< איוב 27 >
ויסף איוב שאת משלו ויאמר׃ | 1 |
Ayubu akaendelea kuoengea na kusema,
חי אל הסיר משפטי ושדי המר נפשי׃ | 2 |
“Kama aishivyo Mungu, ameniondolea haki yangu, Mwenyezi, aliyeyafanya machungu maisha yangu,
כי כל עוד נשמתי בי ורוח אלוה באפי׃ | 3 |
kadili uhai ungalimo ndani yangu uzima wa Mungu upo puani mwangu.
אם תדברנה שפתי עולה ולשוני אם יהגה רמיה׃ | 4 |
Hakika midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu kunena uongo.
חלילה לי אם אצדיק אתכם עד אגוע לא אסיר תמתי ממני׃ | 5 |
Sitakiri kwamba mko sahihi; hata nifapo sitakana uadilifu wangu.
בצדקתי החזקתי ולא ארפה לא יחרף לבבי מימי׃ | 6 |
Naishikilia haki yangu na sitaiacha; nafsi yangu haitanisuta kadili ninavyoishi.
יהי כרשע איבי ומתקוממי כעול׃ | 7 |
Adui yangu na awe kama mwovu; anayeinuka kunyume changu na awe kama asiye haki.
כי מה תקות חנף כי יבצע כי ישל אלוה נפשו׃ | 8 |
Kwani tumaini la mwovu ni nini Mungu anapomwondoa, Mungu anapochukua uhai wake?
הצעקתו ישמע אל כי תבוא עליו צרה׃ | 9 |
Je Mungu atasikiliza kilio chake tabu zinapompat?
אם על שדי יתענג יקרא אלוה בכל עת׃ | 10 |
Je atajifurahisha katika Mwenyezi na kumwita Mungu nyakati zote
אורה אתכם ביד אל אשר עם שדי לא אכחד׃ | 11 |
Nitawafundisha kuhusu uwezo wa Mungu; sitabatilisha mawazo ya Mwenyezi.
הן אתם כלכם חזיתם ולמה זה הבל תהבלו׃ | 12 |
Tazama, ninyi nyote mmeona; kwa nini basi mmeongea yasiyo na maana.
זה חלק אדם רשע עם אל ונחלת עריצים משדי יקחו׃ | 13 |
Hii ndiyo hatima ya waovu mbele za Mungu, urithi wa mtesaji aupokeao kutoka kwa Mwenyezi.
אם ירבו בניו למו חרב וצאצאיו לא ישבעו לחם׃ | 14 |
Ikiwa watoto wake wataongezeka, ni kwa upanga; uzao wake utakuwa na njaa.
שרידו במות יקברו ואלמנתיו לא תבכינה׃ | 15 |
Wanaomsalia watauawa kwa tauni, na wajane wao hawatawaombolezea.
אם יצבר כעפר כסף וכחמר יכין מלבוש׃ | 16 |
Japokuwa waovu hurundika mali kama mavumbi,
יכין וצדיק ילבש וכסף נקי יחלק׃ | 17 |
na kukusanya mavazi kama udongo, atakusanya mavazi, lakini mwenye haki atavaa, na wasio na hatia watagawana mali.
בנה כעש ביתו וכסכה עשה נצר׃ | 18 |
Hujenga nyumba yake kama buibui, kama kibanda cha muda afanyacho mlinzi.
עשיר ישכב ולא יאסף עיניו פקח ואיננו׃ | 19 |
Hulala kitandani akiwa tajiri, lakini hataendelea hivyo; na afumbuapo macho, hana kitu.
תשיגהו כמים בלהות לילה גנבתו סופה׃ | 20 |
Vitisho humpata kama maji, dhoruba humwondoa usiku.
ישאהו קדים וילך וישערהו ממקמו׃ | 21 |
Upepo wa mashariki umwondoa, naye huondoka; humwondoa mahali pake.
וישלך עליו ולא יחמל מידו ברוח יברח׃ | 22 |
Humpiga bila kukoma; hujaribu kumnasua katika uwezo wake.
ישפק עלימו כפימו וישרק עליו ממקמו׃ | 23 |
Unampigia makofi kwa kejeli; humwondoa mahali pake.