< לוּקָס 20 >
ויהי היום והוא מלמד את העם במקדש ומבשר ויגשו הכהנים והסופרים עם הזקנים׃ | 1 |
Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
ויאמרו אליו אמר נא לנו באי זו רשות אתה עשה את אלה או מי הוא הנתן לך את הרשות הזאת׃ | 2 |
Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
ויען ויאמר אליהם אף אני אשאלכם דבר ואמרו לי׃ | 3 |
Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
טבילת יוחנן המן השמים היתה אם מבני אדם׃ | 4 |
Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
ויחשבו בלבם לאמר אם נאמר מן השמים ואמר למה זה לא האמנתם לו׃ | 5 |
Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
ואם נאמר מבני אדם וסקלנו כל העם בעמדם על דעתם כי יוחנן נביא היה׃ | 6 |
Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
ויאמר ישוע אליהם גם אני לא אמר לכם באי זו רשות אני עשה אלה׃ | 8 |
Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
ויחל לדבר אל העם את המשל הזה איש אחד נטע כרם ויתן אתו אל כרמים וילך בדרך מרחוק לימים רבים׃ | 9 |
Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
ולמועד שלח עבד אל הכרמים לתת לו מפרי הכרם והכרמים הכהו וישלחהו ריקם׃ | 10 |
Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
ויסף שלח עבד אחר ויכו גם אתו ויחרפהו וישלחהו ריקם׃ | 11 |
Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
ויסף לשלח שלישי וגם אתו פצעו ויגרשהו וידחפהו חוצה׃ | 12 |
Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
ויאמר בעל הכרם מה אעשה אשלחה את בני את ידידי כראותם אותו אולי יגורו מפניו׃ | 13 |
“Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
וכראות אתו הכרמים נועצו יחדו לאמר זה הוא היורש לכו ונהרגהו ותהי לנו הירשה׃ | 14 |
“Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
ויגרשו אותו אל מחוץ לכרם ויהרגהו ועתה מה יעשה להם בעל הכרם׃ | 15 |
Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
יבוא ויאבד את הכרמים האלה ויתן את הכרם לאחרים ויהי כשמעם ויאמרו חלילה מהיות כזאת׃ | 16 |
Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
ויבט בם ויאמר ומה הוא זה הכתוב אבן מאסו הבונים היתה לראש פנה׃ | 17 |
Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
כל הנפל על האבן ההיא ישבר ואת אשר תפל עליו תשחקהו׃ | 18 |
Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
ויבקשו הכהנים הגדולים והסופרים לשלח בו את ידם בעת ההיא וייראו מפני העם כי ידעו אשר עליהם דבר את המשל הזה׃ | 19 |
Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
ויארבו לו וישלחו מארבים והם נדמו כצדיקים למען ילכדו אותו בדבר להסגירו אל השררה ואל יד ההגמון׃ | 20 |
Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
וישאלהו לאמר רבי ידענו כי נכונה תדבר ותלמד ולא תשא פנים כי באמת מורה אתה את דרך אלהים׃ | 21 |
Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
המתר לנו לתת מס אל הקיסר אם לא׃ | 22 |
Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
ויכר את נכליהם ויאמר להם׃ | 23 |
Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
מה תנסוני הראוני דינר של מי הצורה והמכתב אשר עליו ויענו ויאמרו של הקיסר׃ | 24 |
“Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
ויאמר אליהם לכן תנו לקיסר את אשר לקיסר ולאלהים את אשר לאלהים׃ | 25 |
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
ולא יכלו ללכדו בדבר לפני העם ויתמהו על מענהו ויחרישו׃ | 26 |
Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
ויקרבו אנשים מן הצדוקים הכפרים בתחית המתים וישאלהו לאמר׃ | 27 |
Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
מורה משה כתב לנו כי ימות אח בעל אשה ובנים אין לו ולקח אחיו את אשתו והקים זרע לאחיו׃ | 28 |
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
והנה היו שבעה אחים והראשון לקח אשה וימת לא בנים׃ | 29 |
Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
ויקח אתה השני וימת גם הוא לא בנים׃ | 30 |
Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
ויקח אתה השלישי וככה עשו אף השבעה ולא הניחו בנים וימותו׃ | 31 |
naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
והנה בתחית המתים למי מהם תהיה לאשה כי היתה אשה לשבעה׃ | 33 |
Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
ויען ישוע ויאמר אליהם בני העולם הזה ישאו נשים ותנשאנה׃ (aiōn ) | 34 |
Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn )
והזכים לנחל את העולם הבא ואת תחית המתים לא ישאו נשים ולא תנשאנה׃ (aiōn ) | 35 |
Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn )
כי לא יוכלו עוד למות כי שוים הם למלאכים ובני אלהים המה בהיותם בני התקומה׃ | 36 |
Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
וגם משה רמז בסנה כי יקומו המתים בקראו את יהוה אלהי אברהם אלהי יצחק ואלהי יעקב׃ | 37 |
Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
והאלהים איננו אלהי המתים כי אם אלהי החיים כי כלם חיים לו׃ | 38 |
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
ויענו מן הסופרים רבי יפה דברת׃ | 39 |
Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
ולא ערבו עוד את לבם לשאל אותו דבר׃ | 40 |
Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
ויאמר אליהם איך יאמרו על המשיח כי הוא בן דוד׃ | 41 |
Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
והוא דוד אמר בספר תהלים נאם יהוה לאדני שב לימיני׃ | 42 |
Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
עד אשית איביך הדם לרגליך׃ | 43 |
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
הנה דוד קרא לו אדון ואיך הוא בנו׃ | 44 |
Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
ויאמר אל תלמידיו באזני כל העם׃ | 45 |
Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
הזהרו מן הסופרים החפצים להתהלך עטופי טלית ואהבים את שאלות שלומם בשוקים ואת מושבי הראש בבתי הכנסיות ואת מסבות הראש בסעודות׃ | 46 |
“Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
הבלעים את בתי האלמנות ומאריכים תפלתם למראה עינים המה משפט על יתר יקחו׃ | 47 |
Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”