< ג'ון 12 >

וששת ימים לפני חג הפסח בא ישוע לבית היני מקום לעזר אשר העיר אתו מעם המתים׃ 1
Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
ויעשו לו שם משתה בערב ומרתא משרתת ולעזר היה אחד מן המסבים אתו׃ 2
Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
ותקח מרים מרקחת נרד זך ויקר מאד לטרא אחת משקלה ותמשח בה את רגלי ישוע ותנגב את רגליו בשערותיה והבית ימלא ריח המרקחת׃ 3
Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
ויאמר אחד מתלמידיו הוא יהודה בן שמעון איש קריות העתיד למסרו׃ 4
Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
מדוע לא נמכרה המרקחת בשלש מאות דינר ונתן לעניים׃ 5
“Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
והוא לא דבר את זאת מחמלתו על העניים כי אם גנב היה וכיס הכסף אתו וישא כל אשר ישימו בו׃ 6
Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
ויאמר ישוע הניחה לה ליום קבורתי צפנה זאת׃ 7
Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
כי העניים תמיד המה עמכם ואני אינני תמיד עמכם׃ 8
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
וישמעו עם רב ביהודה כי שם הוא ויבאו לא בעבור ישוע לבדו כי אם לראות גם את לעזר אשר העירו מעם המתים׃ 9
Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
וראשי הכהנים התיעצו להרג גם את לעזר׃ 10
Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
כי בגללו באו שמה רבים מן היהודים ויאמינו בישוע׃ 11
kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
ויהי ממחרת כשמוע המון רב אשר באו לחג החג כי יבא ישוע ירושלים׃ 12
Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
ויקחו בידם כפות תמרים ויצאו לקראתו ויריעו לאמר הושע נא ברוך הבא בשם יהוה מלך ישראל׃ 13
Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
וימצא ישוע עיר אחד וירכב עליו כאשר כתוב׃ 14
Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
אל תיראי בת ציון הנה מלכך יבוא לך רכב על עיר בן אתנות׃ 15
“Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
וכל זאת לא הבינו תלמידיו בראשונה אך אחרי אשר נתפאר ישוע זכרו כי כן כתוב עליו וכי זאת עשו לו׃ 16
Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
ויעידו העם אשר היו אצלו בקראו אל לעזר לצאת מן הקבר ויער אתו מעם המתים׃ 17
Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
על זאת גם המון העם יצא לקראתו על שמעם כי עשה האות הזה׃ 18
Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
והפרושים דברו איש את אחיו לאמר הראיתם כי הועיל לא תועילו מאומה הנה כל העולם נמשך אחריו׃ 19
Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
ובתוך העלים להשתחות בחג היו אנשים יונים׃ 20
Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
ויקרבו אל פילפוס איש בית צידה אשר בארץ הגליל וישאלו ממנו לאמר אדני לראות את ישוע חפצנו׃ 21
Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
ויבא פילפוס ויגד זאת אל אנדרי ואנדרי ופילפוס הגידו אל ישוע׃ 22
Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
ויען אותם ישוע ויאמר באה השעה שיפאר בן האדם׃ 23
Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
אמן אמן אני אמר לכם אם לא יפל גרגר החטא אל תוך האדמה ומת ישאר לבדו וכאשר מת יעשה פרי הרבה׃ 24
Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
האהב את נפשו יאבדנה והשנא את נפשו בעולם הזה ינצרה לחיי נצח׃ (aiōnios g166) 25
Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios g166)
החפץ לשרתני ילך אחרי ובאשר אהיה שם יהיה גם משרתי ואיש אשר ישרתני אתו יכבד אבי׃ 26
Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
עתה נבהלה נפשי ומה אמר הושיעני אבי מן השעה הזאת אך על כן באתי אל השעה הזאת׃ 27
“Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
אבי פאר את שמך ותצא בת קול מן השמים גם פארתי וגם אוסיף לפאר׃ 28
Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
והעם העמדים שמה כשמעם אמרו רעם נשמע ואחרים אמרו מלאך דבר אתו׃ 29
Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
ויען ישוע ויאמר לא למעני היה הקול הזה כי אם למענכם׃ 30
Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
עתה משפט בא על העולם הזה עתה ישלך שר העולם הזה חוצה׃ 31
Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
ואני בהנשאי מעל הארץ אמשך כלם אלי׃ 32
Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
וזאת דבר לרמוז אי זה מות הוא עתיד למות׃ 33
Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
ויענו אתו העם ויאמרו הנה שמענו בתורה כי המשיח יכון לעולם ואיך אמרת כי בן האדם צריך להנשא ומי בן האדם הלזה׃ (aiōn g165) 34
Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn g165)
ויאמר אליהם ישוע אך למצער יהיה האור עמכם התהלכו בעוד לכם האור פן ישופכם חשך וההלך בחשך לא ידע אנה הוא הלך׃ 35
Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
בעוד לכם האור האמינו באור למען תהיו בני האור את הדברים האלה דבר ישוע וילך לו ויסתר מפניהם׃ 36
Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
רבים האתות אשר עשה לעיניהם ובכל זאת לא האמינו בו׃ 37
Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
למלאת דבר ישעיהו הנביא אשר אמר יהוה מי האמין לשמעתנו וזרוע יהוה על מי נגלתה׃ 38
Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
על כן לא יכלו להאמין כי עוד אמר ישעיהו׃ 39
Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
השע עיניהם והשמין לבבם פן יראו בעיניהם ולבבם יבין ושבו ורפאתי להם׃ 40
“Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
כזאת דבר ישעיהו בראותו את תפארתו וינבא עליו׃ 41
Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
אולם רבים אף מן השרים האמינו בו אך בגלל הפרושים לא הודו למען אשר לא ינדו׃ 42
Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
כי אהבו כבוד אנשים יותר מכבוד האלהים׃ 43
Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
ויקרא ישוע ויאמר המאמין בי לא בי הוא מאמין כי אם בשלח אתי׃ 44
Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
והראה אתי את אשר שלחני הוא ראה׃ 45
Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
אני באתי לאור אל העולם למען כל אשר יאמין בי לא ישב בחשך׃ 46
Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
והשמע את דברי ולא ישמרם אני לא אשפט אתו כי לא באתי לשפט את העולם כי אם להושיע את העולם׃ 47
“Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
ואיש אשר יבזני ולא יקח אמרי יש אחד אשר ידין אתו הדבר אשר דברתי הוא ידין אתו ביום האחרון׃ 48
Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
כי אני לא מלבי דברתי כי אם אבי השלח אתי הוא צוני את אשר אמר ואת אשר אדבר׃ 49
Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
ואני ידעתי כי מצותו חיי עולם לכן כל אשר אדבר כאשר אמר אלי אבי כן אני מדבר׃ (aiōnios g166) 50
Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios g166)

< ג'ון 12 >