< מִשְׁלֵי 7 >

בני שמר אמרי ומצותי תצפן אתך׃ 1
Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
שמר מצותי וחיה ותורתי כאישון עיניך׃ 2
Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
קשרם על אצבעתיך כתבם על לוח לבך׃ 3
Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
אמר לחכמה אחתי את ומדע לבינה תקרא׃ 4
Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
לשמרך מאשה זרה מנכריה אמריה החליקה׃ 5
watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
כי בחלון ביתי בעד אשנבי נשקפתי׃ 6
Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
וארא בפתאים אבינה בבנים נער חסר לב׃ 7
Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
עבר בשוק אצל פנה ודרך ביתה יצעד׃ 8
Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
בנשף בערב יום באישון לילה ואפלה׃ 9
wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
והנה אשה לקראתו שית זונה ונצרת לב׃ 10
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
המיה היא וסררת בביתה לא ישכנו רגליה׃ 11
(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
פעם בחוץ פעם ברחבות ואצל כל פנה תארב׃ 12
mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
והחזיקה בו ונשקה לו העזה פניה ותאמר לו׃ 13
Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
זבחי שלמים עלי היום שלמתי נדרי׃ 14
“Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
על כן יצאתי לקראתך לשחר פניך ואמצאך׃ 15
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
מרבדים רבדתי ערשי חטבות אטון מצרים׃ 16
Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
נפתי משכבי מר אהלים וקנמון׃ 17
Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
לכה נרוה דדים עד הבקר נתעלסה באהבים׃ 18
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
כי אין האיש בביתו הלך בדרך מרחוק׃ 19
Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
צרור הכסף לקח בידו ליום הכסא יבא ביתו׃ 20
Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
הטתו ברב לקחה בחלק שפתיה תדיחנו׃ 21
Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
הולך אחריה פתאם כשור אל טבח יבוא וכעכס אל מוסר אויל׃ 22
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
עד יפלח חץ כבדו כמהר צפור אל פח ולא ידע כי בנפשו הוא׃ 23
mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
ועתה בנים שמעו לי והקשיבו לאמרי פי׃ 24
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
אל ישט אל דרכיה לבך אל תתע בנתיבותיה׃ 25
Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
כי רבים חללים הפילה ועצמים כל הרגיה׃ 26
Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
דרכי שאול ביתה ירדות אל חדרי מות׃ (Sheol h7585) 27
Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< מִשְׁלֵי 7 >