< מִשְׁלֵי 17 >
טוב פת חרבה ושלוה בה מבית מלא זבחי ריב׃ | 1 |
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
עבד משכיל ימשל בבן מביש ובתוך אחים יחלק נחלה׃ | 2 |
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
מצרף לכסף וכור לזהב ובחן לבות יהוה׃ | 3 |
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
מרע מקשיב על שפת און שקר מזין על לשון הות׃ | 4 |
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
לעג לרש חרף עשהו שמח לאיד לא ינקה׃ | 5 |
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
עטרת זקנים בני בנים ותפארת בנים אבותם׃ | 6 |
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
לא נאוה לנבל שפת יתר אף כי לנדיב שפת שקר׃ | 7 |
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
אבן חן השחד בעיני בעליו אל כל אשר יפנה ישכיל׃ | 8 |
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
מכסה פשע מבקש אהבה ושנה בדבר מפריד אלוף׃ | 9 |
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
תחת גערה במבין מהכות כסיל מאה׃ | 10 |
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
אך מרי יבקש רע ומלאך אכזרי ישלח בו׃ | 11 |
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
פגוש דב שכול באיש ואל כסיל באולתו׃ | 12 |
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
משיב רעה תחת טובה לא תמיש רעה מביתו׃ | 13 |
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
פוטר מים ראשית מדון ולפני התגלע הריב נטוש׃ | 14 |
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
מצדיק רשע ומרשיע צדיק תועבת יהוה גם שניהם׃ | 15 |
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
למה זה מחיר ביד כסיל לקנות חכמה ולב אין׃ | 16 |
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
בכל עת אהב הרע ואח לצרה יולד׃ | 17 |
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
אדם חסר לב תוקע כף ערב ערבה לפני רעהו׃ | 18 |
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
אהב פשע אהב מצה מגביה פתחו מבקש שבר׃ | 19 |
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
עקש לב לא ימצא טוב ונהפך בלשונו יפול ברעה׃ | 20 |
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
ילד כסיל לתוגה לו ולא ישמח אבי נבל׃ | 21 |
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
לב שמח ייטב גהה ורוח נכאה תיבש גרם׃ | 22 |
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
שחד מחיק רשע יקח להטות ארחות משפט׃ | 23 |
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
את פני מבין חכמה ועיני כסיל בקצה ארץ׃ | 24 |
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
כעס לאביו בן כסיל וממר ליולדתו׃ | 25 |
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
גם ענוש לצדיק לא טוב להכות נדיבים על ישר׃ | 26 |
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
חושך אמריו יודע דעת וקר רוח איש תבונה׃ | 27 |
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
גם אויל מחריש חכם יחשב אטם שפתיו נבון׃ | 28 |
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.