< תהילים 95 >
לכו נרננה ליהוה נריעה לצור ישענו | 1 |
Njooni, tumwimbie Bwana kwa furaha; tumfanyie kelele za shangwe Mwamba wa wokovu wetu.
נקדמה פניו בתודה בזמרות נריע לו | 2 |
Tuje mbele zake kwa shukrani, tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.
כי אל גדול יהוה ומלך גדול על-כל-אלהים | 3 |
Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu, mfalme mkuu juu ya miungu yote.
אשר בידו מחקרי-ארץ ותועפת הרים לו | 4 |
Mkononi mwake mna vilindi vya dunia, na vilele vya milima ni mali yake.
אשר-לו הים והוא עשהו ויבשת ידיו יצרו | 5 |
Bahari ni yake, kwani ndiye aliifanya, na mikono yake iliumba nchi kavu.
באו נשתחוה ונכרעה נברכה לפני-יהוה עשנו | 6 |
Njooni, tusujudu, tumwabudu, tupige magoti mbele za Bwana Muumba wetu,
כי הוא אלהינו-- ואנחנו עם מרעיתו וצאן ידו היום אם-בקלו תשמעו | 7 |
kwa maana yeye ndiye Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake, kondoo chini ya utunzaji wake. Kama mkiisikia sauti yake leo,
אל-תקשו לבבכם כמריבה כיום מסה במדבר | 8 |
msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya kule Meriba, kama mlivyofanya siku ile kule Masa jangwani,
אשר נסוני אבותיכם בחנוני גם-ראו פעלי | 9 |
ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu.
ארבעים שנה אקוט בדור-- ואמר עם תעי לבב הם והם לא-ידעו דרכי | 10 |
Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile, nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.”
אשר-נשבעתי באפי אם-יבאון אל-מנוחתי | 11 |
Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”