< תהילים 95 >
לכו נרננה ליהוה נריעה לצור ישענו | 1 |
Oh njoni, tumwimbie Yahwe; na tumwimbie kwa shangwe mwamba wa wokovu wetu.
נקדמה פניו בתודה בזמרות נריע לו | 2 |
Tuingie uweponi mwake kwa shukrani; tumwimbie yeye kwa zaburi ya sifa.
כי אל גדול יהוה ומלך גדול על-כל-אלהים | 3 |
Kwa maana Yahwe ni Mungu mkuu na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
אשר בידו מחקרי-ארץ ותועפת הרים לו | 4 |
Mkononi mwake zimo bonde za dunia; navyo vilele vya milima ni vyake.
אשר-לו הים והוא עשהו ויבשת ידיו יצרו | 5 |
Bahari ni yake, maana aliiumba, na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.
באו נשתחוה ונכרעה נברכה לפני-יהוה עשנו | 6 |
Oh njoni, tumwabudu na tupige magoti; tupige magoti mbele za Yahwe, muumbaji wetu:
כי הוא אלהינו-- ואנחנו עם מרעיתו וצאן ידו היום אם-בקלו תשמעו | 7 |
Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi tu watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake. Ni heri leo mngesikia sauti yake!
אל-תקשו לבבכם כמריבה כיום מסה במדבר | 8 |
Msiifanye migumu mioyo yenu, kama vile huko Meriba, au kama ile siku ya Masa jangwani,
אשר נסוני אבותיכם בחנוני גם-ראו פעלי | 9 |
ambako baba zenu walinijaribu na kunipima, japo walikuwa wameyaona matendo yangu.
ארבעים שנה אקוט בדור-- ואמר עם תעי לבב הם והם לא-ידעו דרכי | 10 |
Kwa miaka arobaini nilikasirishwa na kizazi hicho na kusema, 'Hawa ni watu ambao mioyo yao imepotoka; hawazijui njia zangu.'
אשר-נשבעתי באפי אם-יבאון אל-מנוחתי | 11 |
Hivyo katika hasira yangu niliapa kwamba wasingeingia kamwe mahali pa pumziko.”