< מִשְׁלֵי 1 >
משלי שלמה בן דוד מלך ישראל׃ | 1 |
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
לדעת חכמה ומוסר להבין אמרי בינה׃ | 2 |
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
לקחת מוסר השכל צדק ומשפט ומישרים׃ | 3 |
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
לתת לפתאים ערמה לנער דעת ומזמה׃ | 4 |
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
ישמע חכם ויוסף לקח ונבון תחבלות יקנה׃ | 5 |
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
להבין משל ומליצה דברי חכמים וחידתם׃ | 6 |
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
יראת יהוה ראשית דעת חכמה ומוסר אוילים בזו׃ | 7 |
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
שמע בני מוסר אביך ואל תטש תורת אמך׃ | 8 |
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
כי לוית חן הם לראשך וענקים לגרגרתיך׃ | 9 |
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
בני אם יפתוך חטאים אל תבא׃ | 10 |
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
אם יאמרו לכה אתנו נארבה לדם נצפנה לנקי חנם׃ | 11 |
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
נבלעם כשאול חיים ותמימים כיורדי בור׃ (Sheol ) | 12 |
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni. (Sheol )
כל הון יקר נמצא נמלא בתינו שלל׃ | 13 |
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
גורלך תפיל בתוכנו כיס אחד יהיה לכלנו׃ | 14 |
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
בני אל תלך בדרך אתם מנע רגלך מנתיבתם׃ | 15 |
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
כי רגליהם לרע ירוצו וימהרו לשפך דם׃ | 16 |
kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni wepesi kumwaga damu.
כי חנם מזרה הרשת בעיני כל בעל כנף׃ | 17 |
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu wakati ndege wote wanakuona!
והם לדמם יארבו יצפנו לנפשתם׃ | 18 |
Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!
כן ארחות כל בצע בצע את נפש בעליו יקח׃ | 19 |
Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila; huuondoa uhai wa wale wenye mali.
חכמות בחוץ תרנה ברחבות תתן קולה׃ | 20 |
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
בראש המיות תקרא בפתחי שערים בעיר אמריה תאמר׃ | 21 |
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
עד מתי פתים תאהבו פתי ולצים לצון חמדו להם וכסילים ישנאו דעת׃ | 22 |
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
תשובו לתוכחתי הנה אביעה לכם רוחי אודיעה דברי אתכם׃ | 23 |
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
יען קראתי ותמאנו נטיתי ידי ואין מקשיב׃ | 24 |
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
ותפרעו כל עצתי ותוכחתי לא אביתם׃ | 25 |
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
גם אני באידכם אשחק אלעג בבא פחדכם׃ | 26 |
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
בבא כשאוה פחדכם ואידכם כסופה יאתה בבא עליכם צרה וצוקה׃ | 27 |
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
אז יקראנני ולא אענה ישחרנני ולא ימצאנני׃ | 28 |
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
תחת כי שנאו דעת ויראת יהוה לא בחרו׃ | 29 |
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
לא אבו לעצתי נאצו כל תוכחתי׃ | 30 |
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
ויאכלו מפרי דרכם וממעצתיהם ישבעו׃ | 31 |
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
כי משובת פתים תהרגם ושלות כסילים תאבדם׃ | 32 |
Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua, nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
ושמע לי ישכן בטח ושאנן מפחד רעה׃ | 33 |
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”