< מִשְׁלֵי 16 >
לאדם מערכי לב ומיהוה מענה לשון׃ | 1 |
Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu, bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana.
כל דרכי איש זך בעיניו ותכן רוחות יהוה׃ | 2 |
Njia zote za mtu huonekana safi machoni pake mwenyewe, bali makusudi hupimwa na Bwana.
גל אל יהוה מעשיך ויכנו מחשבתיך׃ | 3 |
Mkabidhi Bwana lolote ufanyalo, nayo mipango yako itafanikiwa.
כל פעל יהוה למענהו וגם רשע ליום רעה׃ | 4 |
Bwana hufanya kila kitu kwa kusudi lake mwenyewe; hata waovu kwa siku ya maangamizi.
תועבת יהוה כל גבה לב יד ליד לא ינקה׃ | 5 |
Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo. Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.
בחסד ואמת יכפר עון וביראת יהוה סור מרע׃ | 6 |
Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa; kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya.
ברצות יהוה דרכי איש גם אויביו ישלם אתו׃ | 7 |
Njia za mtu zinapompendeza Bwana, huwafanya hata adui zake waishi naye kwa amani.
טוב מעט בצדקה מרב תבואות בלא משפט׃ | 8 |
Afadhali kitu kidogo pamoja na haki kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
לב אדם יחשב דרכו ויהוה יכין צעדו׃ | 9 |
Moyo wa mtu huifikiri njia yake, bali Bwana huelekeza hatua zake.
קסם על שפתי מלך במשפט לא ימעל פיו׃ | 10 |
Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu, wala kinywa chake hakipotoshi haki.
פלס ומאזני משפט ליהוה מעשהו כל אבני כיס׃ | 11 |
Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana; mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye.
תועבת מלכים עשות רשע כי בצדקה יכון כסא׃ | 12 |
Wafalme huchukia sana kutenda maovu, kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki.
רצון מלכים שפתי צדק ודבר ישרים יאהב׃ | 13 |
Wafalme hufurahia midomo ya uaminifu; humthamini mtu asemaye kweli.
חמת מלך מלאכי מות ואיש חכם יכפרנה׃ | 14 |
Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti, bali mtu mwenye hekima ataituliza.
באור פני מלך חיים ורצונו כעב מלקוש׃ | 15 |
Uso wa mfalme ungʼaapo, inamaanisha uhai; upendeleo wake ni kama wingu la mvua wakati wa vuli.
קנה חכמה מה טוב מחרוץ וקנות בינה נבחר מכסף׃ | 16 |
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu, kuchagua ufahamu kuliko fedha!
מסלת ישרים סור מרע שמר נפשו נצר דרכו׃ | 17 |
Njia kuu ya wanyofu huepuka ubaya; yeye aichungaye njia yake, huchunga maisha yake.
לפני שבר גאון ולפני כשלון גבה רוח׃ | 18 |
Kiburi hutangulia maangamizi, roho ya majivuno hutangulia maanguko.
טוב שפל רוח את עניים מחלק שלל את גאים׃ | 19 |
Ni afadhali kuwa mnyenyekevu katika roho miongoni mwa walioonewa kuliko kugawana nyara pamoja na wenye kiburi.
משכיל על דבר ימצא טוב ובוטח ביהוה אשריו׃ | 20 |
Yeyote anayekubali mafundisho hustawi, tena amebarikiwa yeye anayemtumaini Bwana.
לחכם לב יקרא נבון ומתק שפתים יסיף לקח׃ | 21 |
Wenye hekima moyoni huitwa wenye ufahamu, na maneno ya kupendeza huchochea mafundisho.
מקור חיים שכל בעליו ומוסר אולים אולת׃ | 22 |
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wale walio nao, bali upumbavu huleta adhabu kwa wapumbavu.
לב חכם ישכיל פיהו ועל שפתיו יסיף לקח׃ | 23 |
Moyo wa mtu mwenye hekima huongoza kinywa chake, na midomo yake huchochea mafundisho.
צוף דבש אמרי נעם מתוק לנפש ומרפא לעצם׃ | 24 |
Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali, ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa.
יש דרך ישר לפני איש ואחריתה דרכי מות׃ | 25 |
Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu, bali mwisho wake huelekeza mautini.
נפש עמל עמלה לו כי אכף עליו פיהו׃ | 26 |
Shauku ya mfanyakazi humhimiza kufanya kazi; njaa yake humsukuma aendelee.
איש בליעל כרה רעה ועל שפתיו כאש צרבת׃ | 27 |
Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya, maneno yake ni kama moto uunguzao.
איש תהפכות ישלח מדון ונרגן מפריד אלוף׃ | 28 |
Mtu mpotovu huchochea ugomvi, nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu.
איש חמס יפתה רעהו והוליכו בדרך לא טוב׃ | 29 |
Mtu mkali humvuta jirani yake na kumwongoza katika mapito yale mabaya.
עצה עיניו לחשב תהפכות קרץ שפתיו כלה רעה׃ | 30 |
Yeye akonyezaye kwa jicho lake anapanga upotovu; naye akazaye midomo yake amenuia mabaya.
עטרת תפארת שיבה בדרך צדקה תמצא׃ | 31 |
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.
טוב ארך אפים מגבור ומשל ברוחו מלכד עיר׃ | 32 |
Ni afadhali mtu mstahimilivu kuliko shujaa, mtu anayeitawala hasira yake kuliko yule autekaye mji.
בחיק יוטל את הגורל ומיהוה כל משפטו׃ | 33 |
Kura hupigwa kwa siri, lakini kila uamuzi wake hutoka kwa Bwana.