< תהילים 64 >
למנצח מזמור לדוד ב שמע-אלהים קולי בשיחי מפחד אויב תצר חיי | 1 |
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
תסתירני מסוד מרעים מרגשת פעלי און | 2 |
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
אשר שננו כחרב לשונם דרכו חצם דבר מר | 3 |
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
לירת במסתרים תם פתאם ירהו ולא ייראו | 4 |
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
יחזקו-למו דבר רע-- יספרו לטמון מוקשים אמרו מי יראה-למו | 5 |
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
יחפשו עולת-- תמנו חפש מחפש וקרב איש ולב עמק | 6 |
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
וירם אלהים חץ פתאום--היו מכותם | 7 |
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
ויכשילוהו עלימו לשונם יתנדדו כל-ראה בם | 8 |
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
וייראו כל-אדם ויגידו פעל אלהים ומעשהו השכילו | 9 |
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
ישמח צדיק ביהוה וחסה בו ויתהללו כל-ישרי-לב | 10 |
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.