< איוב 3 >

אחרי כן פתח איוב את פיהו ויקלל את יומו׃ 1
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
ויען איוב ויאמר׃ 2
Kisha akasema:
יאבד יום אולד בו והלילה אמר הרה גבר׃ 3
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
היום ההוא יהי חשך אל ידרשהו אלוה ממעל ואל תופע עליו נהרה׃ 4
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
יגאלהו חשך וצלמות תשכן עליו עננה יבעתהו כמרירי יום׃ 5
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
הלילה ההוא יקחהו אפל אל יחד בימי שנה במספר ירחים אל יבא׃ 6
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
הנה הלילה ההוא יהי גלמוד אל תבא רננה בו׃ 7
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
יקבהו אררי יום העתידים ערר לויתן׃ 8
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
יחשכו כוכבי נשפו יקו לאור ואין ואל יראה בעפעפי שחר׃ 9
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
כי לא סגר דלתי בטני ויסתר עמל מעיני׃ 10
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
למה לא מרחם אמות מבטן יצאתי ואגוע׃ 11
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
מדוע קדמוני ברכים ומה שדים כי אינק׃ 12
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
כי עתה שכבתי ואשקוט ישנתי אז ינוח לי׃ 13
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
עם מלכים ויעצי ארץ הבנים חרבות למו׃ 14
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
או עם שרים זהב להם הממלאים בתיהם כסף׃ 15
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
או כנפל טמון לא אהיה כעללים לא ראו אור׃ 16
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
שם רשעים חדלו רגז ושם ינוחו יגיעי כח׃ 17
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
יחד אסירים שאננו לא שמעו קול נגש׃ 18
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
קטן וגדול שם הוא ועבד חפשי מאדניו׃ 19
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
למה יתן לעמל אור וחיים למרי נפש׃ 20
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
המחכים למות ואיננו ויחפרהו ממטמונים׃ 21
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
השמחים אלי גיל ישישו כי ימצאו קבר׃ 22
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
לגבר אשר דרכו נסתרה ויסך אלוה בעדו׃ 23
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
כי לפני לחמי אנחתי תבא ויתכו כמים שאגתי׃ 24
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
כי פחד פחדתי ויאתיני ואשר יגרתי יבא לי׃ 25
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
לא שלותי ולא שקטתי ולא נחתי ויבא רגז׃ 26
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< איוב 3 >