< איוב 5 >
קרא נא היש עונך ואל מי מקדשים תפנה׃ | 1 |
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
כי לאויל יהרג כעש ופתה תמית קנאה׃ | 2 |
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
אני ראיתי אויל משריש ואקוב נוהו פתאם׃ | 3 |
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
ירחקו בניו מישע וידכאו בשער ואין מציל׃ | 4 |
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
אשר קצירו רעב יאכל ואל מצנים יקחהו ושאף צמים חילם׃ | 5 |
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
כי לא יצא מעפר און ומאדמה לא יצמח עמל׃ | 6 |
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
כי אדם לעמל יולד ובני רשף יגביהו עוף׃ | 7 |
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
אולם אני אדרש אל אל ואל אלהים אשים דברתי׃ | 8 |
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
עשה גדלות ואין חקר נפלאות עד אין מספר׃ | 9 |
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
הנתן מטר על פני ארץ ושלח מים על פני חוצות׃ | 10 |
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
לשום שפלים למרום וקדרים שגבו ישע׃ | 11 |
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
מפר מחשבות ערומים ולא תעשינה ידיהם תושיה׃ | 12 |
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
לכד חכמים בערמם ועצת נפתלים נמהרה׃ | 13 |
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
יומם יפגשו חשך וכלילה ימששו בצהרים׃ | 14 |
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
וישע מחרב מפיהם ומיד חזק אביון׃ | 15 |
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
ותהי לדל תקוה ועלתה קפצה פיה׃ | 16 |
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
הנה אשרי אנוש יוכחנו אלוה ומוסר שדי אל תמאס׃ | 17 |
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
כי הוא יכאיב ויחבש ימחץ וידו תרפינה׃ | 18 |
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
בשש צרות יצילך ובשבע לא יגע בך רע׃ | 19 |
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
ברעב פדך ממות ובמלחמה מידי חרב׃ | 20 |
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
בשוט לשון תחבא ולא תירא משד כי יבוא׃ | 21 |
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
לשד ולכפן תשחק ומחית הארץ אל תירא׃ | 22 |
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
כי עם אבני השדה בריתך וחית השדה השלמה לך׃ | 23 |
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
וידעת כי שלום אהלך ופקדת נוך ולא תחטא׃ | 24 |
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
וידעת כי רב זרעך וצאצאיך כעשב הארץ׃ | 25 |
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
תבוא בכלח אלי קבר כעלות גדיש בעתו׃ | 26 |
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
הנה זאת חקרנוה כן היא שמענה ואתה דע לך׃ | 27 |
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”