< תהילים 73 >

מזמור לאסף אך טוב לישראל אלהים-- לברי לבב 1
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
ואני--כמעט נטוי (נטיו) רגלי כאין שפכה (שפכו) אשרי 2
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
כי-קנאתי בהוללים שלום רשעים אראה 3
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
כי אין חרצבות למותם ובריא אולם 4
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
בעמל אנוש אינמו ועם-אדם לא ינגעו 5
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
לכן ענקתמו גאוה יעטף-שית חמס למו 6
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
יצא מחלב עינמו עברו משכיות לבב 7
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
ימיקו וידברו ברע עשק ממרום ידברו 8
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
שתו בשמים פיהם ולשונם תהלך בארץ 9
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
לכן ישיב (ישוב) עמו הלם ומי מלא ימצו למו 10
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
ואמרו איכה ידע-אל ויש דעה בעליון 11
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
הנה-אלה רשעים ושלוי עולם השגו-חיל 12
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
אך-ריק זכיתי לבבי וארחץ בנקיון כפי 13
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
ואהי נגוע כל-היום ותוכחתי לבקרים 14
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
אם-אמרתי אספרה כמו הנה דור בניך בגדתי 15
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
ואחשבה לדעת זאת עמל היא (הוא) בעיני 16
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
עד-אבוא אל-מקדשי-אל אבינה לאחריתם 17
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
אך בחלקות תשית למו הפלתם למשואות 18
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
איך היו לשמה כרגע ספו תמו מן-בלהות 19
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
כחלום מהקיץ-- אדני בעיר צלמם תבזה 20
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
כי יתחמץ לבבי וכליותי אשתונן 21
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
ואני-בער ולא אדע בהמות הייתי עמך 22
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
ואני תמיד עמך אחזת ביד-ימיני 23
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
בעצתך תנחני ואחר כבוד תקחני 24
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
מי-לי בשמים ועמך לא-חפצתי בארץ 25
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
כלה שארי ולבבי צור-לבבי וחלקי--אלהים לעולם 26
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
כי-הנה רחקיך יאבדו הצמתה כל-זונה ממך 27
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
ואני קרבת אלהים-- לי-טוב שתי באדני יהוה מחסי לספר כל-מלאכותיך 28
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< תהילים 73 >