< תהילים 95 >

לכו נרננה ליהוה נריעה לצור ישענו 1
Njooni, tumwimbie Bwana kwa furaha; tumfanyie kelele za shangwe Mwamba wa wokovu wetu.
נקדמה פניו בתודה בזמרות נריע לו 2
Tuje mbele zake kwa shukrani, tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.
כי אל גדול יהוה ומלך גדול על-כל-אלהים 3
Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu, mfalme mkuu juu ya miungu yote.
אשר בידו מחקרי-ארץ ותועפת הרים לו 4
Mkononi mwake mna vilindi vya dunia, na vilele vya milima ni mali yake.
אשר-לו הים והוא עשהו ויבשת ידיו יצרו 5
Bahari ni yake, kwani ndiye aliifanya, na mikono yake iliumba nchi kavu.
באו נשתחוה ונכרעה נברכה לפני-יהוה עשנו 6
Njooni, tusujudu, tumwabudu, tupige magoti mbele za Bwana Muumba wetu,
כי הוא אלהינו-- ואנחנו עם מרעיתו וצאן ידו היום אם-בקלו תשמעו 7
kwa maana yeye ndiye Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake, kondoo chini ya utunzaji wake. Kama mkiisikia sauti yake leo,
אל-תקשו לבבכם כמריבה כיום מסה במדבר 8
msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya kule Meriba, kama mlivyofanya siku ile kule Masa jangwani,
אשר נסוני אבותיכם בחנוני גם-ראו פעלי 9
ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu.
ארבעים שנה אקוט בדור-- ואמר עם תעי לבב הם והם לא-ידעו דרכי 10
Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile, nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.”
אשר-נשבעתי באפי אם-יבאון אל-מנוחתי 11
Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”

< תהילים 95 >