< איוב 18 >
Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema, “
עד אנה תשימון קנצי למלין תבינו ואחר נדבר׃ | 2 |
Je, lini utaacha kusema kwako? Fikiri, na baadaye tutazungumza.
מדוע נחשבנו כבהמה נטמינו בעיניכם׃ | 3 |
Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama mwitu; kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?
טרף נפשו באפו הלמענך תעזב ארץ ויעתק צור ממקמו׃ | 4 |
Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako, nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?
גם אור רשעים ידעך ולא יגה שביב אשו׃ | 5 |
Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.
אור חשך באהלו ונרו עליו ידעך׃ | 6 |
Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa nje.
יצרו צעדי אונו ותשליכהו עצתו׃ | 7 |
Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi; mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.
כי שלח ברשת ברגליו ועל שבכה יתהלך׃ | 8 |
Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.
יאחז בעקב פח יחזק עליו צמים׃ | 9 |
Tanzi litamchukua yeye kwa kisigino; mtego utabaki kushikilia juu yake.
טמון בארץ חבלו ומלכדתו עלי נתיב׃ | 10 |
Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi; na mtego kwa ajili yake katika njia.
סביב בעתהו בלהות והפיצהו לרגליו׃ | 11 |
Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote; wao watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.
יהי רעב אנו ואיד נכון לצלעו׃ | 12 |
Utajiri wake utageuka kuwa njaa, na majanga yatakuwa tayari upande wake.
יאכל בדי עורו יאכל בדיו בכור מות׃ | 13 |
Sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa; Hakika, mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.
ינתק מאהלו מבטחו ותצעדהו למלך בלהות׃ | 14 |
Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake na hakuweza kutembea kwenda kwa mfalme mwenye utisho.
תשכון באהלו מבלי לו יזרה על נוהו גפרית׃ | 15 |
Watu ambao siyo wa kwake wataishi kwenye hema yake baada ya kuona ule moto mesambaa ndani ya nyumba yake yeye.
מתחת שרשיו יבשו וממעל ימל קצירו׃ | 16 |
Mizizi yake itanyauka chini yake; juu tawi lake yeye litakatwa.
זכרו אבד מני ארץ ולא שם לו על פני חוץ׃ | 17 |
Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.
יהדפהו מאור אל חשך ומתבל ינדהו׃ | 18 |
Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.
לא נין לו ולא נכד בעמו ואין שריד במגוריו׃ | 19 |
Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.
על יומו נשמו אחרנים וקדמנים אחזו שער׃ | 20 |
Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.
אך אלה משכנות עול וזה מקום לא ידע אל׃ | 21 |
Hakika hizo ni nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu.”