< איוב 6 >
לו שקול ישקל כעשי והיתי במאזנים ישאו יחד׃ | 2 |
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
כי עתה מחול ימים יכבד על כן דברי לעו׃ | 3 |
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
כי חצי שדי עמדי אשר חמתם שתה רוחי בעותי אלוה יערכוני׃ | 4 |
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
הינהק פרא עלי דשא אם יגעה שור על בלילו׃ | 5 |
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
היאכל תפל מבלי מלח אם יש טעם בריר חלמות׃ | 6 |
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
מאנה לנגוע נפשי המה כדוי לחמי׃ | 7 |
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
מי יתן תבוא שאלתי ותקותי יתן אלוה׃ | 8 |
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
ויאל אלוה וידכאני יתר ידו ויבצעני׃ | 9 |
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
ותהי עוד נחמתי ואסלדה בחילה לא יחמול כי לא כחדתי אמרי קדוש׃ | 10 |
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
מה כחי כי איחל ומה קצי כי אאריך נפשי׃ | 11 |
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
אם כח אבנים כחי אם בשרי נחוש׃ | 12 |
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
האם אין עזרתי בי ותשיה נדחה ממני׃ | 13 |
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
למס מרעהו חסד ויראת שדי יעזוב׃ | 14 |
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
אחי בגדו כמו נחל כאפיק נחלים יעברו׃ | 15 |
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
הקדרים מני קרח עלימו יתעלם שלג׃ | 16 |
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
בעת יזרבו נצמתו בחמו נדעכו ממקומם׃ | 17 |
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
ילפתו ארחות דרכם יעלו בתהו ויאבדו׃ | 18 |
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
הביטו ארחות תמא הליכת שבא קוו למו׃ | 19 |
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
בשו כי בטח באו עדיה ויחפרו׃ | 20 |
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
כי עתה הייתם לא תראו חתת ותיראו׃ | 21 |
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
הכי אמרתי הבו לי ומכחכם שחדו בעדי׃ | 22 |
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
ומלטוני מיד צר ומיד עריצים תפדוני׃ | 23 |
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
הורוני ואני אחריש ומה שגיתי הבינו לי׃ | 24 |
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
מה נמרצו אמרי ישר ומה יוכיח הוכח מכם׃ | 25 |
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
הלהוכח מלים תחשבו ולרוח אמרי נאש׃ | 26 |
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
אף על יתום תפילו ותכרו על ריעכם׃ | 27 |
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
ועתה הואילו פנו בי ועל פניכם אם אכזב׃ | 28 |
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
שבו נא אל תהי עולה ושבי עוד צדקי בה׃ | 29 |
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
היש בלשוני עולה אם חכי לא יבין הוות׃ | 30 |
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?