< איוב 21 >
שמעו שמוע מלתי ותהי זאת תנחומתיכם׃ | 2 |
“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini; hii na iwe faraja mnayonipa mimi.
שאוני ואנכי אדבר ואחר דברי תלעיג׃ | 3 |
Nivumilieni ninapozungumza, nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.
האנכי לאדם שיחי ואם מדוע לא תקצר רוחי׃ | 4 |
“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu? Kwa nini nisikose subira?
פנו אלי והשמו ושימו יד על פה׃ | 5 |
Niangalieni mkastaajabu; mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.
ואם זכרתי ונבהלתי ואחז בשרי פלצות׃ | 6 |
Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa, nao mwili wangu unatetemeka.
מדוע רשעים יחיו עתקו גם גברו חיל׃ | 7 |
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?
זרעם נכון לפניהם עמם וצאצאיהם לעיניהם׃ | 8 |
Huwaona watoto wao wakithibitika wakiwa wamewazunguka, wazao wao mbele za macho yao.
בתיהם שלום מפחד ולא שבט אלוה עליהם׃ | 9 |
Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; fimbo ya Mungu haiko juu yao.
שורו עבר ולא יגעל תפלט פרתו ולא תשכל׃ | 10 |
Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.
ישלחו כצאן עויליהם וילדיהם ירקדון׃ | 11 |
Huwatoa watoto wao nje kama kundi; wadogo wao huchezacheza.
ישאו כתף וכנור וישמחו לקול עוגב׃ | 12 |
Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, nao huifurahia sauti ya filimbi.
יבלו בטוב ימיהם וברגע שאול יחתו׃ (Sheol ) | 13 |
Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani. (Sheol )
ויאמרו לאל סור ממנו ודעת דרכיך לא חפצנו׃ | 14 |
Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’ Hatuna haja ya kufahamu njia zako.
מה שדי כי נעבדנו ומה נועיל כי נפגע בו׃ | 15 |
Mwenyezi ni nani hata tumtumikie? Tutapata faida gani kumwomba?
הן לא בידם טובם עצת רשעים רחקה מני׃ | 16 |
Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe, hivyo najitenga mbali na shauri la waovu.
כמה נר רשעים ידעך ויבא עלימו אידם חבלים יחלק באפו׃ | 17 |
“Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa? Ni mara ngapi maafa huwajia, yale yawapatayo ambayo Mungu huwapangia katika hasira yake?
יהיו כתבן לפני רוח וכמץ גנבתו סופה׃ | 18 |
Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo, kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?
אלוה יצפן לבניו אונו ישלם אליו וידע׃ | 19 |
Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu kwa ajili ya wanawe.’ Mungu na amlipe mtu mwenyewe, ili apate kulijua!
יראו עינו כידו ומחמת שדי ישתה׃ | 20 |
Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake; yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi.
כי מה חפצו בביתו אחריו ומספר חדשיו חצצו׃ | 21 |
Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma, miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho?
הלאל ילמד דעת והוא רמים ישפוט׃ | 22 |
“Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa, iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote?
זה ימות בעצם תמו כלו שלאנן ושליו׃ | 23 |
Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili, akiwa salama na mwenye raha kamili,
עטיניו מלאו חלב ומח עצמותיו ישקה׃ | 24 |
mwili wake ukiwa umenawiri, nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.
וזה ימות בנפש מרה ולא אכל בטובה׃ | 25 |
Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi, akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.
יחד על עפר ישכבו ורמה תכסה עליהם׃ | 26 |
Hao wote hulala mavumbini, nao mabuu huwafunika wote.
הן ידעתי מחשבותיכם ומזמות עלי תחמסו׃ | 27 |
“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri, mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.
כי תאמרו איה בית נדיב ואיה אהל משכנות רשעים׃ | 28 |
Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu, mahema ambayo watu waovu walikaa?’
הלא שאלתם עוברי דרך ואתתם לא תנכרו׃ | 29 |
Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri? Je, hamkutafakari taarifa zao:
כי ליום איד יחשך רע ליום עברות יובלו׃ | 30 |
kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa, kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?
מי יגיד על פניו דרכו והוא עשה מי ישלם לו׃ | 31 |
Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake? Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?
והוא לקברות יובל ועל גדיש ישקוד׃ | 32 |
Hupelekwa kaburini, nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.
מתקו לו רגבי נחל ואחריו כל אדם ימשוך ולפניו אין מספר׃ | 33 |
Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake; watu wote watamfuata, nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.
ואיך תנחמוני הבל ותשובתיכם נשאר מעל׃ | 34 |
“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu? Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”