< יהושע 19 >

ויצא הגורל השני לשמעון למטה בני שמעון למשפחותם ויהי נחלתם בתוך נחלת בני יהודה׃ 1
Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
ויהי להם בנחלתם באר שבע ושבע ומולדה׃ 2
Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
וחצר שועל ובלה ועצם׃ 3
Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
ואלתולד ובתול וחרמה׃ 4
Elitoladi, Bethuli na Horma.
וצקלג ובית המרכבות וחצר סוסה׃ 5
Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
ובית לבאות ושרוחן ערים שלש עשרה וחצריהן׃ 6
Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
עין רמון ועתר ועשן ערים ארבע וחצריהן׃ 7
Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
וכל החצרים אשר סביבות הערים האלה עד בעלת באר ראמת נגב זאת נחלת מטה בני שמעון למשפחתם׃ 8
Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
מחבל בני יהודה נחלת בני שמעון כי היה חלק בני יהודה רב מהם וינחלו בני שמעון בתוך נחלתם׃ 9
Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
ויעל הגורל השלישי לבני זבולן למשפחתם ויהי גבול נחלתם עד שריד׃ 10
Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
ועלה גבולם לימה ומרעלה ופגע בדבשת ופגע אל הנחל אשר על פני יקנעם׃ 11
Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
ושב משריד קדמה מזרח השמש על גבול כסלת תבר ויצא אל הדברת ועלה יפיע׃ 12
Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
ומשם עבר קדמה מזרחה גתה חפר עתה קצין ויצא רמון המתאר הנעה׃ 13
Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
ונסב אתו הגבול מצפון חנתן והיו תצאתיו גי יפתח אל׃ 14
Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
וקטת ונהלל ושמרון וידאלה ובית לחם ערים שתים עשרה וחצריהן׃ 15
Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
זאת נחלת בני זבולן למשפחותם הערים האלה וחצריהן׃ 16
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
ליששכר יצא הגורל הרביעי לבני יששכר למשפחותם׃ 17
Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
ויהי גבולם יזרעאלה והכסולת ושונם׃ 18
Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
וחפרים ושיאן ואנחרת׃ 19
Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
והרבית וקשיון ואבץ׃ 20
Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
ורמת ועין גנים ועין חדה ובית פצץ׃ 21
Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
ופגע הגבול בתבור ושחצומה ובית שמש והיו תצאות גבולם הירדן ערים שש עשרה וחצריהן׃ 22
Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
זאת נחלת מטה בני יששכר למשפחתם הערים וחצריהן׃ 23
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
ויצא הגורל החמישי למטה בני אשר למשפחותם׃ 24
Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
ויהי גבולם חלקת וחלי ובטן ואכשף׃ 25
Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
ואלמלך ועמעד ומשאל ופגע בכרמל הימה ובשיחור לבנת׃ 26
Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
ושב מזרח השמש בית דגן ופגע בזבלון ובגי יפתח אל צפונה בית העמק ונעיאל ויצא אל כבול משמאל׃ 27
Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
ועברן ורחב וחמון וקנה עד צידון רבה׃ 28
Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
ושב הגבול הרמה ועד עיר מבצר צר ושב הגבול חסה ויהיו תצאתיו הימה מחבל אכזיבה׃ 29
Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
ועמה ואפק ורחב ערים עשרים ושתים וחצריהן׃ 30
Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
זאת נחלת מטה בני אשר למשפחתם הערים האלה וחצריהן׃ 31
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
לבני נפתלי יצא הגורל הששי לבני נפתלי למשפחתם׃ 32
Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
ויהי גבולם מחלף מאלון בצעננים ואדמי הנקב ויבנאל עד לקום ויהי תצאתיו הירדן׃ 33
Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
ושב הגבול ימה אזנות תבור ויצא משם חוקקה ופגע בזבלון מנגב ובאשר פגע מים וביהודה הירדן מזרח השמש׃ 34
Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
וערי מבצר הצדים צר וחמת רקת וכנרת׃ 35
Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
ואדמה והרמה וחצור׃ 36
Adama, Rama, Hazori,
וקדש ואדרעי ועין חצור׃ 37
Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
ויראון ומגדל אל חרם ובית ענת ובית שמש ערים תשע עשרה וחצריהן׃ 38
Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
זאת נחלת מטה בני נפתלי למשפחתם הערים וחצריהן׃ 39
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
למטה בני דן למשפחתם יצא הגורל השביעי׃ 40
Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
ויהי גבול נחלתם צרעה ואשתאול ועיר שמש׃ 41
Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
ושעלבין ואילון ויתלה׃ 42
Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
ואילון ותמנתה ועקרון׃ 43
Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
ואלתקה וגבתון ובעלת׃ 44
Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
ויהד ובני ברק וגת רמון׃ 45
Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
ומי הירקון והרקון עם הגבול מול יפו׃ 46
Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
ויצא גבול בני דן מהם ויעלו בני דן וילחמו עם לשם וילכדו אותה ויכו אותה לפי חרב וירשו אותה וישבו בה ויקראו ללשם דן כשם דן אביהם׃ 47
Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
זאת נחלת מטה בני דן למשפחתם הערים האלה וחצריהן׃ 48
Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
ויכלו לנחל את הארץ לגבולתיה ויתנו בני ישראל נחלה ליהושע בן נון בתוכם׃ 49
Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
על פי יהוה נתנו לו את העיר אשר שאל את תמנת סרח בהר אפרים ויבנה את העיר וישב בה׃ 50
Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
אלה הנחלת אשר נחלו אלעזר הכהן ויהושע בן נון וראשי האבות למטות בני ישראל בגורל בשלה לפני יהוה פתח אהל מועד ויכלו מחלק את הארץ׃ 51
Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.

< יהושע 19 >