< איוב 12 >
אמנם כי אתם עם ועמכם תמות חכמה׃ | 2 |
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
גם לי לבב כמוכם לא נפל אנכי מכם ואת מי אין כמו אלה׃ | 3 |
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
שחק לרעהו אהיה קרא לאלוה ויענהו שחוק צדיק תמים׃ | 4 |
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
לפיד בוז לעשתות שאנן נכון למועדי רגל׃ | 5 |
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
ישליו אהלים לשדדים ובטחות למרגיזי אל לאשר הביא אלוה בידו׃ | 6 |
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
ואולם שאל נא בהמות ותרך ועוף השמים ויגד לך׃ | 7 |
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
או שיח לארץ ותרך ויספרו לך דגי הים׃ | 8 |
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
מי לא ידע בכל אלה כי יד יהוה עשתה זאת׃ | 9 |
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
אשר בידו נפש כל חי ורוח כל בשר איש׃ | 10 |
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
הלא אזן מלין תבחן וחך אכל יטעם לו׃ | 11 |
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
בישישים חכמה וארך ימים תבונה׃ | 12 |
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
עמו חכמה וגבורה לו עצה ותבונה׃ | 13 |
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
הן יהרוס ולא יבנה יסגר על איש ולא יפתח׃ | 14 |
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
הן יעצר במים ויבשו וישלחם ויהפכו ארץ׃ | 15 |
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
עמו עז ותושיה לו שגג ומשגה׃ | 16 |
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
מוליך יועצים שולל ושפטים יהולל׃ | 17 |
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
מוסר מלכים פתח ויאסר אזור במתניהם׃ | 18 |
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
מוליך כהנים שולל ואתנים יסלף׃ | 19 |
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
מסיר שפה לנאמנים וטעם זקנים יקח׃ | 20 |
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
שופך בוז על נדיבים ומזיח אפיקים רפה׃ | 21 |
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
מגלה עמקות מני חשך ויצא לאור צלמות׃ | 22 |
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
משגיא לגוים ויאבדם שטח לגוים וינחם׃ | 23 |
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
מסיר לב ראשי עם הארץ ויתעם בתהו לא דרך׃ | 24 |
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
ימששו חשך ולא אור ויתעם כשכור׃ | 25 |
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.