< תהילים 97 >

יהוה מלך תגל הארץ ישמחו איים רבים 1
Bwana anatawala, nchi na ifurahi, visiwa vyote vishangilie.
ענן וערפל סביביו צדק ומשפט מכון כסאו 2
Mawingu na giza nene vinamzunguka, haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi.
אש לפניו תלך ותלהט סביב צריו 3
Moto hutangulia mbele zake na huteketeza adui zake pande zote.
האירו ברקיו תבל ראתה ותחל הארץ 4
Umeme wake wa radi humulika dunia, nchi huona na kutetemeka.
הרים--כדונג נמסו מלפני יהוה מלפני אדון כל-הארץ 5
Milima huyeyuka kama nta mbele za Bwana, mbele za Bwana wa dunia yote.
הגידו השמים צדקו וראו כל-העמים כבודו 6
Mbingu zinatangaza haki yake, na mataifa yote huona utukufu wake.
יבשו כל-עבדי פסל-- המתהללים באלילים השתחוו-לו כל-אלהים 7
Wote waabuduo sanamu waaibishwa, wale wajisifiao sanamu: mwabuduni yeye, enyi miungu yote!
שמעה ותשמח ציון ותגלנה בנות יהודה-- למען משפטיך יהוה 8
Sayuni husikia na kushangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana.
כי-אתה יהוה עליון על-כל-הארץ מאד נעלית על-כל-אלהים 9
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; umetukuka sana juu ya miungu yote.
אהבי יהוה שנאו-רע שמר נפשות חסידיו מיד רשעים יצילם 10
Wale wanaompenda Bwana na wauchukie uovu, kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu.
אור זרע לצדיק ולישרי-לב שמחה 11
Nuru huangaza wenye haki na furaha kwa watu wanyofu wa moyo.
שמחו צדיקים ביהוה והודו לזכר קדשו 12
Furahini katika Bwana, ninyi mlio wenye haki, lisifuni jina lake takatifu.

< תהילים 97 >