< מִשְׁלֵי 20 >
לץ היין המה שכר וכל שגה בו לא יחכם׃ | 1 |
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
נהם ככפיר אימת מלך מתעברו חוטא נפשו׃ | 2 |
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
כבוד לאיש שבת מריב וכל אויל יתגלע׃ | 3 |
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
מחרף עצל לא יחרש ישאל בקציר ואין׃ | 4 |
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
מים עמקים עצה בלב איש ואיש תבונה ידלנה׃ | 5 |
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
רב אדם יקרא איש חסדו ואיש אמונים מי ימצא׃ | 6 |
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
מתהלך בתמו צדיק אשרי בניו אחריו׃ | 7 |
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
מלך יושב על כסא דין מזרה בעיניו כל רע׃ | 8 |
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
מי יאמר זכיתי לבי טהרתי מחטאתי׃ | 9 |
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
אבן ואבן איפה ואיפה תועבת יהוה גם שניהם׃ | 10 |
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
גם במעלליו יתנכר נער אם זך ואם ישר פעלו׃ | 11 |
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
אזן שמעת ועין ראה יהוה עשה גם שניהם׃ | 12 |
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
אל תאהב שנה פן תורש פקח עיניך שבע לחם׃ | 13 |
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
רע רע יאמר הקונה ואזל לו אז יתהלל׃ | 14 |
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
יש זהב ורב פנינים וכלי יקר שפתי דעת׃ | 15 |
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
לקח בגדו כי ערב זר ובעד נכרים חבלהו׃ | 16 |
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
ערב לאיש לחם שקר ואחר ימלא פיהו חצץ׃ | 17 |
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
מחשבות בעצה תכון ובתחבלות עשה מלחמה׃ | 18 |
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
גולה סוד הולך רכיל ולפתה שפתיו לא תתערב׃ | 19 |
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
מקלל אביו ואמו ידעך נרו באישון חשך׃ | 20 |
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
נחלה מבחלת בראשנה ואחריתה לא תברך׃ | 21 |
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
אל תאמר אשלמה רע קוה ליהוה וישע לך׃ | 22 |
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
תועבת יהוה אבן ואבן ומאזני מרמה לא טוב׃ | 23 |
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
מיהוה מצעדי גבר ואדם מה יבין דרכו׃ | 24 |
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
מוקש אדם ילע קדש ואחר נדרים לבקר׃ | 25 |
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
מזרה רשעים מלך חכם וישב עליהם אופן׃ | 26 |
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
נר יהוה נשמת אדם חפש כל חדרי בטן׃ | 27 |
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
חסד ואמת יצרו מלך וסעד בחסד כסאו׃ | 28 |
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
תפארת בחורים כחם והדר זקנים שיבה׃ | 29 |
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
חברות פצע תמריק ברע ומכות חדרי בטן׃ | 30 |
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.