< איוב 40 >
ויען יהוה את איוב ויאמר׃ | 1 |
Bwana akamwambia Ayubu:
הרב עם שדי יסור מוכיח אלוה יעננה׃ | 2 |
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
ויען איוב את יהוה ויאמר׃ | 3 |
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
הן קלתי מה אשיבך ידי שמתי למו פי׃ | 4 |
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
אחת דברתי ולא אענה ושתים ולא אוסיף׃ | 5 |
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
ויען יהוה את איוב מן סערה ויאמר׃ | 6 |
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
אזר נא כגבר חלציך אשאלך והודיעני׃ | 7 |
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
האף תפר משפטי תרשיעני למען תצדק׃ | 8 |
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
ואם זרוע כאל לך ובקול כמהו תרעם׃ | 9 |
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
עדה נא גאון וגבה והוד והדר תלבש׃ | 10 |
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
הפץ עברות אפך וראה כל גאה והשפילהו׃ | 11 |
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
ראה כל גאה הכניעהו והדך רשעים תחתם׃ | 12 |
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
טמנם בעפר יחד פניהם חבש בטמון׃ | 13 |
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
וגם אני אודך כי תושע לך ימינך׃ | 14 |
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
הנה נא בהמות אשר עשיתי עמך חציר כבקר יאכל׃ | 15 |
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
הנה נא כחו במתניו ואנו בשרירי בטנו׃ | 16 |
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
יחפץ זנבו כמו ארז גידי פחדו ישרגו׃ | 17 |
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
עצמיו אפיקי נחושה גרמיו כמטיל ברזל׃ | 18 |
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
הוא ראשית דרכי אל העשו יגש חרבו׃ | 19 |
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
כי בול הרים ישאו לו וכל חית השדה ישחקו שם׃ | 20 |
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
תחת צאלים ישכב בסתר קנה ובצה׃ | 21 |
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
יסכהו צאלים צללו יסבוהו ערבי נחל׃ | 22 |
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
הן יעשק נהר לא יחפוז יבטח כי יגיח ירדן אל פיהו׃ | 23 |
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
בעיניו יקחנו במוקשים ינקב אף׃ | 24 |
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?