< מִשְׁלֵי 18 >
לתאוה יבקש נפרד בכל תושיה יתגלע׃ | 1 |
Mtu ajitengaye na wengine hufuata matakwa yake mwenyewe; hupiga vita kila shauri jema.
לא יחפץ כסיל בתבונה כי אם בהתגלות לבו׃ | 2 |
Mpumbavu hafurahii ufahamu, bali hufurahia kutangaza maoni yake mwenyewe.
בבוא רשע בא גם בוז ועם קלון חרפה׃ | 3 |
Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia, pamoja na aibu huja lawama.
מים עמקים דברי פי איש נחל נבע מקור חכמה׃ | 4 |
Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji, bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
שאת פני רשע לא טוב להטות צדיק במשפט׃ | 5 |
Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu, au kumnyima haki asiye na hatia.
שפתי כסיל יבאו בריב ופיו למהלמות יקרא׃ | 6 |
Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.
פי כסיל מחתה לו ושפתיו מוקש נפשו׃ | 7 |
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.
דברי נרגן כמתלהמים והם ירדו חדרי בטן׃ | 8 |
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
גם מתרפה במלאכתו אח הוא לבעל משחית׃ | 9 |
Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu.
מגדל עז שם יהוה בו ירוץ צדיק ונשגב׃ | 10 |
Jina la Bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.
הון עשיר קרית עזו וכחומה נשגבה במשכיתו׃ | 11 |
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.
לפני שבר יגבה לב איש ולפני כבוד ענוה׃ | 12 |
Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi, bali unyenyekevu hutangulia heshima.
משיב דבר בטרם ישמע אולת היא לו וכלמה׃ | 13 |
Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza, huo ni upumbavu wake na aibu yake.
רוח איש יכלכל מחלהו ורוח נכאה מי ישאנה׃ | 14 |
Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?
לב נבון יקנה דעת ואזן חכמים תבקש דעת׃ | 15 |
Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa, masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.
מתן אדם ירחיב לו ולפני גדלים ינחנו׃ | 16 |
Zawadi humfungulia njia mtoaji, nayo humleta mbele ya wakuu.
צדיק הראשון בריבו יבא רעהו וחקרו׃ | 17 |
Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi, hadi mwingine ajitokezapo na kumuuliza maswali.
מדינים ישבית הגורל ובין עצומים יפריד׃ | 18 |
Kupiga kura hukomesha mashindano na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.
אח נפשע מקרית עז ומדונים כבריח ארמון׃ | 19 |
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika kuliko mji uliozungushiwa ngome, nayo mabishano ni kama malango ya ngome yenye makomeo.
מפרי פי איש תשבע בטנו תבואת שפתיו ישבע׃ | 20 |
Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake, atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.
מות וחיים ביד לשון ואהביה יאכל פריה׃ | 21 |
Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi, nao waupendao watakula matunda yake.
מצא אשה מצא טוב ויפק רצון מיהוה׃ | 22 |
Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa Bwana.
תחנונים ידבר רש ועשיר יענה עזות׃ | 23 |
Mtu maskini huomba kuhurumiwa bali tajiri hujibu kwa ukali.
איש רעים להתרעע ויש אהב דבק מאח׃ | 24 |
Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu, bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.