< מִשְׁלֵי 7 >
בני שמר אמרי ומצותי תצפן אתך׃ | 1 |
Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
שמר מצותי וחיה ותורתי כאישון עיניך׃ | 2 |
Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
קשרם על אצבעתיך כתבם על לוח לבך׃ | 3 |
Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
אמר לחכמה אחתי את ומדע לבינה תקרא׃ | 4 |
Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
לשמרך מאשה זרה מנכריה אמריה החליקה׃ | 5 |
watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
כי בחלון ביתי בעד אשנבי נשקפתי׃ | 6 |
Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
וארא בפתאים אבינה בבנים נער חסר לב׃ | 7 |
Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
עבר בשוק אצל פנה ודרך ביתה יצעד׃ | 8 |
Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
בנשף בערב יום באישון לילה ואפלה׃ | 9 |
wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
והנה אשה לקראתו שית זונה ונצרת לב׃ | 10 |
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
המיה היא וסררת בביתה לא ישכנו רגליה׃ | 11 |
(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
פעם בחוץ פעם ברחבות ואצל כל פנה תארב׃ | 12 |
mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
והחזיקה בו ונשקה לו העזה פניה ותאמר לו׃ | 13 |
Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
זבחי שלמים עלי היום שלמתי נדרי׃ | 14 |
“Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
על כן יצאתי לקראתך לשחר פניך ואמצאך׃ | 15 |
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
מרבדים רבדתי ערשי חטבות אטון מצרים׃ | 16 |
Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
נפתי משכבי מר אהלים וקנמון׃ | 17 |
Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
לכה נרוה דדים עד הבקר נתעלסה באהבים׃ | 18 |
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
כי אין האיש בביתו הלך בדרך מרחוק׃ | 19 |
Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
צרור הכסף לקח בידו ליום הכסא יבא ביתו׃ | 20 |
Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
הטתו ברב לקחה בחלק שפתיה תדיחנו׃ | 21 |
Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
הולך אחריה פתאם כשור אל טבח יבוא וכעכס אל מוסר אויל׃ | 22 |
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
עד יפלח חץ כבדו כמהר צפור אל פח ולא ידע כי בנפשו הוא׃ | 23 |
mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
ועתה בנים שמעו לי והקשיבו לאמרי פי׃ | 24 |
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
אל ישט אל דרכיה לבך אל תתע בנתיבותיה׃ | 25 |
Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
כי רבים חללים הפילה ועצמים כל הרגיה׃ | 26 |
Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
דרכי שאול ביתה ירדות אל חדרי מות׃ (Sheol ) | 27 |
Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )