< איכה 5 >
זכר יהוה מה היה לנו הביט וראה את חרפתנו׃ | 1 |
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
נחלתנו נהפכה לזרים בתינו לנכרים׃ | 2 |
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
יתומים היינו אין אב אמתינו כאלמנות׃ | 3 |
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
מימינו בכסף שתינו עצינו במחיר יבאו׃ | 4 |
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
על צוארנו נרדפנו יגענו לא הונח לנו׃ | 5 |
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
מצרים נתנו יד אשור לשבע לחם׃ | 6 |
Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
אבתינו חטאו אינם אנחנו עונתיהם סבלנו׃ | 7 |
Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
עבדים משלו בנו פרק אין מידם׃ | 8 |
Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
בנפשנו נביא לחמנו מפני חרב המדבר׃ | 9 |
Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
עורנו כתנור נכמרו מפני זלעפות רעב׃ | 10 |
Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
נשים בציון ענו בתלת בערי יהודה׃ | 11 |
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
שרים בידם נתלו פני זקנים לא נהדרו׃ | 12 |
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
בחורים טחון נשאו ונערים בעץ כשלו׃ | 13 |
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
זקנים משער שבתו בחורים מנגינתם׃ | 14 |
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
שבת משוש לבנו נהפך לאבל מחלנו׃ | 15 |
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
נפלה עטרת ראשנו אוי נא לנו כי חטאנו׃ | 16 |
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
על זה היה דוה לבנו על אלה חשכו עינינו׃ | 17 |
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
על הר ציון ששמם שועלים הלכו בו׃ | 18 |
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
אתה יהוה לעולם תשב כסאך לדר ודור׃ | 19 |
Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
למה לנצח תשכחנו תעזבנו לארך ימים׃ | 20 |
Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
השיבנו יהוה אליך ונשוב חדש ימינו כקדם׃ | 21 |
Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
כי אם מאס מאסתנו קצפת עלינו עד מאד׃ | 22 |
isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.