< מִשְׁלֵי 7 >
בני שמר אמרי ומצותי תצפן אתך׃ | 1 |
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
שמר מצותי וחיה ותורתי כאישון עיניך׃ | 2 |
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
קשרם על אצבעתיך כתבם על לוח לבך׃ | 3 |
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
אמר לחכמה אחתי את ומדע לבינה תקרא׃ | 4 |
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
לשמרך מאשה זרה מנכריה אמריה החליקה׃ | 5 |
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
כי בחלון ביתי בעד אשנבי נשקפתי׃ | 6 |
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
וארא בפתאים אבינה בבנים נער חסר לב׃ | 7 |
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
עבר בשוק אצל פנה ודרך ביתה יצעד׃ | 8 |
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
בנשף בערב יום באישון לילה ואפלה׃ | 9 |
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
והנה אשה לקראתו שית זונה ונצרת לב׃ | 10 |
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
המיה היא וסררת בביתה לא ישכנו רגליה׃ | 11 |
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
פעם בחוץ פעם ברחבות ואצל כל פנה תארב׃ | 12 |
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
והחזיקה בו ונשקה לו העזה פניה ותאמר לו׃ | 13 |
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
זבחי שלמים עלי היום שלמתי נדרי׃ | 14 |
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
על כן יצאתי לקראתך לשחר פניך ואמצאך׃ | 15 |
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
מרבדים רבדתי ערשי חטבות אטון מצרים׃ | 16 |
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
נפתי משכבי מר אהלים וקנמון׃ | 17 |
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
לכה נרוה דדים עד הבקר נתעלסה באהבים׃ | 18 |
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
כי אין האיש בביתו הלך בדרך מרחוק׃ | 19 |
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
צרור הכסף לקח בידו ליום הכסא יבא ביתו׃ | 20 |
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
הטתו ברב לקחה בחלק שפתיה תדיחנו׃ | 21 |
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
הולך אחריה פתאם כשור אל טבח יבוא וכעכס אל מוסר אויל׃ | 22 |
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
עד יפלח חץ כבדו כמהר צפור אל פח ולא ידע כי בנפשו הוא׃ | 23 |
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
ועתה בנים שמעו לי והקשיבו לאמרי פי׃ | 24 |
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
אל ישט אל דרכיה לבך אל תתע בנתיבותיה׃ | 25 |
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
כי רבים חללים הפילה ועצמים כל הרגיה׃ | 26 |
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
דרכי שאול ביתה ירדות אל חדרי מות׃ (Sheol ) | 27 |
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )