< תהילים 64 >

למנצח מזמור לדוד ב שמע-אלהים קולי בשיחי מפחד אויב תצר חיי 1
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
תסתירני מסוד מרעים מרגשת פעלי און 2
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
אשר שננו כחרב לשונם דרכו חצם דבר מר 3
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
לירת במסתרים תם פתאם ירהו ולא ייראו 4
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
יחזקו-למו דבר רע-- יספרו לטמון מוקשים אמרו מי יראה-למו 5
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
יחפשו עולת-- תמנו חפש מחפש וקרב איש ולב עמק 6
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
וירם אלהים חץ פתאום--היו מכותם 7
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
ויכשילוהו עלימו לשונם יתנדדו כל-ראה בם 8
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
וייראו כל-אדם ויגידו פעל אלהים ומעשהו השכילו 9
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
ישמח צדיק ביהוה וחסה בו ויתהללו כל-ישרי-לב 10
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.

< תהילים 64 >