< מִשְׁלֵי 1 >

משלי שלמה בן דוד מלך ישראל׃ 1
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
לדעת חכמה ומוסר להבין אמרי בינה׃ 2
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
לקחת מוסר השכל צדק ומשפט ומישרים׃ 3
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
לתת לפתאים ערמה לנער דעת ומזמה׃ 4
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
ישמע חכם ויוסף לקח ונבון תחבלות יקנה׃ 5
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
להבין משל ומליצה דברי חכמים וחידתם׃ 6
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
יראת יהוה ראשית דעת חכמה ומוסר אוילים בזו׃ 7
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
שמע בני מוסר אביך ואל תטש תורת אמך׃ 8
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
כי לוית חן הם לראשך וענקים לגרגרתיך׃ 9
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
בני אם יפתוך חטאים אל תבא׃ 10
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
אם יאמרו לכה אתנו נארבה לדם נצפנה לנקי חנם׃ 11
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
נבלעם כשאול חיים ותמימים כיורדי בור׃ (Sheol h7585) 12
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni. (Sheol h7585)
כל הון יקר נמצא נמלא בתינו שלל׃ 13
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
גורלך תפיל בתוכנו כיס אחד יהיה לכלנו׃ 14
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
בני אל תלך בדרך אתם מנע רגלך מנתיבתם׃ 15
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
כי רגליהם לרע ירוצו וימהרו לשפך דם׃ 16
kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni wepesi kumwaga damu.
כי חנם מזרה הרשת בעיני כל בעל כנף׃ 17
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu wakati ndege wote wanakuona!
והם לדמם יארבו יצפנו לנפשתם׃ 18
Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!
כן ארחות כל בצע בצע את נפש בעליו יקח׃ 19
Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila; huuondoa uhai wa wale wenye mali.
חכמות בחוץ תרנה ברחבות תתן קולה׃ 20
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
בראש המיות תקרא בפתחי שערים בעיר אמריה תאמר׃ 21
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
עד מתי פתים תאהבו פתי ולצים לצון חמדו להם וכסילים ישנאו דעת׃ 22
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
תשובו לתוכחתי הנה אביעה לכם רוחי אודיעה דברי אתכם׃ 23
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
יען קראתי ותמאנו נטיתי ידי ואין מקשיב׃ 24
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
ותפרעו כל עצתי ותוכחתי לא אביתם׃ 25
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
גם אני באידכם אשחק אלעג בבא פחדכם׃ 26
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
בבא כשאוה פחדכם ואידכם כסופה יאתה בבא עליכם צרה וצוקה׃ 27
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
אז יקראנני ולא אענה ישחרנני ולא ימצאנני׃ 28
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
תחת כי שנאו דעת ויראת יהוה לא בחרו׃ 29
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
לא אבו לעצתי נאצו כל תוכחתי׃ 30
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
ויאכלו מפרי דרכם וממעצתיהם ישבעו׃ 31
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
כי משובת פתים תהרגם ושלות כסילים תאבדם׃ 32
Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua, nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
ושמע לי ישכן בטח ושאנן מפחד רעה׃ 33
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

< מִשְׁלֵי 1 >