< תהילים 72 >
לשלמה אלהים--משפטיך למלך תן וצדקתך לבן-מלך | 1 |
Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
ידין עמך בצדק וענייך במשפט | 2 |
Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
ישאו הרים שלום לעם וגבעות בצדקה | 3 |
Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
ישפט עניי-עם--יושיע לבני אביון וידכא עושק | 4 |
Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
ייראוך עם-שמש ולפני ירח דור דורים | 5 |
Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
ירד כמטר על-גז כרביבים זרזיף ארץ | 6 |
Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
יפרח-בימיו צדיק ורב שלום עד-בלי ירח | 7 |
Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
וירד מים עד-ים ומנהר עד-אפסי-ארץ | 8 |
Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
לפניו יכרעו ציים ואיביו עפר ילחכו | 9 |
Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
מלכי תרשיש ואיים מנחה ישיבו מלכי שבא וסבא אשכר יקריבו | 10 |
Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
וישתחוו-לו כל-מלכים כל-גוים יעבדוהו | 11 |
Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
כי-יציל אביון משוע ועני ואין-עזר לו | 12 |
Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
יחס על-דל ואביון ונפשות אביונים יושיע | 13 |
Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
מתוך ומחמס יגאל נפשם וייקר דמם בעיניו | 14 |
Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
ויחי-- ויתן-לו מזהב שבא ויתפלל בעדו תמיד כל-היום יברכנהו | 15 |
Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
יהי פסת-בר בארץ-- בראש הרים ירעש כלבנון פריו ויציצו מעיר כעשב הארץ | 16 |
Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
יהי שמו לעולם-- לפני-שמש ינין (ינון) שמו ויתברכו בו כל-גוים יאשרוהו | 17 |
Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
ברוך יהוה אלהים--אלהי ישראל עשה נפלאות לבדו | 18 |
Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
וברוך שם כבודו-- לעולם וימלא כבודו את-כל הארץ-- אמן ואמן | 19 |
Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
כלו תפלות-- דוד בן-ישי | 20 |
Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.