< איוב 3 >

אחרי כן פתח איוב את פיהו ויקלל את יומו׃ 1
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
ויען איוב ויאמר׃ 2
Akasema,
יאבד יום אולד בו והלילה אמר הרה גבר׃ 3
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
היום ההוא יהי חשך אל ידרשהו אלוה ממעל ואל תופע עליו נהרה׃ 4
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
יגאלהו חשך וצלמות תשכן עליו עננה יבעתהו כמרירי יום׃ 5
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
הלילה ההוא יקחהו אפל אל יחד בימי שנה במספר ירחים אל יבא׃ 6
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
הנה הלילה ההוא יהי גלמוד אל תבא רננה בו׃ 7
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
יקבהו אררי יום העתידים ערר לויתן׃ 8
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
יחשכו כוכבי נשפו יקו לאור ואין ואל יראה בעפעפי שחר׃ 9
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
כי לא סגר דלתי בטני ויסתר עמל מעיני׃ 10
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
למה לא מרחם אמות מבטן יצאתי ואגוע׃ 11
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
מדוע קדמוני ברכים ומה שדים כי אינק׃ 12
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
כי עתה שכבתי ואשקוט ישנתי אז ינוח לי׃ 13
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
עם מלכים ויעצי ארץ הבנים חרבות למו׃ 14
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
או עם שרים זהב להם הממלאים בתיהם כסף׃ 15
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
או כנפל טמון לא אהיה כעללים לא ראו אור׃ 16
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
שם רשעים חדלו רגז ושם ינוחו יגיעי כח׃ 17
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
יחד אסירים שאננו לא שמעו קול נגש׃ 18
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
קטן וגדול שם הוא ועבד חפשי מאדניו׃ 19
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
למה יתן לעמל אור וחיים למרי נפש׃ 20
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
המחכים למות ואיננו ויחפרהו ממטמונים׃ 21
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
השמחים אלי גיל ישישו כי ימצאו קבר׃ 22
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
לגבר אשר דרכו נסתרה ויסך אלוה בעדו׃ 23
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
כי לפני לחמי אנחתי תבא ויתכו כמים שאגתי׃ 24
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
כי פחד פחדתי ויאתיני ואשר יגרתי יבא לי׃ 25
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
לא שלותי ולא שקטתי ולא נחתי ויבא רגז׃ 26
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”

< איוב 3 >