< ג'ון 1 >
בראשית היה הדבר, והדבר היה עם האלוהים, ואלוהים היה הדבר. | 1 |
Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
הוא היה בראשית עם האלוהים. | 2 |
Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
דרכו נברא הכל, אין דבר שלא נברא על־ידו. | 3 |
Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
בו היו חיים, וחיים אלה היו האור לבני־האדם. | 4 |
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
האור מאיר בחושך, והחושך לא התגבר עליו. | 5 |
Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
אלוהים שלח אדם בשם יוחנן | 6 |
Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
להעיד על האור האמתי, כדי שכולם יאמינו בו. | 7 |
Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
יוחנן עצמו לא היה האור; הוא רק נשלח להעיד על האור | 8 |
Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
האמתי שבא לעולם כדי להאיר לכל בני־האדם. | 9 |
Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
האור בא אל העולם שנברא על ידו, אך העולם לא הכיר אותו. | 10 |
Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
הוא בא אל שלו, אך אלה לא קיבלו אותו. | 11 |
Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
אבל לכל אלה שהאמינו בו הוא העניק את הזכות להיות בני־אלוהים. | 12 |
Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
כל המאמינים בו נולדו מחדש – לא בלידה ביולוגית מגבר ואישה, ולא מרצון האדם, אלא מרצון האלוהים. | 13 |
Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
הדבר נהיה בשר ושכן בתוכינו. אנחנו ראינו את כבודו, כבוד הבן היחיד מהאב, מלא חסד ואמת. | 14 |
Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
יוחנן העיד עליו וקרא:”הנה האדם שאליו התכוונתי, כשסיפרתי לכם שאחרי עומד לבוא אדם גדול ונעלה ממני, כי הוא היה לפני שהייתי אני.“ | 15 |
Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
כולנו התברכנו בברכות רבות מעושרו ומחסדו. | 16 |
Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
כי בעוד שמשה רבנו מסר לנו את התורה, ישוע המשיח העניק לנו חסד ואמת. | 17 |
Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
איש לא ראה מעולם את האלוהים, מלבד בנו היחיד הנמצא בחיקו, והוא סיפר לנו על אביו. | 18 |
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
זוהי, אם כן, עדותו של יוחנן: כאשר שלחו אליו היהודים כוהנים ולווים מירושלים כדי לברר מי הוא, | 19 |
Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
יוחנן הודה מיד:”אינני המשיח!“ | 20 |
Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
”אם כן, מי אתה?“דרשו לדעת.”האם אתה אליהו?“”לא“, השיב יוחנן.”האם אתה הנביא?“”לא“השיב להם. | 21 |
Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
”מי אתה? מה יש לך לומר? ברצוננו לדעת מה להשיב לשולחינו.“ | 22 |
Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
”אני הקול הקורא במדבר כנבואת ישעיהו:’פנו דרך ה׳!‘“השיב יוחנן. | 23 |
Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
אנשים אלה, שנשלחו על־ידי הפרושים, המשיכו לשאול אותו:”אם אינך המשיח, אינך אליהו ואינך הנביא, מדוע אתה מטביל את האנשים?“ | 24 |
Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
”אני מטביל רק במים, “השיב יוחנן,”אולם דעו ביניכם עומד אדם שלא פגשתם מעולם. | 26 |
Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
למרות שהוא בא אחרי הוא היה לפני, ואיני ראוי אפילו להתיר את שרוך נעליו.“ | 27 |
Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
כל זה התרחש בכפר בית־עניה שעל חוף הירדן – במקום שבו נהג יוחנן להטביל. | 28 |
Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
למחרת ראה יוחנן את ישוע בא לקראתו והכריז:”הביטו! הנה שה האלוהים הנושא את חטאי העולם. | 29 |
Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
אליו התכוונתי כשסיפרתי לכם שאחרי עומד לבוא אדם גדול ונעלה ממני, כי הוא היה לפני שהייתי אני. | 30 |
Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
אני עצמי לא הכרתי אותו; אני באתי רק להטביל אנשים במים ולהצביע עליו לעם ישראל.“ | 31 |
Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
יוחנן סיפר להם שהוא ראה את רוח הקודש יורדת בדמות יונה ונחה על ישוע. | 32 |
Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
”לא הכרתי את ישוע לפני כן, “חזר ואמר יוחנן,”אולם כאשר אלוהים שלח אותי להטביל במים הוא אמר לי:’בראותך את רוח הקודש יורדת ונחה על איש, דע כי אותו אתה מבקש – זהו האיש שיטביל ברוח הקודש‘. | 33 |
Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
אני ראיתי את רוח הקודש יורדת ונחה על האיש הזה, ולכן אני מעיד שהוא בן האלוהים.“ | 34 |
Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
למחרת שוב עמד יוחנן באותו מקום עם שניים מתלמידיו. | 35 |
Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
בראותו את ישוע בא לקראתו הוא קרא:”הנה שה האלוהים!“ | 36 |
Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
כששמעו שני התלמידים את קריאתו של יוחנן, פנו ללכת בעקבות ישוע. | 37 |
Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
ישוע הביט לאחור וראה שהשניים הולכים בעקבותיו.”מה רצונכם?“שאל אותם.”רבי, היכן אתה גר?“השיבו בשאלה. | 38 |
Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
”בואו וראו“, ענה ישוע. השניים הלכו אחריו למקום מגוריו, ונשארו איתו משעה ארבע אחר־הצהריים עד הערב. | 39 |
Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
אַנְדְּרֵי, אחיו של שמעון פטרוס, היה אחד משני התלמידים שהלכו אחריו. | 40 |
Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
אַנְדְּרֵי הלך מיד לחפש את אחיו, וכשמצא אותו קרא בהתרגשות:”מצאנו את המשיח!“ | 41 |
Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
כשהביא אַנְדְּרֵי את פטרוס אל ישוע, הביט ישוע בפטרוס לרגע ואמר:”אתה אמנם שמעון בנו של יונה, אך מעתה ואילך תיקרא: פטרוס – כֵּיפָא!“ | 42 |
Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
למחרת החליט ישוע ללכת לגליל. הוא פגש בדרך את פיליפוס ואמר לו:”בוא אחרי.“ | 43 |
Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
פיליפוס היה מבית־צידה, עירם של אַנְדְּרֵי ופטרוס. | 44 |
Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
פיליפוס הלך לחפש את נתנאל, וכשמצא אותו קרא:”מצאנו את המשיח שעליו סיפרו משה רבנו והנביאים! שמו ישוע, בנו של יוסף מנצרת!“ | 45 |
Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
”נצרת?“קרא נתנאל בחוסר אמון.”איזה דבר טוב יכול לצאת מנצרת?“”בוא וראה במו עיניך“, הפציר בו פיליפוס. | 46 |
Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
כשראה ישוע את נתנאל בא לקראתו, קרא:”הנה בא לקראתנו בן ישראל אמתי – אדם ישר אמתי שאין בו מרמה.“ | 47 |
Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
”כיצד אתה יודע מי אני ומה אני?“תמה נתנאל.”ראיתי אותך יושב תחת עץ התאנה עוד לפני שפיליפוס מצא אותך“, ענה ישוע. | 48 |
Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
”אדוני, אתה באמת בן־האלוהים, מלך ישראל!“קרא נתנאל. | 49 |
Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
”האם אתה מאמין בכך רק משום שאמרתי כי ראיתי אותך יושב תחת עץ התאנה?“שאל ישוע.”עוד תראה דברים גדולים מאלה! | 50 |
Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
אפילו תראה את השמים נפתחים ומלאכי אלוהים עולים ויורדים על בן־האדם.“ | 51 |
Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”