< איוב 13 >

הן כל ראתה עיני שמעה אזני ותבן לה׃ 1
Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
כדעתכם ידעתי גם אני לא נפל אנכי מכם׃ 2
Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
אולם אני אל שדי אדבר והוכח אל אל אחפץ׃ 3
Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
ואולם אתם טפלי שקר רפאי אלל כלכם׃ 4
Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
מי יתן החרש תחרישון ותהי לכם לחכמה׃ 5
Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
שמעו נא תוכחתי ורבות שפתי הקשיבו׃ 6
Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
הלאל תדברו עולה ולו תדברו רמיה׃ 7
Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
הפניו תשאון אם לאל תריבון׃ 8
Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
הטוב כי יחקר אתכם אם כהתל באנוש תהתלו בו׃ 9
Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
הוכח יוכיח אתכם אם בסתר פנים תשאון׃ 10
Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
הלא שאתו תבעת אתכם ופחדו יפל עליכם׃ 11
Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
זכרניכם משלי אפר לגבי חמר גביכם׃ 12
Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
החרישו ממני ואדברה אני ויעבר עלי מה׃ 13
Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
על מה אשא בשרי בשני ונפשי אשים בכפי׃ 14
Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
הן יקטלני לא איחל אך דרכי אל פניו אוכיח׃ 15
Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
גם הוא לי לישועה כי לא לפניו חנף יבוא׃ 16
Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
שמעו שמוע מלתי ואחותי באזניכם׃ 17
Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
הנה נא ערכתי משפט ידעתי כי אני אצדק׃ 18
Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
מי הוא יריב עמדי כי עתה אחריש ואגוע׃ 19
Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
אך שתים אל תעש עמדי אז מפניך לא אסתר׃ 20
Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
כפך מעלי הרחק ואמתך אל תבעתני׃ 21
Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
וקרא ואנכי אענה או אדבר והשיבני׃ 22
Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
כמה לי עונות וחטאות פשעי וחטאתי הדיעני׃ 23
Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
למה פניך תסתיר ותחשבני לאויב לך׃ 24
Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
העלה נדף תערוץ ואת קש יבש תרדף׃ 25
Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
כי תכתב עלי מררות ותורישני עונות נעורי׃ 26
Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
ותשם בסד רגלי ותשמור כל ארחותי על שרשי רגלי תתחקה׃ 27
Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
והוא כרקב יבלה כבגד אכלו עש׃ 28
japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.

< איוב 13 >