< אֶל־הָאֶפְסִיִּים 4 >
לכן אזהירכם אני האסור באדון להתהלך כאשר יאתה למשמרתכם אשר נקראתם לה׃ | 1 |
Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa.
בכל נמיכות וענוה ובארך רוח לשאת איש את רעהו באהבה׃ | 2 |
Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo.
ושקדו לשמר את אחדות הרוח באגדת השלום׃ | 3 |
Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
גוף אחד ורוח אחד כאשר גם נקראתם בתקות משמרתכם האחת׃ | 4 |
Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja.
אדון אחד אמונה אחת טבילה אחת׃ | 5 |
Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
אל ואב אחד לכל שהוא על כל ובכל ובתוך כלכם׃ | 6 |
Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.
אבל לכל אחד ואחד ממנו נתן החסד כמדת מתנת המשיח׃ | 7 |
Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo.
על כן הוא אומר עלה למרום שבה שבי ויתן מתנות לאדם׃ | 8 |
Kwa hiyo husema: “Alipopaa juu zaidi, aliteka mateka, akawapa wanadamu vipawa.”
ועלה שאמר מה הוא אם לא שירד ירד מקדם לתחתיות ארץ׃ | 9 |
(Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?
הירד הוא אשר גם עלה למעלה מכל השמים למען ימלא את הכל׃ | 10 |
Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.)
והוא נתן את אלה שליחים ואת אלה נביאים ואת אלה מבשרים ואת אלה רעים ומלמדים׃ | 11 |
Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu,
להשלים את הקדשים למעשה העבודה לבנין גוף המשיח׃ | 12 |
kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa
עד כי נגיע כלנו לאחדות האמונה ודעת בן האלהים כאיש אחד שלם לשעור קומת מלוא המשיח׃ | 13 |
mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.
ולא נהיה עוד ילדים נגרשים ונדפים בכל רוח הלמוד בתרמית בני אדם ומקשותם אשר שתו להתעות׃ | 14 |
Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu.
כי אם נדבר האמת באהבה ונגדלה בכל דבר לו למשיח שהוא הראש׃ | 15 |
Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo.
אשר ממנו כל הגוף בהיותו מרכב ומדבק בכל חבור השמוש כפי מדת הפעלה הנתונה לכל אבר ואבר ירבה ויגדל להשלמת בנינו באהבה׃ | 16 |
Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.
והנה זאת אני אמר ומעיד באדון כי מעתה לא תלכו עוד כיתר הגוים ההלכים בהבלי שכלם׃ | 17 |
Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao.
חשכי הדעת ומוזרים לחיי אלהים מפני אולתם אשר בהם כי טח מהשכיל לבבם׃ | 18 |
Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao.
אשר השמינו ויתנו את נפשם לזמה לעשות כל תועבה באהבת הבצע׃ | 19 |
Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.
ואתם לא כן למדתם את המשיח׃ | 20 |
Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo.
אם אמנם אתו שמעתם ובו למדתם כפי האמת בישוע׃ | 21 |
Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu.
אשר תסורו מדרכיכם הראשנים ותפשטו את האדם הישן הנשחת בתאות התרמית׃ | 22 |
Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu,
ili mfanywe upya roho na nia zenu,
ותלבשו את האדם החדש הנברא כדמות אלהים בצדקה וקדשת האמת׃ | 24 |
mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.
על כן הסירו מכם את השקר ודברו אמת איש את רעהו כי אברים כלנו יחד איש לאיש׃ | 25 |
Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja.
רגזו ואל תחטאו אל תשקע החמה על רגזכם׃ | 26 |
Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika,
wala msimpe ibilisi nafasi.
מי שגנב אל יסף לגנב כי אם ייגע ובידיו יעשה את הטוב למען יהיה לו לתת לאיש מחסור׃ | 28 |
Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.
כל דבר נבול לא יצא מפיכם כי אם הטוב והמועיל לבנות לפי הצרך למען יתן חן לשמעיו׃ | 29 |
Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.
ולא תעצבו את רוח הקדש של אלהים אשר נחתמתם בו אל יום הגאלה׃ | 30 |
Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
כל מרירות וחמה ורגז וצעקה וגדוף תסירו מכם עם כל הרשעה׃ | 31 |
Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu.
והיו טובים איש אל רעהו ורחמנים וסלחים איש לאחיו כאשר סלח לכם האלהים במשיח׃ | 32 |
Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.