< איוב 28 >
כי יש לכסף מוצא ומקום לזהב יזקו׃ | 1 |
Hakika kuna machimbo ya fedha, wanaposafisha dhahabu.
ברזל מעפר יקח ואבן יצוק נחושה׃ | 2 |
Chuma uchimbwa; shaba uyeyushwa kutoka katika jiwe.
קץ שם לחשך ולכל תכלית הוא חוקר אבן אפל וצלמות׃ | 3 |
Mtu anaondoa giza na kutafuta, katika mpaka wa mbali, mawe hayaonekani na giza totoro.
פרץ נחל מעם גר הנשכחים מני רגל דלו מאנוש נעו׃ | 4 |
Huchimba shimo mbali na makazi ya watu, mahali pasipopitwa na mtu. Huning'inia mbali na watu; uharakisha kwenda na kurudi.
ארץ ממנה יצא לחם ותחתיה נהפך כמו אש׃ | 5 |
Kwa nchi, kizalishwapo chakula, inapinduliwa kama kwa moto.
מקום ספיר אבניה ועפרת זהב לו׃ | 6 |
Mawe yake yana johari, na vumbi lake lina dhahabu.
נתיב לא ידעו עיט ולא שזפתו עין איה׃ | 7 |
Hata ndege mwindaji hapajui, wala jicho la kipanga halijapaona.
לא הדריכהו בני שחץ לא עדה עליו שחל׃ | 8 |
Ndege mwenye majivuna hajawai kuiona njia hiyo, wala simba mkali kupita pale.
בחלמיש שלח ידו הפך משרש הרים׃ | 9 |
Mtu huchimba mwamba mgumu; hupindua milima katika vyanzo vyake.
בצורות יארים בקע וכל יקר ראתה עינו׃ | 10 |
Huweka njia katika miamba; macho yake pale kila kilicho cha thamani.
מבכי נהרות חבש ותעלמה יצא אור׃ | 11 |
Hufunga vyanzo hata wasiondoke; kilichofichika pale hukifunua.
והחכמה מאין תמצא ואי זה מקום בינה׃ | 12 |
Hekima itakuwa wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
לא ידע אנוש ערכה ולא תמצא בארץ החיים׃ | 13 |
Mtu hafahamu thamani yake; wala haipatikani katika nchi ya walio hai.
תהום אמר לא בי היא וים אמר אין עמדי׃ | 14 |
Vilindi vya maji chini ya nchi husema, 'Haiko kwangu'; bahari husema, 'Haipo pamoja nami.'
לא יתן סגור תחתיה ולא ישקל כסף מחירה׃ | 15 |
Hainunuliwi kwa dhahabu; wala hailinganishwi na fedha.
לא תסלה בכתם אופיר בשהם יקר וספיר׃ | 16 |
Haiwezi kuthamanishwa na dhahabu ya Ofiri, kwa jiwe jeusi la thamani au johari.
לא יערכנה זהב וזכוכית ותמורתה כלי פז׃ | 17 |
Dhahabu na fuwele hailingani nayo kwa thamani; wala haiwezi kubadilishwa kwa vito vya dhahabu safi.
ראמות וגביש לא יזכר ומשך חכמה מפנינים׃ | 18 |
Hailinganishwi na marijani wala yaspi; hakika, thamani ya hekima inapita madini ya rubi.
לא יערכנה פטדת כוש בכתם טהור לא תסלה׃ | 19 |
Topazi ya Ethiopia hailinganishwi nayo; wala kuthamanishwa kwa dhahabu safi.
והחכמה מאין תבוא ואי זה מקום בינה׃ | 20 |
Je hekima inatoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?
ונעלמה מעיני כל חי ומעוף השמים נסתרה׃ | 21 |
Hekima imejificha mbali na macho ya viumbe wote na ndege wa angani.
אבדון ומות אמרו באזנינו שמענו שמעה׃ | 22 |
Mauti na uharibifu husema, 'Tumesikia tu tetesi kwa masikio yetu.'
אלהים הבין דרכה והוא ידע את מקומה׃ | 23 |
Mungu hufahamu njia ya kuipata; anapafahamu ilipo.
כי הוא לקצות הארץ יביט תחת כל השמים יראה׃ | 24 |
Kwani uona miisho yote ya dunia na huona chini ya mbingu zote.
לעשות לרוח משקל ומים תכן במדה׃ | 25 |
Hapo kale, alifanya nguvu za upepo na kuyagawanya maji kwa kipimo.
בעשתו למטר חק ודרך לחזיז קלות׃ | 26 |
Aliiwekea mvua tamko na njia ya radi na munguromo.
אז ראה ויספרה הכינה וגם חקרה׃ | 27 |
Kisha akaiona hekima na kuitangaza; aliianzisha, bila shaka, na kuipima.
ויאמר לאדם הן יראת אדני היא חכמה וסור מרע בינה׃ | 28 |
Aliwambia watu, 'Tazameni, kumcha Bwana - ni hekima; kuacha uovu ni ufahamu.”