< איוב 39 >
הידעת עת לדת יעלי סלע חלל אילות תשמר׃ | 1 |
“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
תספר ירחים תמלאנה וידעת עת לדתנה׃ | 2 |
Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
תכרענה ילדיהן תפלחנה חבליהם תשלחנה׃ | 3 |
Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
יחלמו בניהם ירבו בבר יצאו ולא שבו למו׃ | 4 |
Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
מי שלח פרא חפשי ומסרות ערוד מי פתח׃ | 5 |
“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
אשר שמתי ערבה ביתו ומשכנותיו מלחה׃ | 6 |
Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
ישחק להמון קריה תשאות נוגש לא ישמע׃ | 7 |
Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
יתור הרים מרעהו ואחר כל ירוק ידרוש׃ | 8 |
Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
היאבה רים עבדך אם ילין על אבוסך׃ | 9 |
“Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
התקשר רים בתלם עבתו אם ישדד עמקים אחריך׃ | 10 |
Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
התבטח בו כי רב כחו ותעזב אליו יגיעך׃ | 11 |
Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
התאמין בו כי ישוב זרעך וגרנך יאסף׃ | 12 |
Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
כנף רננים נעלסה אם אברה חסידה ונצה׃ | 13 |
“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
כי תעזב לארץ בציה ועל עפר תחמם׃ | 14 |
Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
ותשכח כי רגל תזורה וחית השדה תדושה׃ | 15 |
bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
הקשיח בניה ללא לה לריק יגיעה בלי פחד׃ | 16 |
Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
כי השה אלוה חכמה ולא חלק לה בבינה׃ | 17 |
kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
כעת במרום תמריא תשחק לסוס ולרכבו׃ | 18 |
Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
התתן לסוס גבורה התלביש צוארו רעמה׃ | 19 |
“Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
התרעישנו כארבה הוד נחרו אימה׃ | 20 |
Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
יחפרו בעמק וישיש בכח יצא לקראת נשק׃ | 21 |
Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
ישחק לפחד ולא יחת ולא ישוב מפני חרב׃ | 22 |
Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
עליו תרנה אשפה להב חנית וכידון׃ | 23 |
Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
ברעש ורגז יגמא ארץ ולא יאמין כי קול שופר׃ | 24 |
Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
בדי שפר יאמר האח ומרחוק יריח מלחמה רעם שרים ותרועה׃ | 25 |
Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
המבינתך יאבר נץ יפרש כנפו לתימן׃ | 26 |
“Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
אם על פיך יגביה נשר וכי ירים קנו׃ | 27 |
Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
סלע ישכן ויתלנן על שן סלע ומצודה׃ | 28 |
Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
משם חפר אכל למרחוק עיניו יביטו׃ | 29 |
Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
ואפרחו יעלעו דם ובאשר חללים שם הוא׃ | 30 |
Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”