< מִשְׁלֵי 9 >

חכמות בנתה ביתה חצבה עמודיה שבעה׃ 1
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
טבחה טבחה מסכה יינה אף ערכה שלחנה׃ 2
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
שלחה נערתיה תקרא על גפי מרמי קרת׃ 3
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
מי פתי יסר הנה חסר לב אמרה לו׃ 4
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
לכו לחמו בלחמי ושתו ביין מסכתי׃ 5
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
עזבו פתאים וחיו ואשרו בדרך בינה׃ 6
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
יסר לץ לקח לו קלון ומוכיח לרשע מומו׃ 7
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
אל תוכח לץ פן ישנאך הוכח לחכם ויאהבך׃ 8
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
תן לחכם ויחכם עוד הודע לצדיק ויוסף לקח׃ 9
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
תחלת חכמה יראת יהוה ודעת קדשים בינה׃ 10
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
כי בי ירבו ימיך ויוסיפו לך שנות חיים׃ 11
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
אם חכמת חכמת לך ולצת לבדך תשא׃ 12
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
אשת כסילות המיה פתיות ובל ידעה מה׃ 13
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
וישבה לפתח ביתה על כסא מרמי קרת׃ 14
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
לקרא לעברי דרך המישרים ארחותם׃ 15
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
מי פתי יסר הנה וחסר לב ואמרה לו׃ 16
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
מים גנובים ימתקו ולחם סתרים ינעם׃ 17
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
ולא ידע כי רפאים שם בעמקי שאול קראיה׃ (Sheol h7585) 18
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< מִשְׁלֵי 9 >