< איוב 27 >

ויסף איוב שאת משלו ויאמר׃ 1
Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
חי אל הסיר משפטי ושדי המר נפשי׃ 2
“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu, Mwenyezi ambaye amenifanya nionje uchungu wa nafsi,
כי כל עוד נשמתי בי ורוח אלוה באפי׃ 3
kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
אם תדברנה שפתי עולה ולשוני אם יהגה רמיה׃ 4
midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
חלילה לי אם אצדיק אתכם עד אגוע לא אסיר תמתי ממני׃ 5
Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
בצדקתי החזקתי ולא ארפה לא יחרף לבבי מימי׃ 6
Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
יהי כרשע איבי ומתקוממי כעול׃ 7
“Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
כי מה תקות חנף כי יבצע כי ישל אלוה נפשו׃ 8
Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
הצעקתו ישמע אל כי תבוא עליו צרה׃ 9
Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
אם על שדי יתענג יקרא אלוה בכל עת׃ 10
Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
אורה אתכם ביד אל אשר עם שדי לא אכחד׃ 11
“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
הן אתם כלכם חזיתם ולמה זה הבל תהבלו׃ 12
Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
זה חלק אדם רשע עם אל ונחלת עריצים משדי יקחו׃ 13
“Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu, urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi:
אם ירבו בניו למו חרב וצאצאיו לא ישבעו לחם׃ 14
Hata kama watoto wake watakuwa wengi kiasi gani, fungu lao ni kuuawa kwa upanga; wazao wake hawatakuwa kamwe na chakula cha kuwatosha.
שרידו במות יקברו ואלמנתיו לא תבכינה׃ 15
Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao, nao wajane wao hawatawaombolezea.
אם יצבר כעפר כסף וכחמר יכין מלבוש׃ 16
Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi, na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi,
יכין וצדיק ילבש וכסף נקי יחלק׃ 17
yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa, naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake.
בנה כעש ביתו וכסכה עשה נצר׃ 18
Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui, kama kibanda alichotengeneza mlinzi.
עשיר ישכב ולא יאסף עיניו פקח ואיננו׃ 19
Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; afunguapo macho yake, yote yametoweka.
תשיגהו כמים בלהות לילה גנבתו סופה׃ 20
Vitisho humjia kama mafuriko; dhoruba humkumba ghafula usiku.
ישאהו קדים וילך וישערהו ממקמו׃ 21
Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; humzoa kutoka mahali pake.
וישלך עליו ולא יחמל מידו ברוח יברח׃ 22
Humvurumisha bila huruma, huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.
ישפק עלימו כפימו וישרק עליו ממקמו׃ 23
Upepo humpigia makofi kwa dharau, na kumfukuza atoke mahali pake.

< איוב 27 >