< תהילים 97 >
יהוה מלך תגל הארץ ישמחו איים רבים | 1 |
Bwana anatawala, nchi na ifurahi, visiwa vyote vishangilie.
ענן וערפל סביביו צדק ומשפט מכון כסאו | 2 |
Mawingu na giza nene vinamzunguka, haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi.
אש לפניו תלך ותלהט סביב צריו | 3 |
Moto hutangulia mbele zake na huteketeza adui zake pande zote.
האירו ברקיו תבל ראתה ותחל הארץ | 4 |
Umeme wake wa radi humulika dunia, nchi huona na kutetemeka.
הרים--כדונג נמסו מלפני יהוה מלפני אדון כל-הארץ | 5 |
Milima huyeyuka kama nta mbele za Bwana, mbele za Bwana wa dunia yote.
הגידו השמים צדקו וראו כל-העמים כבודו | 6 |
Mbingu zinatangaza haki yake, na mataifa yote huona utukufu wake.
יבשו כל-עבדי פסל-- המתהללים באלילים השתחוו-לו כל-אלהים | 7 |
Wote waabuduo sanamu waaibishwa, wale wajisifiao sanamu: mwabuduni yeye, enyi miungu yote!
שמעה ותשמח ציון ותגלנה בנות יהודה-- למען משפטיך יהוה | 8 |
Sayuni husikia na kushangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana.
כי-אתה יהוה עליון על-כל-הארץ מאד נעלית על-כל-אלהים | 9 |
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; umetukuka sana juu ya miungu yote.
אהבי יהוה שנאו-רע שמר נפשות חסידיו מיד רשעים יצילם | 10 |
Wale wanaompenda Bwana na wauchukie uovu, kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu.
אור זרע לצדיק ולישרי-לב שמחה | 11 |
Nuru huangaza wenye haki na furaha kwa watu wanyofu wa moyo.
שמחו צדיקים ביהוה והודו לזכר קדשו | 12 |
Furahini katika Bwana, ninyi mlio wenye haki, lisifuni jina lake takatifu.