< תהילים 65 >
למנצח מזמור לדוד שיר ב לך דמיה תהלה אלהים בציון ולך ישלם-נדר | 1 |
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni; kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
שמע תפלה-- עדיך כל-בשר יבאו | 2 |
Ewe usikiaye maombi, kwako wewe watu wote watakuja.
דברי עונת גברו מני פשעינו אתה תכפרם | 3 |
Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi, wewe ulisamehe makosa yetu.
אשרי תבחר ותקרב-- ישכן חצריך נשבעה בטוב ביתך קדש היכלך | 4 |
Heri wale uliowachagua na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako! Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako, mema ya Hekalu lako takatifu.
נוראות בצדק תעננו-- אלהי ישענו מבטח כל-קצוי-ארץ וים רחקים | 5 |
Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki, Ee Mungu Mwokozi wetu, tumaini la miisho yote ya duniani na la bahari zilizo mbali sana,
מכין הרים בכחו נאזר בגבורה | 6 |
uliyeumba milima kwa uwezo wako, ukiwa umejivika nguvu,
משביח שאון ימים--שאון גליהם והמון לאמים | 7 |
uliyenyamazisha dhoruba za bahari, ngurumo za mawimbi yake, na ghasia za mataifa.
וייראו ישבי קצות--מאותתיך מוצאי בקר וערב תרנין | 8 |
Wale wanaoishi mbali sana wanaogopa maajabu yako, kule asubuhi ipambazukiapo na kule jioni inakofifilia umeziita nyimbo za furaha.
פקדת הארץ ותשקקה רבת תעשרנה-- פלג אלהים מלא מים תכין דגנם כי-כן תכינה | 9 |
Waitunza nchi na kuinyeshea, waitajirisha kwa wingi. Vijito vya Mungu vimejaa maji ili kuwapa watu nafaka, kwa maana wewe umeviamuru.
תלמיה רוה נחת גדודה ברביבים תמגגנה צמחה תברך | 10 |
Umeilowesha mifereji yake na kusawazisha kingo zake; umeilainisha kwa manyunyu na kuibariki mimea yake.
עטרת שנת טובתך ומעגליך ירעפון דשן | 11 |
Umeuvika mwaka taji ya baraka, magari yako yanafurika kwa wingi.
ירעפו נאות מדבר וגיל גבעות תחגרנה | 12 |
Mbuga za majani za jangwani umezineemesha; vilima vimevikwa furaha.
לבשו כרים הצאן-- ועמקים יעטפו-בר יתרועעו אף-ישירו | 13 |
Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama, na mabonde yamepambwa kwa mavuno; vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.