< איוב 23 >
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
גם היום מרי שחי ידי כבדה על אנחתי׃ | 2 |
“Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
מי יתן ידעתי ואמצאהו אבוא עד תכונתו׃ | 3 |
Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
אערכה לפניו משפט ופי אמלא תוכחות׃ | 4 |
Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
אדעה מלים יענני ואבינה מה יאמר לי׃ | 5 |
Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
הברב כח יריב עמדי לא אך הוא ישם בי׃ | 6 |
Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
שם ישר נוכח עמו ואפלטה לנצח משפטי׃ | 7 |
Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
הן קדם אהלך ואיננו ואחור ולא אבין לו׃ | 8 |
Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
שמאול בעשתו ולא אחז יעטף ימין ולא אראה׃ | 9 |
Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
כי ידע דרך עמדי בחנני כזהב אצא׃ | 10 |
Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
באשרו אחזה רגלי דרכו שמרתי ולא אט׃ | 11 |
Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
מצות שפתיו ולא אמיש מחקי צפנתי אמרי פיו׃ | 12 |
Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
והוא באחד ומי ישיבנו ונפשו אותה ויעש׃ | 13 |
Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
כי ישלים חקי וכהנה רבות עמו׃ | 14 |
Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
על כן מפניו אבהל אתבונן ואפחד ממנו׃ | 15 |
Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
ואל הרך לבי ושדי הבהילני׃ | 16 |
Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
כי לא נצמתי מפני חשך ומפני כסה אפל׃ | 17 |
Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.