< איכה 5 >

זכר יהוה מה היה לנו הביט וראה את חרפתנו׃ 1
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
נחלתנו נהפכה לזרים בתינו לנכרים׃ 2
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
יתומים היינו אין אב אמתינו כאלמנות׃ 3
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
מימינו בכסף שתינו עצינו במחיר יבאו׃ 4
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
על צוארנו נרדפנו יגענו לא הונח לנו׃ 5
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
מצרים נתנו יד אשור לשבע לחם׃ 6
Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
אבתינו חטאו אינם אנחנו עונתיהם סבלנו׃ 7
Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
עבדים משלו בנו פרק אין מידם׃ 8
Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
בנפשנו נביא לחמנו מפני חרב המדבר׃ 9
Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
עורנו כתנור נכמרו מפני זלעפות רעב׃ 10
Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
נשים בציון ענו בתלת בערי יהודה׃ 11
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
שרים בידם נתלו פני זקנים לא נהדרו׃ 12
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
בחורים טחון נשאו ונערים בעץ כשלו׃ 13
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
זקנים משער שבתו בחורים מנגינתם׃ 14
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
שבת משוש לבנו נהפך לאבל מחלנו׃ 15
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
נפלה עטרת ראשנו אוי נא לנו כי חטאנו׃ 16
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
על זה היה דוה לבנו על אלה חשכו עינינו׃ 17
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
על הר ציון ששמם שועלים הלכו בו׃ 18
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
אתה יהוה לעולם תשב כסאך לדר ודור׃ 19
Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
למה לנצח תשכחנו תעזבנו לארך ימים׃ 20
Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
השיבנו יהוה אליך ונשוב חדש ימינו כקדם׃ 21
Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
כי אם מאס מאסתנו קצפת עלינו עד מאד׃ 22
isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.

< איכה 5 >