< איוב 27 >

ויסף איוב שאת משלו ויאמר׃ 1
Ayubu akaendelea kuoengea na kusema,
חי אל הסיר משפטי ושדי המר נפשי׃ 2
“Kama aishivyo Mungu, ameniondolea haki yangu, Mwenyezi, aliyeyafanya machungu maisha yangu,
כי כל עוד נשמתי בי ורוח אלוה באפי׃ 3
kadili uhai ungalimo ndani yangu uzima wa Mungu upo puani mwangu.
אם תדברנה שפתי עולה ולשוני אם יהגה רמיה׃ 4
Hakika midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu kunena uongo.
חלילה לי אם אצדיק אתכם עד אגוע לא אסיר תמתי ממני׃ 5
Sitakiri kwamba mko sahihi; hata nifapo sitakana uadilifu wangu.
בצדקתי החזקתי ולא ארפה לא יחרף לבבי מימי׃ 6
Naishikilia haki yangu na sitaiacha; nafsi yangu haitanisuta kadili ninavyoishi.
יהי כרשע איבי ומתקוממי כעול׃ 7
Adui yangu na awe kama mwovu; anayeinuka kunyume changu na awe kama asiye haki.
כי מה תקות חנף כי יבצע כי ישל אלוה נפשו׃ 8
Kwani tumaini la mwovu ni nini Mungu anapomwondoa, Mungu anapochukua uhai wake?
הצעקתו ישמע אל כי תבוא עליו צרה׃ 9
Je Mungu atasikiliza kilio chake tabu zinapompat?
אם על שדי יתענג יקרא אלוה בכל עת׃ 10
Je atajifurahisha katika Mwenyezi na kumwita Mungu nyakati zote
אורה אתכם ביד אל אשר עם שדי לא אכחד׃ 11
Nitawafundisha kuhusu uwezo wa Mungu; sitabatilisha mawazo ya Mwenyezi.
הן אתם כלכם חזיתם ולמה זה הבל תהבלו׃ 12
Tazama, ninyi nyote mmeona; kwa nini basi mmeongea yasiyo na maana.
זה חלק אדם רשע עם אל ונחלת עריצים משדי יקחו׃ 13
Hii ndiyo hatima ya waovu mbele za Mungu, urithi wa mtesaji aupokeao kutoka kwa Mwenyezi.
אם ירבו בניו למו חרב וצאצאיו לא ישבעו לחם׃ 14
Ikiwa watoto wake wataongezeka, ni kwa upanga; uzao wake utakuwa na njaa.
שרידו במות יקברו ואלמנתיו לא תבכינה׃ 15
Wanaomsalia watauawa kwa tauni, na wajane wao hawatawaombolezea.
אם יצבר כעפר כסף וכחמר יכין מלבוש׃ 16
Japokuwa waovu hurundika mali kama mavumbi,
יכין וצדיק ילבש וכסף נקי יחלק׃ 17
na kukusanya mavazi kama udongo, atakusanya mavazi, lakini mwenye haki atavaa, na wasio na hatia watagawana mali.
בנה כעש ביתו וכסכה עשה נצר׃ 18
Hujenga nyumba yake kama buibui, kama kibanda cha muda afanyacho mlinzi.
עשיר ישכב ולא יאסף עיניו פקח ואיננו׃ 19
Hulala kitandani akiwa tajiri, lakini hataendelea hivyo; na afumbuapo macho, hana kitu.
תשיגהו כמים בלהות לילה גנבתו סופה׃ 20
Vitisho humpata kama maji, dhoruba humwondoa usiku.
ישאהו קדים וילך וישערהו ממקמו׃ 21
Upepo wa mashariki umwondoa, naye huondoka; humwondoa mahali pake.
וישלך עליו ולא יחמל מידו ברוח יברח׃ 22
Humpiga bila kukoma; hujaribu kumnasua katika uwezo wake.
ישפק עלימו כפימו וישרק עליו ממקמו׃ 23
Unampigia makofi kwa kejeli; humwondoa mahali pake.

< איוב 27 >