< 1 טימותי 1 >
פולוס שליח ישוע המשיח כמצות האלהים מושיענו והאדון ישוע המשיח תקותנו׃ | 1 |
Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
אל טימותיוס בנו האמתי באמונה חסד ורחמים ושלום מאת אלהים אבינו והמשיח ישוע אדנינו׃ | 2 |
nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
הנה בלכתי למקדוניא בקשתי ממך לשבת באפסוס למען תזהיר מקצת אנשים שלא יורו תורה זרה׃ | 3 |
Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
ולא ישימו לבם להגדות וללמודי תולדות אין קץ המביאים יותר לשאלות מלבנות בית אלהים באמונה׃ | 4 |
Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
כי תכלית המצוה היא האהבה בלב טהור וברוח טובה ובאמונה לא צבועה׃ | 5 |
Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
יש אשר תעו ממנה ויפנו אחרי למודי תהו׃ | 6 |
Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
בחשבם להיות מורי תורה ואינם מבינים מה הם אמרים ומה הם מחליטים׃ | 7 |
Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
אבל ידענו כי התורה טובה היא אם יתנהג בה האדם כתורה׃ | 8 |
Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
בדעתו זאת כי חק לא הושם בעבור הצדיק אלא בעבור הסוררים והמרדים הרשעים והחטאים עשי זמה ונבלה מכי אב ומכי אם ומרצחים׃ | 9 |
Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
וזנים ושכבים את זכר וגנבי נפש וכזבים ונשבעים לשקר וכל מעשה הפך מן הלקח הבריא׃ | 10 |
sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
כפי בשורת כבוד האל המברך אשר פקדה עלי׃ | 11 |
Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
והנני מודה לישוע המשיח אדנינו המאזרני חיל כי חשבני נאמן וישימני למשרת לו׃ | 12 |
Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
אתי אשר מלפנים הייתי מגדף ומרדף ומחרף אבל רחמתי כי עשיתי מבלי דעת באין אמונה׃ | 13 |
ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
ויגדל עלי במאד מאד חסד אדנינו עם האמונה והאהבה במשיח ישוע׃ | 14 |
Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
נאמן הדבר וראוי להתקבל על כל כי המשיח ישוע בא לעולם להושיע את החטאים אשר אנכי הגדול בהם׃ | 15 |
Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
ובעבור זאת רחמתי למען אשר יראה ישוע המשיח בי בראשונה את כל ארך רוחו להיותי למופת לכל אשר יבאו להאמין בו לחיי עולם׃ (aiōnios ) | 16 |
lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele. (aiōnios )
ולמלך עולמים לאלהים הקים לעד והנעלם מעין והחכם לבדו לו הכבוד וההדר לעולמי עולמים אמן׃ (aiōn ) | 17 |
Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee—kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina. (aiōn )
את המצוה הזאת אני מצוך בני טימותיוס כפי הנבואות הקדמות עליך שתלחם לפיהן המלחמה הטובה׃ | 18 |
Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
לאחז באמונה וברוח הטובה אשר יש מאסים בה ותשבר אנית אמונתם׃ | 19 |
na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
ומהם הומניוס ואלכסנדר אשר מסרתים לשטן למען יוסרו לבלתי גדף עוד׃ | 20 |
Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.