< תהילים 119 >
אַשְׁרֵי תְמִֽימֵי־דָרֶךְ הַֽהֹלְכִים בְּתוֹרַת יְהוָֽה׃ | 1 |
Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
אַשְׁרֵי נֹצְרֵי עֵדֹתָיו בְּכָל־לֵב יִדְרְשֽׁוּהוּ׃ | 2 |
Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
אַף לֹֽא־פָעֲלוּ עַוְלָה בִּדְרָכָיו הָלָֽכוּ׃ | 3 |
Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.
אַתָּה צִוִּיתָה פִקֻּדֶיךָ לִשְׁמֹר מְאֹֽד׃ | 4 |
Umetoa maagizo yako ili tuyatii kwa ukamilifu.
אַחֲלַי יִכֹּנוּ דְרָכָי לִשְׁמֹר חֻקֶּֽיךָ׃ | 5 |
Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako!
אָז לֹא־אֵבוֹשׁ בְּהַבִּיטִי אֶל־כָּל־מִצְוֺתֶֽיךָ׃ | 6 |
Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote.
אוֹדְךָ בְּיֹשֶׁר לֵבָב בְּלָמְדִי מִשְׁפְּטֵי צִדְקֶֽךָ׃ | 7 |
Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki.
אֶת־חֻקֶּיךָ אֶשְׁמֹר אַֽל־תַּעַזְבֵנִי עַד־מְאֹֽד׃ | 8 |
Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.
בַּמֶּה יְזַכֶּה־נַּעַר אֶת־אָרְחוֹ לִשְׁמֹר כִּדְבָרֶֽךָ׃ | 9 |
Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani? Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.
בְּכָל־לִבִּי דְרַשְׁתִּיךָ אַל־תַּשְׁגֵּנִי מִמִּצְוֺתֶֽיךָ׃ | 10 |
Ninakutafuta kwa moyo wangu wote, usiniache niende mbali na amri zako.
בְּלִבִּי צָפַנְתִּי אִמְרָתֶךָ לְמַעַן לֹא אֶֽחֱטָא־לָֽךְ׃ | 11 |
Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi.
בָּרוּךְ אַתָּה יְהוָה לַמְּדֵנִי חֻקֶּֽיךָ׃ | 12 |
Sifa ni zako, Ee Bwana, nifundishe maagizo yako.
בִּשְׂפָתַי סִפַּרְתִּי כֹּל מִשְׁפְּטֵי־פִֽיךָ׃ | 13 |
Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote zinazotoka katika kinywa chako.
בְּדֶרֶךְ עֵדְוֺתֶיךָ שַּׂשְׂתִּי כְּעַל כָּל־הֽוֹן׃ | 14 |
Ninafurahia kufuata sheria zako kama mtu afurahiaye mali nyingi.
בְּפִקֻּדֶיךָ אָשִׂיחָה וְאַבִּיטָה אֹרְחֹתֶֽיךָ׃ | 15 |
Ninatafakari maagizo yako na kuziangalia njia zako.
בְּחֻקֹּתֶיךָ אֶֽשְׁתַּעֲשָׁע לֹא אֶשְׁכַּח דְּבָרֶֽךָ׃ | 16 |
Ninafurahia maagizo yako, wala sitalipuuza neno lako.
גְּמֹל עַֽל־עַבְדְּךָ אֶֽחְיֶה וְאֶשְׁמְרָה דְבָרֶֽךָ׃ | 17 |
Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi; nitalitii neno lako.
גַּל־עֵינַי וְאַבִּיטָה נִפְלָאוֹת מִתּוֹרָתֶֽךָ׃ | 18 |
Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
גֵּר אָנֹכִי בָאָרֶץ אַל־תַּסְתֵּר מִמֶּנִּי מִצְוֺתֶֽיךָ׃ | 19 |
Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako.
גָּרְסָה נַפְשִׁי לְתַאֲבָה אֶֽל־מִשְׁפָּטֶיךָ בְכָל־עֵֽת׃ | 20 |
Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa juu ya sheria zako wakati wote.
גָּעַרְתָּ זֵדִים אֲרוּרִים הַשֹּׁגִים מִמִּצְוֺתֶֽיךָ׃ | 21 |
Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.
גַּל מֵֽעָלַי חֶרְפָּה וָבוּז כִּי עֵדֹתֶיךָ נָצָֽרְתִּי׃ | 22 |
Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako.
גַּם יָֽשְׁבוּ שָׂרִים בִּי נִדְבָּרוּ עַבְדְּךָ יָשִׂיחַ בְּחֻקֶּֽיךָ׃ | 23 |
Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
גַּֽם־עֵדֹתֶיךָ שַׁעֲשֻׁעָי אַנְשֵׁי עֲצָתִֽי׃ | 24 |
Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu.
דָּֽבְקָה לֶעָפָר נַפְשִׁי חַיֵּנִי כִּדְבָרֶֽךָ׃ | 25 |
Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
דְּרָכַי סִפַּרְתִּי וַֽתַּעֲנֵנִי לַמְּדֵנִי חֻקֶּֽיךָ׃ | 26 |
Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.
דֶּֽרֶךְ־פִּקּוּדֶיךָ הֲבִינֵנִי וְאָשִׂיחָה בְּנִפְלְאוֹתֶֽיךָ׃ | 27 |
Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
דָּלְפָה נַפְשִׁי מִתּוּגָה קַיְּמֵנִי כִּדְבָרֶֽךָ׃ | 28 |
Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
דֶּֽרֶךְ־שֶׁקֶר הָסֵר מִמֶּנִּי וְֽתוֹרָתְךָ חָנֵּֽנִי׃ | 29 |
Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
דֶּֽרֶךְ־אֱמוּנָה בָחָרְתִּי מִשְׁפָּטֶיךָ שִׁוִּֽיתִי׃ | 30 |
Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
דָּבַקְתִּי בְעֵֽדְוֺתֶיךָ יְהוָה אַל־תְּבִישֵֽׁנִי׃ | 31 |
Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana, usiniache niaibishwe.
דֶּֽרֶךְ־מִצְוֺתֶיךָ אָרוּץ כִּי תַרְחִיב לִבִּֽי׃ | 32 |
Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.
הוֹרֵנִי יְהוָה דֶּרֶךְ חֻקֶּיךָ וְאֶצְּרֶנָּה עֵֽקֶב׃ | 33 |
Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho.
הֲבִינֵנִי וְאֶצְּרָה תֽוֹרָתֶךָ וְאֶשְׁמְרֶנָּה בְכָל־לֵֽב׃ | 34 |
Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote.
הַדְרִיכֵנִי בִּנְתִיב מִצְוֺתֶיךָ כִּי־בוֹ חָפָֽצְתִּי׃ | 35 |
Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha.
הַט־לִבִּי אֶל־עֵדְוֺתֶיךָ וְאַל אֶל־בָּֽצַע׃ | 36 |
Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
הַעֲבֵר עֵינַי מֵרְאוֹת שָׁוְא בִּדְרָכֶךָ חַיֵּֽנִי׃ | 37 |
Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
הָקֵם לְעַבְדְּךָ אִמְרָתֶךָ אֲשֶׁר לְיִרְאָתֶֽךָ׃ | 38 |
Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa.
הַעֲבֵר חֶרְפָּתִי אֲשֶׁר יָגֹרְתִּי כִּי מִשְׁפָּטֶיךָ טוֹבִֽים׃ | 39 |
Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema.
הִנֵּה תָּאַבְתִּי לְפִקֻּדֶיךָ בְּצִדְקָתְךָ חַיֵּֽנִי׃ | 40 |
Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.
וִֽיבֹאֻנִי חֲסָדֶךָ יְהוָה תְּשֽׁוּעָתְךָ כְּאִמְרָתֶֽךָ׃ | 41 |
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
וְאֶֽעֱנֶה חֹרְפִי דָבָר כִּֽי־בָטַחְתִּי בִּדְבָרֶֽךָ׃ | 42 |
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
וְֽאַל־תַּצֵּל מִפִּי דְבַר־אֱמֶת עַד־מְאֹד כִּי לְמִשְׁפָּטֶךָ יִחָֽלְתִּי׃ | 43 |
Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
וְאֶשְׁמְרָה תוֹרָתְךָ תָמִיד לְעוֹלָם וָעֶֽד׃ | 44 |
Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
וְאֶתְהַלְּכָה בָרְחָבָה כִּי פִקֻּדֶיךָ דָרָֽשְׁתִּי׃ | 45 |
Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
וַאֲדַבְּרָה בְעֵדֹתֶיךָ נֶגֶד מְלָכִים וְלֹא אֵבֽוֹשׁ׃ | 46 |
Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,
וְאֶשְׁתַּֽעֲשַׁע בְּמִצְוֺתֶיךָ אֲשֶׁר אָהָֽבְתִּי׃ | 47 |
kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.
וְאֶשָּֽׂא־כַפַּי אֶֽל־מִצְוֺתֶיךָ אֲשֶׁר אָהָבְתִּי וְאָשִׂיחָה בְחֻקֶּֽיךָ׃ | 48 |
Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.
זְכֹר־דָּבָר לְעַבְדֶּךָ עַל אֲשֶׁר יִֽחַלְתָּֽנִי׃ | 49 |
Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.
זֹאת נֶחָמָתִי בְעָנְיִי כִּי אִמְרָתְךָ חִיָּֽתְנִי׃ | 50 |
Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
זֵדִים הֱלִיצֻנִי עַד־מְאֹד מִתּֽוֹרָתְךָ לֹא נָטִֽיתִי׃ | 51 |
Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.
זָכַרְתִּי מִשְׁפָּטֶיךָ מֵעוֹלָם ׀ יְהוָה וָֽאֶתְנֶחָֽם׃ | 52 |
Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.
זַלְעָפָה אֲחָזַתְנִי מֵרְשָׁעִים עֹזְבֵי תּוֹרָתֶֽךָ׃ | 53 |
Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.
זְמִרוֹת הָֽיוּ־לִי חֻקֶּיךָ בְּבֵית מְגוּרָֽי׃ | 54 |
Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.
זָכַרְתִּי בַלַּיְלָה שִׁמְךָ יְהוָה וָֽאֶשְׁמְרָה תּוֹרָתֶֽךָ׃ | 55 |
Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako.
זֹאת הָֽיְתָה־לִּי כִּי פִקֻּדֶיךָ נָצָֽרְתִּי׃ | 56 |
Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.
חֶלְקִי יְהוָה אָמַרְתִּי לִשְׁמֹר דְּבָרֶֽיךָ׃ | 57 |
Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.
חִלִּיתִי פָנֶיךָ בְכָל־לֵב חָנֵּנִי כְּאִמְרָתֶֽךָ׃ | 58 |
Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.
חִשַּׁבְתִּי דְרָכָי וָאָשִׁיבָה רַגְלַי אֶל־עֵדֹתֶֽיךָ׃ | 59 |
Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
חַשְׁתִּי וְלֹא הִתְמַהְמָהְתִּי לִשְׁמֹר מִצְוֺתֶֽיךָ׃ | 60 |
Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
חֶבְלֵי רְשָׁעִים עִוְּדֻנִי תּֽוֹרָתְךָ לֹא שָׁכָֽחְתִּי׃ | 61 |
Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.
חֲצֽוֹת־לַיְלָה אָקוּם לְהוֹדוֹת לָךְ עַל מִשְׁפְּטֵי צִדְקֶֽךָ׃ | 62 |
Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.
חָבֵר אָנִי לְכָל־אֲשֶׁר יְרֵאוּךָ וּלְשֹׁמְרֵי פִּקּוּדֶֽיךָ׃ | 63 |
Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.
חַסְדְּךָ יְהוָה מָלְאָה הָאָרֶץ חֻקֶּיךָ לַמְּדֵֽנִי׃ | 64 |
Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.
טוֹב עָשִׂיתָ עִֽם־עַבְדְּךָ יְהוָה כִּדְבָרֶֽךָ׃ | 65 |
Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
טוּב טַעַם וָדַעַת לַמְּדֵנִי כִּי בְמִצְוֺתֶיךָ הֶאֱמָֽנְתִּי׃ | 66 |
Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.
טֶרֶם אֶעֱנֶה אֲנִי שֹׁגֵג וְעַתָּה אִמְרָתְךָ שָׁמָֽרְתִּי׃ | 67 |
Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.
טוֹב־אַתָּה וּמֵטִיב לַמְּדֵנִי חֻקֶּֽיךָ׃ | 68 |
Wewe ni mwema, unalotenda ni jema, nifundishe maagizo yako.
טָפְלוּ עָלַי שֶׁקֶר זֵדִים אֲנִי בְּכָל־לֵב ׀ אֱצֹּר פִּקּוּדֶֽיךָ׃ | 69 |
Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.
טָפַשׁ כַּחֵלֶב לִבָּם אֲנִי תּוֹרָתְךָ שִֽׁעֲשָֽׁעְתִּי׃ | 70 |
Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.
טֽוֹב־לִי כִֽי־עֻנֵּיתִי לְמַעַן אֶלְמַד חֻקֶּֽיךָ׃ | 71 |
Ilikuwa vyema mimi kupata shida ili nipate kujifunza maagizo yako.
טֽוֹב־לִי תֽוֹרַת־פִּיךָ מֵאַלְפֵי זָהָב וָכָֽסֶף׃ | 72 |
Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.
יָדֶיךָ עָשׂוּנִי וַֽיְכוֹנְנוּנִי הֲבִינֵנִי וְאֶלְמְדָה מִצְוֺתֶֽיךָ׃ | 73 |
Mikono yako ilinifanya na kuniumba, nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
יְרֵאֶיךָ יִרְאוּנִי וְיִשְׂמָחוּ כִּי לִדְבָרְךָ יִחָֽלְתִּי׃ | 74 |
Wakuchao wafurahie wanaponiona, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
יָדַעְתִּי יְהוָה כִּי־צֶדֶק מִשְׁפָּטֶיךָ וֶאֱמוּנָה עִנִּיתָֽנִי׃ | 75 |
Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.
יְהִי־נָא חַסְדְּךָ לְנַחֲמֵנִי כְּאִמְרָתְךָ לְעַבְדֶּֽךָ׃ | 76 |
Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu, sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
יְבֹאוּנִי רַחֲמֶיךָ וְאֶֽחְיֶה כִּי־תֽוֹרָתְךָ שַֽׁעֲשֻׁעָֽי׃ | 77 |
Huruma yako na inijie ili nipate kuishi, kwa kuwa naifurahia sheria yako.
יֵבֹשׁוּ זֵדִים כִּי־שֶׁקֶר עִוְּתוּנִי אֲנִי אָשִׂיחַ בְּפִקּוּדֶֽיךָ׃ | 78 |
Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
יָשׁוּבוּ לִי יְרֵאֶיךָ וידעו וְיֹדְעֵי עֵדֹתֶֽיךָ׃ | 79 |
Wale wakuchao na wanigeukie mimi, hao ambao wanazielewa sheria zako.
יְהִֽי־לִבִּי תָמִים בְּחֻקֶּיךָ לְמַעַן לֹא אֵבֽוֹשׁ׃ | 80 |
Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako, ili nisiaibishwe.
כָּלְתָה לִתְשׁוּעָתְךָ נַפְשִׁי לִדְבָרְךָ יִחָֽלְתִּי׃ | 81 |
Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.
כָּלוּ עֵינַי לְאִמְרָתֶךָ לֵאמֹר מָתַי תְּֽנַחֲמֵֽנִי׃ | 82 |
Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifajiri lini?”
כִּֽי־הָיִיתִי כְּנֹאד בְּקִיטוֹר חֻקֶּיךָ לֹא שָׁכָֽחְתִּי׃ | 83 |
Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi, bado sijasahau maagizo yako.
כַּמָּה יְמֵֽי־עַבְדֶּךָ מָתַי תַּעֲשֶׂה בְרֹדְפַי מִשְׁפָּֽט׃ | 84 |
Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini? Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?
כָּֽרוּ־לִי זֵדִים שִׁיחוֹת אֲשֶׁר לֹא כְתוֹרָתֶֽךָ׃ | 85 |
Wenye majivuno wananichimbia mashimo, kinyume na sheria yako.
כָּל־מִצְוֺתֶיךָ אֱמוּנָה שֶׁקֶר רְדָפוּנִי עָזְרֵֽנִי׃ | 86 |
Amri zako zote ni za kuaminika; unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.
כִּמְעַט כִּלּוּנִי בָאָרֶץ וַאֲנִי לֹא־עָזַבְתִּי פִקֻּודֶֽיךָ׃ | 87 |
Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia, lakini sijaacha mausia yako.
כְּחַסְדְּךָ חַיֵּנִי וְאֶשְׁמְרָה עֵדוּת פִּֽיךָ׃ | 88 |
Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako, nami nitatii sheria za kinywa chako.
לְעוֹלָם יְהוָה דְּבָרְךָ נִצָּב בַּשָּׁמָֽיִם׃ | 89 |
Ee Bwana, neno lako ni la milele, linasimama imara mbinguni.
לְדֹר וָדֹר אֱמֽוּנָתֶךָ כּוֹנַנְתָּ אֶרֶץ וַֽתַּעֲמֹֽד׃ | 90 |
Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote, umeiumba dunia, nayo inadumu.
לְֽמִשְׁפָּטֶיךָ עָמְדוּ הַיּוֹם כִּי הַכֹּל עֲבָדֶֽיךָ׃ | 91 |
Sheria zako zinadumu hadi leo, kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
לוּלֵי תוֹרָתְךָ שַׁעֲשֻׁעָי אָז אָבַדְתִּי בְעָנְיִֽי׃ | 92 |
Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.
לְעוֹלָם לֹא־אֶשְׁכַּח פִּקּוּדֶיךָ כִּי בָם חִיִּיתָֽנִי׃ | 93 |
Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
לְֽךָ־אֲנִי הוֹשִׁיעֵנִי כִּי פִקּוּדֶיךָ דָרָֽשְׁתִּי׃ | 94 |
Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
לִי קִוּוּ רְשָׁעִים לְאַבְּדֵנִי עֵדֹתֶיךָ אֶתְבּוֹנָֽן׃ | 95 |
Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
לְֽכָל תִּכְלָה רָאִיתִי קֵץ רְחָבָה מִצְוָתְךָ מְאֹֽד׃ | 96 |
Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
מָֽה־אָהַבְתִּי תוֹרָתֶךָ כָּל־הַיּוֹם הִיא שִׂיחָתִֽי׃ | 97 |
Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
מֵאֹיְבַי תְּחַכְּמֵנִי מִצְוֺתֶךָ כִּי לְעוֹלָם הִיא־לִֽי׃ | 98 |
Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
מִכָּל־מְלַמְּדַי הִשְׂכַּלְתִּי כִּי עֵדְוֺתֶיךָ שִׂיחָה לִֽֿי׃ | 99 |
Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
מִזְּקֵנִים אֶתְבּוֹנָן כִּי פִקּוּדֶיךָ נָצָֽרְתִּי׃ | 100 |
Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
מִכָּל־אֹרַח רָע כָּלִאתִי רַגְלָי לְמַעַן אֶשְׁמֹר דְּבָרֶֽךָ׃ | 101 |
Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
מִמִּשְׁפָּטֶיךָ לֹא־סָרְתִּי כִּֽי־אַתָּה הוֹרֵתָֽנִי׃ | 102 |
Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
מַה־נִּמְלְצוּ לְחִכִּי אִמְרָתֶךָ מִדְּבַשׁ לְפִֽי׃ | 103 |
Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
מִפִּקּוּדֶיךָ אֶתְבּוֹנָן עַל־כֵּן שָׂנֵאתִי ׀ כָּל־אֹרַח שָֽׁקֶר׃ | 104 |
Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
נֵר־לְרַגְלִי דְבָרֶךָ וְאוֹר לִנְתִיבָתִֽי׃ | 105 |
Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
נִשְׁבַּעְתִּי וָאֲקַיֵּמָה לִשְׁמֹר מִשְׁפְּטֵי צִדְקֶֽךָ׃ | 106 |
Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
נַעֲנֵיתִי עַד־מְאֹד יְהוָה חַיֵּנִי כִדְבָרֶֽךָ׃ | 107 |
Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
נִדְבוֹת פִּי רְצֵה־נָא יְהוָה וּֽמִשְׁפָּטֶיךָ לַמְּדֵֽנִי׃ | 108 |
Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
נַפְשִׁי בְכַפִּי תָמִיד וְתֽוֹרָתְךָ לֹא שָׁכָֽחְתִּי׃ | 109 |
Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
נָתְנוּ רְשָׁעִים פַּח לִי וּמִפִּקּוּדֶיךָ לֹא תָעִֽיתִי׃ | 110 |
Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
נָחַלְתִּי עֵדְוֺתֶיךָ לְעוֹלָם כִּֽי־שְׂשׂוֹן לִבִּי הֵֽמָּה׃ | 111 |
Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
נָטִיתִי לִבִּי לַעֲשׂוֹת חֻקֶּיךָ לְעוֹלָם עֵֽקֶב׃ | 112 |
Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
סֵעֲפִים שָׂנֵאתִי וְֽתוֹרָתְךָ אָהָֽבְתִּי׃ | 113 |
Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
סִתְרִי וּמָגִנִּי אָתָּה לִדְבָרְךָ יִחָֽלְתִּי׃ | 114 |
Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
סֽוּרוּ־מִמֶּנִּי מְרֵעִים וְאֶצְּרָה מִצְוֺת אֱלֹהָֽי׃ | 115 |
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
סָמְכֵנִי כְאִמְרָתְךָ וְאֶֽחְיֶה וְאַל־תְּבִישֵׁנִי מִשִּׂבְרִֽי׃ | 116 |
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
סְעָדֵנִי וְאִוָּשֵׁעָה וְאֶשְׁעָה בְחֻקֶּיךָ תָמִֽיד׃ | 117 |
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.
סָלִיתָ כָּל־שׁוֹגִים מֵחֻקֶּיךָ כִּי־שֶׁקֶר תַּרְמִיתָֽם׃ | 118 |
Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako, kwa maana udanganyifu wao ni bure.
סִגִים הִשְׁבַּתָּ כָל־רִשְׁעֵי־אָרֶץ לָכֵן אָהַבְתִּי עֵדֹתֶֽיךָ׃ | 119 |
Waovu wa nchi unawatupa kama takataka, kwa hivyo nazipenda sheria zako.
סָמַר מִפַּחְדְּךָ בְשָׂרִי וּֽמִמִּשְׁפָּטֶיךָ יָרֵֽאתִי׃ | 120 |
Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe, ninaziogopa sheria zako.
עָשִׂיתִי מִשְׁפָּט וָצֶדֶק בַּל־תַּנִּיחֵנִי לְעֹֽשְׁקָֽי׃ | 121 |
Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
עֲרֹב עַבְדְּךָ לְטוֹב אַֽל־יַעַשְׁקֻנִי זֵדִֽים׃ | 122 |
Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
עֵינַי כָּלוּ לִֽישׁוּעָתֶךָ וּלְאִמְרַת צִדְקֶֽךָ׃ | 123 |
Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
עֲשֵׂה עִם־עַבְדְּךָ כְחַסְדֶּךָ וְחֻקֶּיךָ לַמְּדֵֽנִי׃ | 124 |
Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
עַבְדְּךָ־אָנִי הֲבִינֵנִי וְאֵדְעָה עֵדֹתֶֽיךָ׃ | 125 |
Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
עֵת לַעֲשׂוֹת לַיהוָה הֵפֵרוּ תּוֹרָתֶֽךָ׃ | 126 |
Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.
עַל־כֵּן אָהַבְתִּי מִצְוֺתֶיךָ מִזָּהָב וּמִפָּֽז׃ | 127 |
Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu, naam, zaidi ya dhahabu safi,
עַל־כֵּן ׀ כָּל־פִּקּוּדֵי כֹל יִשָּׁרְתִּי כָּל־אֹרַח שֶׁקֶר שָׂנֵֽאתִי׃ | 128 |
na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili, nachukia kila njia potovu.
פְּלָאוֹת עֵדְוֺתֶיךָ עַל־כֵּן נְצָרָתַם נַפְשִֽׁי׃ | 129 |
Sheria zako ni za ajabu, hivyo ninazitii.
פֵּתַח דְּבָרֶיךָ יָאִיר מֵבִין פְּתָיִֽים׃ | 130 |
Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru, kunampa mjinga ufahamu.
פִּֽי־פָעַרְתִּי וָאֶשְׁאָפָה כִּי לְמִצְוֺתֶיךָ יָאָֽבְתִּי׃ | 131 |
Nimefungua kinywa changu na kuhema, nikitamani amri zako.
פְּנֵה־אֵלַי וְחָנֵּנִי כְּמִשְׁפָּט לְאֹהֲבֵי שְׁמֶֽךָ׃ | 132 |
Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote wale wanaolipenda jina lako.
פְּעָמַי הָכֵן בְּאִמְרָתֶךָ וְֽאַל־תַּשְׁלֶט־בִּי כָל־אָֽוֶן׃ | 133 |
Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako, usiache dhambi yoyote initawale.
פְּדֵנִי מֵעֹשֶׁק אָדָם וְאֶשְׁמְרָה פִּקּוּדֶֽיךָ׃ | 134 |
Niokoe na uonevu wa wanadamu, ili niweze kutii mausia yako.
פָּנֶיךָ הָאֵר בְּעַבְדֶּךָ וְלַמְּדֵנִי אֶת־חֻקֶּֽיךָ׃ | 135 |
Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
פַּלְגֵי־מַיִם יָרְדוּ עֵינָי עַל לֹא־שָׁמְרוּ תוֹרָתֶֽךָ׃ | 136 |
Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
צַדִּיק אַתָּה יְהוָה וְיָשָׁר מִשְׁפָּטֶֽיךָ׃ | 137 |
Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
צִוִּיתָ צֶדֶק עֵדֹתֶיךָ וֶֽאֱמוּנָה מְאֹֽד׃ | 138 |
Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
צִמְּתַתְנִי קִנְאָתִי כִּֽי־שָׁכְחוּ דְבָרֶיךָ צָרָֽי׃ | 139 |
Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
צְרוּפָה אִמְרָתְךָ מְאֹד וְֽעַבְדְּךָ אֲהֵבָֽהּ׃ | 140 |
Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
צָעִיר אָנֹכִי וְנִבְזֶה פִּקֻּדֶיךָ לֹא שָׁכָֽחְתִּי׃ | 141 |
Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
צִדְקָתְךָ צֶדֶק לְעוֹלָם וְֽתוֹרָתְךָ אֱמֶֽת׃ | 142 |
Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
צַר־וּמָצוֹק מְצָאוּנִי מִצְוֺתֶיךָ שַׁעֲשֻׁעָֽי׃ | 143 |
Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
צֶדֶק עֵדְוֺתֶיךָ לְעוֹלָם הֲבִינֵנִי וְאֶחְיֶֽה׃ | 144 |
Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
קָרָאתִי בְכָל־לֵב עֲנֵנִי יְהוָה חֻקֶּיךָ אֶצֹּֽרָה׃ | 145 |
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
קְרָאתִיךָ הוֹשִׁיעֵנִי וְאֶשְׁמְרָה עֵדֹתֶֽיךָ׃ | 146 |
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
קִדַּמְתִּי בַנֶּשֶׁף וָאֲשַׁוֵּעָה לדבריך לִדְבָרְךָ יִחָֽלְתִּי׃ | 147 |
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
קִדְּמוּ עֵינַי אַשְׁמֻרוֹת לָשִׂיחַ בְּאִמְרָתֶֽךָ׃ | 148 |
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
קוֹלִי שִׁמְעָה כְחַסְדֶּךָ יְהוָה כְּֽמִשְׁפָּטֶךָ חַיֵּֽנִי׃ | 149 |
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
קָרְבוּ רֹדְפֵי זִמָּה מִתּוֹרָתְךָ רָחָֽקוּ׃ | 150 |
Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
קָרוֹב אַתָּה יְהוָה וְֽכָל־מִצְוֺתֶיךָ אֱמֶֽת׃ | 151 |
Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
קֶדֶם יָדַעְתִּי מֵעֵדֹתֶיךָ כִּי לְעוֹלָם יְסַדְתָּֽם׃ | 152 |
Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
רְאֵֽה־עָנְיִי וְחַלְּצֵנִי כִּי־תֽוֹרָתְךָ לֹא שָׁכָֽחְתִּי׃ | 153 |
Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako.
רִיבָה רִיבִי וּגְאָלֵנִי לְאִמְרָתְךָ חַיֵּֽנִי׃ | 154 |
Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
רָחוֹק מֵרְשָׁעִים יְשׁוּעָה כִּֽי־חֻקֶּיךָ לֹא דָרָֽשׁוּ׃ | 155 |
Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
רַחֲמֶיךָ רַבִּים ׀ יְהוָה כְּֽמִשְׁפָּטֶיךָ חַיֵּֽנִי׃ | 156 |
Ee Bwana, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
רַבִּים רֹדְפַי וְצָרָי מֵעֵדְוֺתֶיךָ לֹא נָטִֽיתִי׃ | 157 |
Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako.
רָאִיתִי בֹגְדִים וָֽאֶתְקוֹטָטָה אֲשֶׁר אִמְרָתְךָ לֹא שָׁמָֽרוּ׃ | 158 |
Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako.
רְאֵה כִּי־פִקּוּדֶיךָ אָהָבְתִּי יְהוָה כְּֽחַסְדְּךָ חַיֵּֽנִי׃ | 159 |
Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.
רֹאשׁ־דְּבָרְךָ אֱמֶת וּלְעוֹלָם כָּל־מִשְׁפַּט צִדְקֶֽךָ׃ | 160 |
Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.
שָׂרִים רְדָפוּנִי חִנָּם ומדבריך וּמִדְּבָרְךָ פָּחַד לִבִּֽי׃ | 161 |
Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
שָׂשׂ אָנֹכִֽי עַל־אִמְרָתֶךָ כְּמוֹצֵא שָׁלָל רָֽב׃ | 162 |
Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
שֶׁקֶר שָׂנֵאתִי וַאֲתַעֵבָה תּוֹרָתְךָ אָהָֽבְתִּי׃ | 163 |
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
שֶׁבַע בַּיּוֹם הִלַּלְתִּיךָ עַל מִשְׁפְּטֵי צִדְקֶֽךָ׃ | 164 |
Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
שָׁלוֹם רָב לְאֹהֲבֵי תוֹרָתֶךָ וְאֵֽין־לָמוֹ מִכְשֽׁוֹל׃ | 165 |
Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
שִׂבַּרְתִּי לִֽישׁוּעָתְךָ יְהוָה וּֽמִצְוֺתֶיךָ עָשִֽׂיתִי׃ | 166 |
Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
שָֽׁמְרָה נַפְשִׁי עֵדֹתֶיךָ וָאֹהֲבֵם מְאֹֽד׃ | 167 |
Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
שָׁמַרְתִּי פִקּוּדֶיךָ וְעֵדֹתֶיךָ כִּי כָל־דְּרָכַי נֶגְדֶּֽךָ׃ | 168 |
Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
תִּקְרַב רִנָּתִי לְפָנֶיךָ יְהוָה כִּדְבָרְךָ הֲבִינֵֽנִי׃ | 169 |
Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako, nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
תָּבוֹא תְחִנָּתִי לְפָנֶיךָ כְּאִמְרָתְךָ הַצִּילֵֽנִי׃ | 170 |
Maombi yangu na yafike mbele zako, niokoe sawasawa na ahadi yako.
תַּבַּעְנָה שְׂפָתַי תְּהִלָּה כִּי תְלַמְּדֵנִי חֻקֶּֽיךָ׃ | 171 |
Midomo yangu na ibubujike sifa, kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
תַּעַן לְשׁוֹנִי אִמְרָתֶךָ כִּי כָל־מִצְוֺתֶיךָ צֶּֽדֶק׃ | 172 |
Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
תְּהִֽי־יָדְךָ לְעָזְרֵנִי כִּי פִקּוּדֶיךָ בָחָֽרְתִּי׃ | 173 |
Mkono wako uwe tayari kunisaidia, kwa kuwa nimechagua mausia yako.
תָּאַבְתִּי לִֽישׁוּעָתְךָ יְהוָה וְתֽוֹרָתְךָ שַׁעֲשֻׁעָֽי׃ | 174 |
Ee Bwana, ninatamani wokovu wako, na sheria yako ni furaha yangu.
תְּֽחִי־נַפְשִׁי וּֽתְהַֽלְלֶךָּ וּֽמִשְׁפָּטֶךָ יַעֲזְרֻֽנִי׃ | 175 |
Nijalie kuishi ili nipate kukusifu, na sheria zako zinitegemeze.
תָּעִיתִי כְּשֶׂה אֹבֵד בַּקֵּשׁ עַבְדֶּךָ כִּי מִצְוֺתֶיךָ לֹא שָׁכָֽחְתִּי׃ | 176 |
Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.