< תהילים 99 >

יהוה מלך ירגזו עמים ישב כרובים תנוט הארץ 1
Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
יהוה בציון גדול ורם הוא על-כל-העמים 2
Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
יודו שמך גדול ונורא קדוש הוא 3
Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
ועז מלך משפט אהב אתה כוננת מישרים משפט וצדקה ביעקב אתה עשית 4
Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
רוממו יהוה אלהינו והשתחוו להדם רגליו קדוש הוא 5
Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
משה ואהרן בכהניו ושמואל בקראי שמו קראים אל-יהוה והוא יענם 6
Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
בעמוד ענן ידבר אליהם שמרו עדתיו וחק נתן-למו 7
Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
יהוה אלהינו אתה עניתם אל נשא היית להם ונקם על-עלילותם 8
Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
רוממו יהוה אלהינו והשתחוו להר קדשו כי-קדוש יהוה אלהינו 9
Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

< תהילים 99 >