< תהילים 103 >

לדוד ברכי נפשי את יהוה וכל קרבי את שם קדשו׃ 1
Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu.
ברכי נפשי את יהוה ואל תשכחי כל גמוליו׃ 2
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, wala usisahau wema wake wote,
הסלח לכל עונכי הרפא לכל תחלאיכי׃ 3
akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote,
הגואל משחת חייכי המעטרכי חסד ורחמים׃ 4
aukomboa uhai wako na kaburi, akuvika taji ya upendo na huruma,
המשביע בטוב עדיך תתחדש כנשר נעוריכי׃ 5
atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema, ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
עשה צדקות יהוה ומשפטים לכל עשוקים׃ 6
Bwana hutenda haki, naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.
יודיע דרכיו למשה לבני ישראל עלילותיו׃ 7
Alijulisha Mose njia zake, na wana wa Israeli matendo yake.
רחום וחנון יהוה ארך אפים ורב חסד׃ 8
Bwana ni mwingi wa huruma na mwenye neema; si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo.
לא לנצח יריב ולא לעולם יטור׃ 9
Yeye hatalaumu siku zote, wala haweki hasira yake milele,
לא כחטאינו עשה לנו ולא כעונתינו גמל עלינו׃ 10
yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.
כי כגבה שמים על הארץ גבר חסדו על יראיו׃ 11
Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia sana, ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha;
כרחק מזרח ממערב הרחיק ממנו את פשעינו׃ 12
kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi.
כרחם אב על בנים רחם יהוה על יראיו׃ 13
Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha;
כי הוא ידע יצרנו זכור כי עפר אנחנו׃ 14
kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.
אנוש כחציר ימיו כציץ השדה כן יציץ׃ 15
Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, anachanua kama ua la shambani;
כי רוח עברה בו ואיננו ולא יכירנו עוד מקומו׃ 16
upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, mahali pake hapalikumbuki tena.
וחסד יהוה מעולם ועד עולם על יראיו וצדקתו לבני בנים׃ 17
Lakini kutoka milele hata milele upendo wa Bwana uko kwa wale wamchao, nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao:
לשמרי בריתו ולזכרי פקדיו לעשותם׃ 18
kwa wale walishikao agano lake na kukumbuka kuyatii mausia yake.
יהוה בשמים הכין כסאו ומלכותו בכל משלה׃ 19
Bwana ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni, ufalme wake unatawala juu ya vyote.
ברכו יהוה מלאכיו גברי כח עשי דברו לשמע בקול דברו׃ 20
Mhimidini Bwana, enyi malaika zake, ninyi mlio mashujaa mnaozitii amri zake, ninyi mnaotii neno lake.
ברכו יהוה כל צבאיו משרתיו עשי רצונו׃ 21
Mhimidini Bwana, ninyi jeshi lake lote la mbinguni, ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake.
ברכו יהוה כל מעשיו בכל מקמות ממשלתו ברכי נפשי את יהוה׃ 22
Mhimidini Bwana, kazi zake zote kila mahali katika milki yake. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.

< תהילים 103 >