< איוב 6 >

ויען איוב ויאמר׃ 1
Kisha Ayubu akajibu:
לו שקול ישקל כעשי והיתי במאזנים ישאו יחד׃ 2
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
כי עתה מחול ימים יכבד על כן דברי לעו׃ 3
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
כי חצי שדי עמדי אשר חמתם שתה רוחי בעותי אלוה יערכוני׃ 4
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
הינהק פרא עלי דשא אם יגעה שור על בלילו׃ 5
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
היאכל תפל מבלי מלח אם יש טעם בריר חלמות׃ 6
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
מאנה לנגוע נפשי המה כדוי לחמי׃ 7
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
מי יתן תבוא שאלתי ותקותי יתן אלוה׃ 8
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
ויאל אלוה וידכאני יתר ידו ויבצעני׃ 9
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
ותהי עוד נחמתי ואסלדה בחילה לא יחמול כי לא כחדתי אמרי קדוש׃ 10
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
מה כחי כי איחל ומה קצי כי אאריך נפשי׃ 11
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
אם כח אבנים כחי אם בשרי נחוש׃ 12
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
האם אין עזרתי בי ותשיה נדחה ממני׃ 13
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
למס מרעהו חסד ויראת שדי יעזוב׃ 14
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
אחי בגדו כמו נחל כאפיק נחלים יעברו׃ 15
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
הקדרים מני קרח עלימו יתעלם שלג׃ 16
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
בעת יזרבו נצמתו בחמו נדעכו ממקומם׃ 17
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
ילפתו ארחות דרכם יעלו בתהו ויאבדו׃ 18
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
הביטו ארחות תמא הליכת שבא קוו למו׃ 19
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
בשו כי בטח באו עדיה ויחפרו׃ 20
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
כי עתה הייתם לא תראו חתת ותיראו׃ 21
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
הכי אמרתי הבו לי ומכחכם שחדו בעדי׃ 22
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
ומלטוני מיד צר ומיד עריצים תפדוני׃ 23
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
הורוני ואני אחריש ומה שגיתי הבינו לי׃ 24
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
מה נמרצו אמרי ישר ומה יוכיח הוכח מכם׃ 25
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
הלהוכח מלים תחשבו ולרוח אמרי נאש׃ 26
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
אף על יתום תפילו ותכרו על ריעכם׃ 27
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
ועתה הואילו פנו בי ועל פניכם אם אכזב׃ 28
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
שבו נא אל תהי עולה ושבי עוד צדקי בה׃ 29
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
היש בלשוני עולה אם חכי לא יבין הוות׃ 30
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< איוב 6 >