< איוב 3 >
אחרי כן פתח איוב את פיהו ויקלל את יומו׃ | 1 |
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
יאבד יום אולד בו והלילה אמר הרה גבר׃ | 3 |
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
היום ההוא יהי חשך אל ידרשהו אלוה ממעל ואל תופע עליו נהרה׃ | 4 |
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
יגאלהו חשך וצלמות תשכן עליו עננה יבעתהו כמרירי יום׃ | 5 |
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
הלילה ההוא יקחהו אפל אל יחד בימי שנה במספר ירחים אל יבא׃ | 6 |
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
הנה הלילה ההוא יהי גלמוד אל תבא רננה בו׃ | 7 |
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
יקבהו אררי יום העתידים ערר לויתן׃ | 8 |
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
יחשכו כוכבי נשפו יקו לאור ואין ואל יראה בעפעפי שחר׃ | 9 |
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
כי לא סגר דלתי בטני ויסתר עמל מעיני׃ | 10 |
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
למה לא מרחם אמות מבטן יצאתי ואגוע׃ | 11 |
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
מדוע קדמוני ברכים ומה שדים כי אינק׃ | 12 |
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
כי עתה שכבתי ואשקוט ישנתי אז ינוח לי׃ | 13 |
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
עם מלכים ויעצי ארץ הבנים חרבות למו׃ | 14 |
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
או עם שרים זהב להם הממלאים בתיהם כסף׃ | 15 |
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
או כנפל טמון לא אהיה כעללים לא ראו אור׃ | 16 |
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
שם רשעים חדלו רגז ושם ינוחו יגיעי כח׃ | 17 |
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
יחד אסירים שאננו לא שמעו קול נגש׃ | 18 |
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
קטן וגדול שם הוא ועבד חפשי מאדניו׃ | 19 |
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
למה יתן לעמל אור וחיים למרי נפש׃ | 20 |
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
המחכים למות ואיננו ויחפרהו ממטמונים׃ | 21 |
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
השמחים אלי גיל ישישו כי ימצאו קבר׃ | 22 |
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
לגבר אשר דרכו נסתרה ויסך אלוה בעדו׃ | 23 |
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
כי לפני לחמי אנחתי תבא ויתכו כמים שאגתי׃ | 24 |
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
כי פחד פחדתי ויאתיני ואשר יגרתי יבא לי׃ | 25 |
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
לא שלותי ולא שקטתי ולא נחתי ויבא רגז׃ | 26 |
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”