< שמות 25 >

וידבר יהוה אל משה לאמר׃ 1
Bwana akamwambia Mose,
דבר אל בני ישראל ויקחו לי תרומה מאת כל איש אשר ידבנו לבו תקחו את תרומתי׃ 2
“Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
וזאת התרומה אשר תקחו מאתם זהב וכסף ונחשת׃ 3
Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
ותכלת וארגמן ותולעת שני ושש ועזים׃ 4
nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
וערת אילם מאדמים וערת תחשים ועצי שטים׃ 5
ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
שמן למאר בשמים לשמן המשחה ולקטרת הסמים׃ 6
mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
אבני שהם ואבני מלאים לאפד ולחשן׃ 7
na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
ועשו לי מקדש ושכנתי בתוכם׃ 8
“Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
ככל אשר אני מראה אותך את תבנית המשכן ואת תבנית כל כליו וכן תעשו׃ 9
Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
ועשו ארון עצי שטים אמתים וחצי ארכו ואמה וחצי רחבו ואמה וחצי קמתו׃ 10
“Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
וצפית אתו זהב טהור מבית ומחוץ תצפנו ועשית עליו זר זהב סביב׃ 11
Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
ויצקת לו ארבע טבעת זהב ונתתה על ארבע פעמתיו ושתי טבעת על צלעו האחת ושתי טבעת על צלעו השנית׃ 12
Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
ועשית בדי עצי שטים וצפית אתם זהב׃ 13
Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
והבאת את הבדים בטבעת על צלעת הארן לשאת את הארן בהם׃ 14
Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
בטבעת הארן יהיו הבדים לא יסרו ממנו׃ 15
Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
ונתת אל הארן את העדת אשר אתן אליך׃ 16
Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
ועשית כפרת זהב טהור אמתים וחצי ארכה ואמה וחצי רחבה׃ 17
“Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
ועשית שנים כרבים זהב מקשה תעשה אתם משני קצות הכפרת׃ 18
Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
ועשה כרוב אחד מקצה מזה וכרוב אחד מקצה מזה מן הכפרת תעשו את הכרבים על שני קצותיו׃ 19
Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
והיו הכרבים פרשי כנפים למעלה סככים בכנפיהם על הכפרת ופניהם איש אל אחיו אל הכפרת יהיו פני הכרבים׃ 20
Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
ונתת את הכפרת על הארן מלמעלה ואל הארן תתן את העדת אשר אתן אליך׃ 21
Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
ונועדתי לך שם ודברתי אתך מעל הכפרת מבין שני הכרבים אשר על ארן העדת את כל אשר אצוה אותך אל בני ישראל׃ 22
Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
ועשית שלחן עצי שטים אמתים ארכו ואמה רחבו ואמה וחצי קמתו׃ 23
“Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
וצפית אתו זהב טהור ועשית לו זר זהב סביב׃ 24
Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
ועשית לו מסגרת טפח סביב ועשית זר זהב למסגרתו סביב׃ 25
Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
ועשית לו ארבע טבעת זהב ונתת את הטבעת על ארבע הפאת אשר לארבע רגליו׃ 26
Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
לעמת המסגרת תהיין הטבעת לבתים לבדים לשאת את השלחן׃ 27
Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
ועשית את הבדים עצי שטים וצפית אתם זהב ונשא בם את השלחן׃ 28
Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
ועשית קערתיו וכפתיו וקשותיו ומנקיתיו אשר יסך בהן זהב טהור תעשה אתם׃ 29
Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
ונתת על השלחן לחם פנים לפני תמיד׃ 30
Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
ועשית מנרת זהב טהור מקשה תעשה המנורה ירכה וקנה גביעיה כפתריה ופרחיה ממנה יהיו׃ 31
“Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
וששה קנים יצאים מצדיה שלשה קני מנרה מצדה האחד ושלשה קני מנרה מצדה השני׃ 32
Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
שלשה גבעים משקדים בקנה האחד כפתר ופרח ושלשה גבעים משקדים בקנה האחד כפתר ופרח כן לששת הקנים היצאים מן המנרה׃ 33
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
ובמנרה ארבעה גבעים משקדים כפתריה ופרחיה׃ 34
Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
וכפתר תחת שני הקנים ממנה וכפתר תחת שני הקנים ממנה וכפתר תחת שני הקנים ממנה לששת הקנים היצאים מן המנרה׃ 35
Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
כפתריהם וקנתם ממנה יהיו כלה מקשה אחת זהב טהור׃ 36
Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
ועשית את נרתיה שבעה והעלה את נרתיה והאיר על עבר פניה׃ 37
“Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
ומלקחיה ומחתתיה זהב טהור׃ 38
Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
ככר זהב טהור יעשה אתה את כל הכלים האלה׃ 39
Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
וראה ועשה בתבניתם אשר אתה מראה בהר׃ 40
Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

< שמות 25 >