< איוב 3 >
אחרי כן פתח איוב את פיהו ויקלל את יומו׃ | 1 |
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
יאבד יום אולד בו והלילה אמר הרה גבר׃ | 3 |
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
היום ההוא יהי חשך אל ידרשהו אלוה ממעל ואל תופע עליו נהרה׃ | 4 |
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
יגאלהו חשך וצלמות תשכן עליו עננה יבעתהו כמרירי יום׃ | 5 |
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
הלילה ההוא יקחהו אפל אל יחד בימי שנה במספר ירחים אל יבא׃ | 6 |
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
הנה הלילה ההוא יהי גלמוד אל תבא רננה בו׃ | 7 |
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
יקבהו אררי יום העתידים ערר לויתן׃ | 8 |
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
יחשכו כוכבי נשפו יקו לאור ואין ואל יראה בעפעפי שחר׃ | 9 |
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
כי לא סגר דלתי בטני ויסתר עמל מעיני׃ | 10 |
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
למה לא מרחם אמות מבטן יצאתי ואגוע׃ | 11 |
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
מדוע קדמוני ברכים ומה שדים כי אינק׃ | 12 |
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
כי עתה שכבתי ואשקוט ישנתי אז ינוח לי׃ | 13 |
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
עם מלכים ויעצי ארץ הבנים חרבות למו׃ | 14 |
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
או עם שרים זהב להם הממלאים בתיהם כסף׃ | 15 |
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
או כנפל טמון לא אהיה כעללים לא ראו אור׃ | 16 |
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
שם רשעים חדלו רגז ושם ינוחו יגיעי כח׃ | 17 |
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
יחד אסירים שאננו לא שמעו קול נגש׃ | 18 |
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
קטן וגדול שם הוא ועבד חפשי מאדניו׃ | 19 |
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
למה יתן לעמל אור וחיים למרי נפש׃ | 20 |
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
המחכים למות ואיננו ויחפרהו ממטמונים׃ | 21 |
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
השמחים אלי גיל ישישו כי ימצאו קבר׃ | 22 |
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
לגבר אשר דרכו נסתרה ויסך אלוה בעדו׃ | 23 |
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
כי לפני לחמי אנחתי תבא ויתכו כמים שאגתי׃ | 24 |
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
כי פחד פחדתי ויאתיני ואשר יגרתי יבא לי׃ | 25 |
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
לא שלותי ולא שקטתי ולא נחתי ויבא רגז׃ | 26 |
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”