< מִשְׁלֵי 4 >

שמעו בנים מוסר אב והקשיבו לדעת בינה׃ 1
Wanangu, sikilizeni, fundisho la baba, na zingatieni ili mjue maana ya ufahamu.
כי לקח טוב נתתי לכם תורתי אל תעזבו׃ 2
Mimi ninawapa mafundisho mazuri; msiyaache mafundisho yangu.
כי בן הייתי לאבי רך ויחיד לפני אמי׃ 3
Mimi nilikuwa mwana kwa baba yangu, mpole na mtoto pekee kwa mama yangu,
וירני ויאמר לי יתמך דברי לבך שמר מצותי וחיה׃ 4
baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
קנה חכמה קנה בינה אל תשכח ואל תט מאמרי פי׃ 5
Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
אל תעזבה ותשמרך אהבה ותצרך׃ 6
usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
ראשית חכמה קנה חכמה ובכל קנינך קנה בינה׃ 7
Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
סלסלה ותרוממך תכבדך כי תחבקנה׃ 8
Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
תתן לראשך לוית חן עטרת תפארת תמגנך׃ 9
Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
שמע בני וקח אמרי וירבו לך שנות חיים׃ 10
Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
בדרך חכמה הרתיך הדרכתיך במעגלי ישר׃ 11
Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
בלכתך לא יצר צעדך ואם תרוץ לא תכשל׃ 12
Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
החזק במוסר אל תרף נצרה כי היא חייך׃ 13
Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
בארח רשעים אל תבא ואל תאשר בדרך רעים׃ 14
Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
פרעהו אל תעבר בו שטה מעליו ועבור׃ 15
Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
כי לא ישנו אם לא ירעו ונגזלה שנתם אם לא יכשולו׃ 16
Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
כי לחמו לחם רשע ויין חמסים ישתו׃ 17
Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
וארח צדיקים כאור נגה הולך ואור עד נכון היום׃ 18
Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
דרך רשעים כאפלה לא ידעו במה יכשלו׃ 19
Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
בני לדברי הקשיבה לאמרי הט אזנך׃ 20
Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
אל יליזו מעיניך שמרם בתוך לבבך׃ 21
Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.
כי חיים הם למצאיהם ולכל בשרו מרפא׃ 22
Maana maneno yangu ni uzima kwa wenye kuyapata na afya katika mwili wao.
מכל משמר נצר לבך כי ממנו תוצאות חיים׃ 23
Ulinde salama moyo wako na uukinge kwa bidii zote; kwa kuwa katika moyo hububujika chemichemi za uzima.
הסר ממך עקשות פה ולזות שפתים הרחק ממך׃ 24
Jiepushe na kauli za udanganyifu na ujiepushe na mazungumzo ya ufisadi.
עיניך לנכח יביטו ועפעפיך יישרו נגדך׃ 25
Macho yako yatazame mbele kwa unyoofu na kwa uthabiti tazama mbele sawasawa.
פלס מעגל רגלך וכל דרכיך יכנו׃ 26
Usawazishe pito la mguu wako; na njia zako zote zitakuwa salama.
אל תט ימין ושמאול הסר רגלך מרע׃ 27
Usigeuke upande wa kulia au kushoto; ondoa mguu wako mbali na uovu.

< מִשְׁלֵי 4 >