< איוב 27 >
ויסף איוב שאת משלו ויאמר׃ | 1 |
Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
חי אל הסיר משפטי ושדי המר נפשי׃ | 2 |
“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu, Mwenyezi ambaye amenifanya nionje uchungu wa nafsi,
כי כל עוד נשמתי בי ורוח אלוה באפי׃ | 3 |
kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
אם תדברנה שפתי עולה ולשוני אם יהגה רמיה׃ | 4 |
midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
חלילה לי אם אצדיק אתכם עד אגוע לא אסיר תמתי ממני׃ | 5 |
Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
בצדקתי החזקתי ולא ארפה לא יחרף לבבי מימי׃ | 6 |
Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
יהי כרשע איבי ומתקוממי כעול׃ | 7 |
“Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
כי מה תקות חנף כי יבצע כי ישל אלוה נפשו׃ | 8 |
Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
הצעקתו ישמע אל כי תבוא עליו צרה׃ | 9 |
Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
אם על שדי יתענג יקרא אלוה בכל עת׃ | 10 |
Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
אורה אתכם ביד אל אשר עם שדי לא אכחד׃ | 11 |
“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
הן אתם כלכם חזיתם ולמה זה הבל תהבלו׃ | 12 |
Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
זה חלק אדם רשע עם אל ונחלת עריצים משדי יקחו׃ | 13 |
“Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu, urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi:
אם ירבו בניו למו חרב וצאצאיו לא ישבעו לחם׃ | 14 |
Hata kama watoto wake watakuwa wengi kiasi gani, fungu lao ni kuuawa kwa upanga; wazao wake hawatakuwa kamwe na chakula cha kuwatosha.
שרידו במות יקברו ואלמנתיו לא תבכינה׃ | 15 |
Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao, nao wajane wao hawatawaombolezea.
אם יצבר כעפר כסף וכחמר יכין מלבוש׃ | 16 |
Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi, na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi,
יכין וצדיק ילבש וכסף נקי יחלק׃ | 17 |
yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa, naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake.
בנה כעש ביתו וכסכה עשה נצר׃ | 18 |
Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui, kama kibanda alichotengeneza mlinzi.
עשיר ישכב ולא יאסף עיניו פקח ואיננו׃ | 19 |
Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; afunguapo macho yake, yote yametoweka.
תשיגהו כמים בלהות לילה גנבתו סופה׃ | 20 |
Vitisho humjia kama mafuriko; dhoruba humkumba ghafula usiku.
ישאהו קדים וילך וישערהו ממקמו׃ | 21 |
Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; humzoa kutoka mahali pake.
וישלך עליו ולא יחמל מידו ברוח יברח׃ | 22 |
Humvurumisha bila huruma, huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.
ישפק עלימו כפימו וישרק עליו ממקמו׃ | 23 |
Upepo humpigia makofi kwa dharau, na kumfukuza atoke mahali pake.