< מִשְׁלֵי 9 >
חכמות בנתה ביתה חצבה עמודיה שבעה׃ | 1 |
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
טבחה טבחה מסכה יינה אף ערכה שלחנה׃ | 2 |
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
שלחה נערתיה תקרא על גפי מרמי קרת׃ | 3 |
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
מי פתי יסר הנה חסר לב אמרה לו׃ | 4 |
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
לכו לחמו בלחמי ושתו ביין מסכתי׃ | 5 |
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
עזבו פתאים וחיו ואשרו בדרך בינה׃ | 6 |
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
יסר לץ לקח לו קלון ומוכיח לרשע מומו׃ | 7 |
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
אל תוכח לץ פן ישנאך הוכח לחכם ויאהבך׃ | 8 |
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
תן לחכם ויחכם עוד הודע לצדיק ויוסף לקח׃ | 9 |
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
תחלת חכמה יראת יהוה ודעת קדשים בינה׃ | 10 |
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
כי בי ירבו ימיך ויוסיפו לך שנות חיים׃ | 11 |
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
אם חכמת חכמת לך ולצת לבדך תשא׃ | 12 |
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
אשת כסילות המיה פתיות ובל ידעה מה׃ | 13 |
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
וישבה לפתח ביתה על כסא מרמי קרת׃ | 14 |
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
לקרא לעברי דרך המישרים ארחותם׃ | 15 |
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
מי פתי יסר הנה וחסר לב ואמרה לו׃ | 16 |
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
מים גנובים ימתקו ולחם סתרים ינעם׃ | 17 |
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
ולא ידע כי רפאים שם בעמקי שאול קראיה׃ (Sheol ) | 18 |
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )