< איוב 40 >

ויען יהוה את איוב ויאמר׃ 1
Bwana akamwambia Ayubu:
הרב עם שדי יסור מוכיח אלוה יעננה׃ 2
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
ויען איוב את יהוה ויאמר׃ 3
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
הן קלתי מה אשיבך ידי שמתי למו פי׃ 4
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
אחת דברתי ולא אענה ושתים ולא אוסיף׃ 5
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
ויען יהוה את איוב מן סערה ויאמר׃ 6
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
אזר נא כגבר חלציך אשאלך והודיעני׃ 7
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
האף תפר משפטי תרשיעני למען תצדק׃ 8
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
ואם זרוע כאל לך ובקול כמהו תרעם׃ 9
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
עדה נא גאון וגבה והוד והדר תלבש׃ 10
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
הפץ עברות אפך וראה כל גאה והשפילהו׃ 11
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
ראה כל גאה הכניעהו והדך רשעים תחתם׃ 12
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
טמנם בעפר יחד פניהם חבש בטמון׃ 13
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
וגם אני אודך כי תושע לך ימינך׃ 14
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
הנה נא בהמות אשר עשיתי עמך חציר כבקר יאכל׃ 15
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
הנה נא כחו במתניו ואנו בשרירי בטנו׃ 16
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
יחפץ זנבו כמו ארז גידי פחדו ישרגו׃ 17
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
עצמיו אפיקי נחושה גרמיו כמטיל ברזל׃ 18
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
הוא ראשית דרכי אל העשו יגש חרבו׃ 19
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
כי בול הרים ישאו לו וכל חית השדה ישחקו שם׃ 20
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
תחת צאלים ישכב בסתר קנה ובצה׃ 21
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
יסכהו צאלים צללו יסבוהו ערבי נחל׃ 22
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
הן יעשק נהר לא יחפוז יבטח כי יגיח ירדן אל פיהו׃ 23
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
בעיניו יקחנו במוקשים ינקב אף׃ 24
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< איוב 40 >