amri zake.
הפך את מימיהם לדם וימת את דגתם׃ | 29 |
Aligeuza maji kuwa damu na aliua samaki wao.
שרץ ארצם צפרדעים בחדרי מלכיהם׃ | 30 |
Nchi yao ilijaa vyura, hata katika vyumba vya watawala wao.
אמר ויבא ערב כנים בכל גבולם׃ | 31 |
Alisema, na makundi ya inzi na chawa wakaja mjini mwote.
נתן גשמיהם ברד אש להבות בארצם׃ | 32 |
Aliigeuza mvua yao kuwa mvua ya mawe, pamoja na miali ya moto juu ya ardhi yao.
ויך גפנם ותאנתם וישבר עץ גבולם׃ | 33 |
Aliiharibu mizabibu yao na mitini yao; akaivunja miti ya mji wao.
אמר ויבא ארבה וילק ואין מספר׃ | 34 |
Alisema, na nzige wakaja, nzige wengi sana.
ויאכל כל עשב בארצם ויאכל פרי אדמתם׃ | 35 |
Nzige walikula mboga zao zote za majani katika nchi yao. Walikula mazao yote ardhini.
ויך כל בכור בארצם ראשית לכל אונם׃ | 36 |
Aliua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao, malimbuko ya nguvu zao.
ויוציאם בכסף וזהב ואין בשבטיו כושל׃ | 37 |
Aliwatoa nje Waisraeli wakiwa na fedha na dhahabu; hakuna mmoja wa kabila lake aliyejikwaa njiani.
שמח מצרים בצאתם כי נפל פחדם עליהם׃ | 38 |
Misri ilifurahi walipoondoka, maana Wamisri waliwaogopa.
פרש ענן למסך ואש להאיר לילה׃ | 39 |
Alitandaza wingu liwafunike na alifanya moto uwaangazie wakati wa usiku.
שאל ויבא שלו ולחם שמים ישביעם׃ | 40 |
Waisraeli waliomba chakula, naye aliwaletea kware na aliwatosheleza kwa mkate kutoka mbiguni.
פתח צור ויזובו מים הלכו בציות נהר׃ | 41 |
Aliugawa mwamba, maji yalimwagika kutoka humo; yalitiririka katika jangwa kama mto.
כי זכר את דבר קדשו את אברהם עבדו׃ | 42 |
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu aliyoifanya kwa Ibrahimu mtumishi wake.
ויוצא עמו בששון ברנה את בחיריו׃ | 43 |
Aliwaongoza watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za ushindi.
ויתן להם ארצות גוים ועמל לאמים יירשו׃ | 44 |
Aliwapa nchi za mataifa; walichukua milki ya mali za watu
בעבור ישמרו חקיו ותורתיו ינצרו הללו יה׃ | 45 |
ili waweze kushika amri zake na kutii sheria zake. Msifuni Yahwe.