< מִשְׁלֵי 21 >

פלגי מים לב מלך ביד יהוה על כל אשר יחפץ יטנו׃ 1
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
כל דרך איש ישר בעיניו ותכן לבות יהוה׃ 2
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
עשה צדקה ומשפט נבחר ליהוה מזבח׃ 3
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
רום עינים ורחב לב נר רשעים חטאת׃ 4
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
מחשבות חרוץ אך למותר וכל אץ אך למחסור׃ 5
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
פעל אוצרות בלשון שקר הבל נדף מבקשי מות׃ 6
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
שד רשעים יגורם כי מאנו לעשות משפט׃ 7
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
הפכפך דרך איש וזר וזך ישר פעלו׃ 8
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
טוב לשבת על פנת גג מאשת מדונים ובית חבר׃ 9
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
נפש רשע אותה רע לא יחן בעיניו רעהו׃ 10
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
בענש לץ יחכם פתי ובהשכיל לחכם יקח דעת׃ 11
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
משכיל צדיק לבית רשע מסלף רשעים לרע׃ 12
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
אטם אזנו מזעקת דל גם הוא יקרא ולא יענה׃ 13
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
מתן בסתר יכפה אף ושחד בחק חמה עזה׃ 14
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
שמחה לצדיק עשות משפט ומחתה לפעלי און׃ 15
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
אדם תועה מדרך השכל בקהל רפאים ינוח׃ 16
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
איש מחסור אהב שמחה אהב יין ושמן לא יעשיר׃ 17
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
כפר לצדיק רשע ותחת ישרים בוגד׃ 18
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
טוב שבת בארץ מדבר מאשת מדונים וכעס׃ 19
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
אוצר נחמד ושמן בנוה חכם וכסיל אדם יבלענו׃ 20
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
רדף צדקה וחסד ימצא חיים צדקה וכבוד׃ 21
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
עיר גברים עלה חכם וירד עז מבטחה׃ 22
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
שמר פיו ולשונו שמר מצרות נפשו׃ 23
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
זד יהיר לץ שמו עושה בעברת זדון׃ 24
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
תאות עצל תמיתנו כי מאנו ידיו לעשות׃ 25
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
כל היום התאוה תאוה וצדיק יתן ולא יחשך׃ 26
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
זבח רשעים תועבה אף כי בזמה יביאנו׃ 27
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
עד כזבים יאבד ואיש שומע לנצח ידבר׃ 28
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
העז איש רשע בפניו וישר הוא יכין דרכיו׃ 29
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
אין חכמה ואין תבונה ואין עצה לנגד יהוה׃ 30
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
סוס מוכן ליום מלחמה וליהוה התשועה׃ 31
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< מִשְׁלֵי 21 >