< מִשְׁלֵי 4 >
שמעו בנים מוסר אב והקשיבו לדעת בינה׃ | 1 |
Wanangu, sikilizeni, fundisho la baba, na zingatieni ili mjue maana ya ufahamu.
כי לקח טוב נתתי לכם תורתי אל תעזבו׃ | 2 |
Mimi ninawapa mafundisho mazuri; msiyaache mafundisho yangu.
כי בן הייתי לאבי רך ויחיד לפני אמי׃ | 3 |
Mimi nilikuwa mwana kwa baba yangu, mpole na mtoto pekee kwa mama yangu,
וירני ויאמר לי יתמך דברי לבך שמר מצותי וחיה׃ | 4 |
baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
קנה חכמה קנה בינה אל תשכח ואל תט מאמרי פי׃ | 5 |
Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
אל תעזבה ותשמרך אהבה ותצרך׃ | 6 |
usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
ראשית חכמה קנה חכמה ובכל קנינך קנה בינה׃ | 7 |
Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
סלסלה ותרוממך תכבדך כי תחבקנה׃ | 8 |
Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
תתן לראשך לוית חן עטרת תפארת תמגנך׃ | 9 |
Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
שמע בני וקח אמרי וירבו לך שנות חיים׃ | 10 |
Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
בדרך חכמה הרתיך הדרכתיך במעגלי ישר׃ | 11 |
Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
בלכתך לא יצר צעדך ואם תרוץ לא תכשל׃ | 12 |
Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
החזק במוסר אל תרף נצרה כי היא חייך׃ | 13 |
Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
בארח רשעים אל תבא ואל תאשר בדרך רעים׃ | 14 |
Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
פרעהו אל תעבר בו שטה מעליו ועבור׃ | 15 |
Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
כי לא ישנו אם לא ירעו ונגזלה שנתם אם לא יכשולו׃ | 16 |
Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
כי לחמו לחם רשע ויין חמסים ישתו׃ | 17 |
Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
וארח צדיקים כאור נגה הולך ואור עד נכון היום׃ | 18 |
Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
דרך רשעים כאפלה לא ידעו במה יכשלו׃ | 19 |
Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
בני לדברי הקשיבה לאמרי הט אזנך׃ | 20 |
Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
אל יליזו מעיניך שמרם בתוך לבבך׃ | 21 |
Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.
כי חיים הם למצאיהם ולכל בשרו מרפא׃ | 22 |
Maana maneno yangu ni uzima kwa wenye kuyapata na afya katika mwili wao.
מכל משמר נצר לבך כי ממנו תוצאות חיים׃ | 23 |
Ulinde salama moyo wako na uukinge kwa bidii zote; kwa kuwa katika moyo hububujika chemichemi za uzima.
הסר ממך עקשות פה ולזות שפתים הרחק ממך׃ | 24 |
Jiepushe na kauli za udanganyifu na ujiepushe na mazungumzo ya ufisadi.
עיניך לנכח יביטו ועפעפיך יישרו נגדך׃ | 25 |
Macho yako yatazame mbele kwa unyoofu na kwa uthabiti tazama mbele sawasawa.
פלס מעגל רגלך וכל דרכיך יכנו׃ | 26 |
Usawazishe pito la mguu wako; na njia zako zote zitakuwa salama.
אל תט ימין ושמאול הסר רגלך מרע׃ | 27 |
Usigeuke upande wa kulia au kushoto; ondoa mguu wako mbali na uovu.