< תהילים 80 >

למנצח אל-ששנים עדות לאסף מזמור ב רעה ישראל האזינה-- נהג כצאן יוסף ישב הכרובים הופיעה 1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
לפני אפרים ובנימן ומנשה-- עוררה את-גבורתך ולכה לישעתה לנו 2
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
אלהים השיבנו והאר פניך ונושעה 3
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
יהוה אלהים צבאות-- עד-מתי עשנת בתפלת עמך 4
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
האכלתם לחם דמעה ותשקמו בדמעות שליש 5
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
תשימנו מדון לשכנינו ואיבינו ילעגו-למו 6
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
אלהים צבאות השיבנו והאר פניך ונושעה 7
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
גפן ממצרים תסיע תגרש גוים ותטעה 8
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
פנית לפניה ותשרש שרשיה ותמלא-ארץ 9
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
כסו הרים צלה וענפיה ארזי-אל 10
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
תשלח קצירה עד-ים ואל-נהר יונקותיה 11
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
למה פרצת גדריה וארוה כל-עברי דרך 12
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
יכרסמנה חזיר מיער וזיז שדי ירענה 13
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
אלהים צבאות שוב-נא הבט משמים וראה ופקד גפן זאת 14
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
וכנה אשר-נטעה ימינך ועל-בן אמצתה לך 15
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
שרפה באש כסוחה מגערת פניך יאבדו 16
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
תהי-ידך על-איש ימינך על-בן-אדם אמצת לך 17
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
ולא-נסוג ממך תחינו ובשמך נקרא 18
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
יהוה אלהים צבאות השיבנו האר פניך ונושעה 19
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< תהילים 80 >