< תהילים 80 >
למנצח אל-ששנים עדות לאסף מזמור ב רעה ישראל האזינה-- נהג כצאן יוסף ישב הכרובים הופיעה | 1 |
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
לפני אפרים ובנימן ומנשה-- עוררה את-גבורתך ולכה לישעתה לנו | 2 |
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
אלהים השיבנו והאר פניך ונושעה | 3 |
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
יהוה אלהים צבאות-- עד-מתי עשנת בתפלת עמך | 4 |
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
האכלתם לחם דמעה ותשקמו בדמעות שליש | 5 |
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
תשימנו מדון לשכנינו ואיבינו ילעגו-למו | 6 |
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
אלהים צבאות השיבנו והאר פניך ונושעה | 7 |
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
גפן ממצרים תסיע תגרש גוים ותטעה | 8 |
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
פנית לפניה ותשרש שרשיה ותמלא-ארץ | 9 |
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
כסו הרים צלה וענפיה ארזי-אל | 10 |
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
תשלח קצירה עד-ים ואל-נהר יונקותיה | 11 |
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
למה פרצת גדריה וארוה כל-עברי דרך | 12 |
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
יכרסמנה חזיר מיער וזיז שדי ירענה | 13 |
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
אלהים צבאות שוב-נא הבט משמים וראה ופקד גפן זאת | 14 |
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
וכנה אשר-נטעה ימינך ועל-בן אמצתה לך | 15 |
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
שרפה באש כסוחה מגערת פניך יאבדו | 16 |
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
תהי-ידך על-איש ימינך על-בן-אדם אמצת לך | 17 |
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
ולא-נסוג ממך תחינו ובשמך נקרא | 18 |
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
יהוה אלהים צבאות השיבנו האר פניך ונושעה | 19 |
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.