< איוב 28 >

כי יש לכסף מוצא ומקום לזהב יזקו׃ 1
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
ברזל מעפר יקח ואבן יצוק נחושה׃ 2
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
קץ שם לחשך ולכל תכלית הוא חוקר אבן אפל וצלמות׃ 3
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
פרץ נחל מעם גר הנשכחים מני רגל דלו מאנוש נעו׃ 4
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
ארץ ממנה יצא לחם ותחתיה נהפך כמו אש׃ 5
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
מקום ספיר אבניה ועפרת זהב לו׃ 6
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
נתיב לא ידעו עיט ולא שזפתו עין איה׃ 7
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
לא הדריכהו בני שחץ לא עדה עליו שחל׃ 8
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
בחלמיש שלח ידו הפך משרש הרים׃ 9
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
בצורות יארים בקע וכל יקר ראתה עינו׃ 10
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
מבכי נהרות חבש ותעלמה יצא אור׃ 11
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
והחכמה מאין תמצא ואי זה מקום בינה׃ 12
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
לא ידע אנוש ערכה ולא תמצא בארץ החיים׃ 13
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
תהום אמר לא בי היא וים אמר אין עמדי׃ 14
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
לא יתן סגור תחתיה ולא ישקל כסף מחירה׃ 15
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
לא תסלה בכתם אופיר בשהם יקר וספיר׃ 16
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
לא יערכנה זהב וזכוכית ותמורתה כלי פז׃ 17
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
ראמות וגביש לא יזכר ומשך חכמה מפנינים׃ 18
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
לא יערכנה פטדת כוש בכתם טהור לא תסלה׃ 19
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
והחכמה מאין תבוא ואי זה מקום בינה׃ 20
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
ונעלמה מעיני כל חי ומעוף השמים נסתרה׃ 21
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
אבדון ומות אמרו באזנינו שמענו שמעה׃ 22
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
אלהים הבין דרכה והוא ידע את מקומה׃ 23
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
כי הוא לקצות הארץ יביט תחת כל השמים יראה׃ 24
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
לעשות לרוח משקל ומים תכן במדה׃ 25
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
בעשתו למטר חק ודרך לחזיז קלות׃ 26
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
אז ראה ויספרה הכינה וגם חקרה׃ 27
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
ויאמר לאדם הן יראת אדני היא חכמה וסור מרע בינה׃ 28
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”

< איוב 28 >