< מִשְׁלֵי 21 >
פלגי מים לב מלך ביד יהוה על כל אשר יחפץ יטנו׃ | 1 |
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
כל דרך איש ישר בעיניו ותכן לבות יהוה׃ | 2 |
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
עשה צדקה ומשפט נבחר ליהוה מזבח׃ | 3 |
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
רום עינים ורחב לב נר רשעים חטאת׃ | 4 |
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
מחשבות חרוץ אך למותר וכל אץ אך למחסור׃ | 5 |
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
פעל אוצרות בלשון שקר הבל נדף מבקשי מות׃ | 6 |
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
שד רשעים יגורם כי מאנו לעשות משפט׃ | 7 |
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
הפכפך דרך איש וזר וזך ישר פעלו׃ | 8 |
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
טוב לשבת על פנת גג מאשת מדונים ובית חבר׃ | 9 |
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
נפש רשע אותה רע לא יחן בעיניו רעהו׃ | 10 |
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
בענש לץ יחכם פתי ובהשכיל לחכם יקח דעת׃ | 11 |
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
משכיל צדיק לבית רשע מסלף רשעים לרע׃ | 12 |
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
אטם אזנו מזעקת דל גם הוא יקרא ולא יענה׃ | 13 |
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
מתן בסתר יכפה אף ושחד בחק חמה עזה׃ | 14 |
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
שמחה לצדיק עשות משפט ומחתה לפעלי און׃ | 15 |
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
אדם תועה מדרך השכל בקהל רפאים ינוח׃ | 16 |
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
איש מחסור אהב שמחה אהב יין ושמן לא יעשיר׃ | 17 |
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
כפר לצדיק רשע ותחת ישרים בוגד׃ | 18 |
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
טוב שבת בארץ מדבר מאשת מדונים וכעס׃ | 19 |
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
אוצר נחמד ושמן בנוה חכם וכסיל אדם יבלענו׃ | 20 |
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
רדף צדקה וחסד ימצא חיים צדקה וכבוד׃ | 21 |
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
עיר גברים עלה חכם וירד עז מבטחה׃ | 22 |
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
שמר פיו ולשונו שמר מצרות נפשו׃ | 23 |
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
זד יהיר לץ שמו עושה בעברת זדון׃ | 24 |
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
תאות עצל תמיתנו כי מאנו ידיו לעשות׃ | 25 |
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
כל היום התאוה תאוה וצדיק יתן ולא יחשך׃ | 26 |
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
זבח רשעים תועבה אף כי בזמה יביאנו׃ | 27 |
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
עד כזבים יאבד ואיש שומע לנצח ידבר׃ | 28 |
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
העז איש רשע בפניו וישר הוא יכין דרכיו׃ | 29 |
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
אין חכמה ואין תבונה ואין עצה לנגד יהוה׃ | 30 |
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
סוס מוכן ליום מלחמה וליהוה התשועה׃ | 31 |
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.