< תהילים 103 >
לדוד ברכי נפשי את יהוה וכל קרבי את שם קדשו׃ | 1 |
Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu.
ברכי נפשי את יהוה ואל תשכחי כל גמוליו׃ | 2 |
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, wala usisahau wema wake wote,
הסלח לכל עונכי הרפא לכל תחלאיכי׃ | 3 |
akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote,
הגואל משחת חייכי המעטרכי חסד ורחמים׃ | 4 |
aukomboa uhai wako na kaburi, akuvika taji ya upendo na huruma,
המשביע בטוב עדיך תתחדש כנשר נעוריכי׃ | 5 |
atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema, ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
עשה צדקות יהוה ומשפטים לכל עשוקים׃ | 6 |
Bwana hutenda haki, naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.
יודיע דרכיו למשה לבני ישראל עלילותיו׃ | 7 |
Alijulisha Mose njia zake, na wana wa Israeli matendo yake.
רחום וחנון יהוה ארך אפים ורב חסד׃ | 8 |
Bwana ni mwingi wa huruma na mwenye neema; si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo.
לא לנצח יריב ולא לעולם יטור׃ | 9 |
Yeye hatalaumu siku zote, wala haweki hasira yake milele,
לא כחטאינו עשה לנו ולא כעונתינו גמל עלינו׃ | 10 |
yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.
כי כגבה שמים על הארץ גבר חסדו על יראיו׃ | 11 |
Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia sana, ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha;
כרחק מזרח ממערב הרחיק ממנו את פשעינו׃ | 12 |
kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi.
כרחם אב על בנים רחם יהוה על יראיו׃ | 13 |
Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha;
כי הוא ידע יצרנו זכור כי עפר אנחנו׃ | 14 |
kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.
אנוש כחציר ימיו כציץ השדה כן יציץ׃ | 15 |
Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, anachanua kama ua la shambani;
כי רוח עברה בו ואיננו ולא יכירנו עוד מקומו׃ | 16 |
upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, mahali pake hapalikumbuki tena.
וחסד יהוה מעולם ועד עולם על יראיו וצדקתו לבני בנים׃ | 17 |
Lakini kutoka milele hata milele upendo wa Bwana uko kwa wale wamchao, nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao:
לשמרי בריתו ולזכרי פקדיו לעשותם׃ | 18 |
kwa wale walishikao agano lake na kukumbuka kuyatii mausia yake.
יהוה בשמים הכין כסאו ומלכותו בכל משלה׃ | 19 |
Bwana ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni, ufalme wake unatawala juu ya vyote.
ברכו יהוה מלאכיו גברי כח עשי דברו לשמע בקול דברו׃ | 20 |
Mhimidini Bwana, enyi malaika zake, ninyi mlio mashujaa mnaozitii amri zake, ninyi mnaotii neno lake.
ברכו יהוה כל צבאיו משרתיו עשי רצונו׃ | 21 |
Mhimidini Bwana, ninyi jeshi lake lote la mbinguni, ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake.
ברכו יהוה כל מעשיו בכל מקמות ממשלתו ברכי נפשי את יהוה׃ | 22 |
Mhimidini Bwana, kazi zake zote kila mahali katika milki yake. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.