< תהילים 58 >

למנצח אל-תשחת לדוד מכתם ב האמנם--אלם צדק תדברון מישרים תשפטו בני אדם 1
Je, ninyi watawala mnaongea haki? Mnahukumu kwa haki, ninyi watu?
אף-בלב עולת תפעלון בארץ--חמס ידיכם תפלסון 2
Hapana, mnafanya uovu mioyoni mwenu; munaeneza vurugu nchi yote kwa mikono yenu.
זרו רשעים מרחם תעו מבטן דברי כזב 3
Waovu huenenda katika upotovu hata walipokuwa tumboni; wao wanaenenda katika upotovu tangu kuzaliwa, wakiongea uongo.
חמת-למו כדמות חמת-נחש כמו-פתן חרש יאטם אזנו 4
Sumu yao ni kama sumu ya nyoka; wako kama fira kiziwi azibaye masikio yake,
אשר לא-ישמע לקול מלחשים חובר חברים מחכם 5
ambaye hasikilizi sauti ya waganga, haijalishi ustadi walio nao.
אלהים--הרס שנימו בפימו מלתעות כפירים נתץ יהוה 6
Vunja meno yao midomoni mwao, Mungu; uyatoe meno ya mwana simba, Yahwe.
ימאסו כמו-מים יתהלכו-למו ידרך חצו כמו יתמללו 7
Wayeyuke kama maporomoko ya maji; wafyatuapo mishale yao, iwe kama haina ncha.
כמו שבלול תמס יהלך נפל אשת בל-חזו שמש 8
Wawe kama konokono ambaye huyeyuka na kutoweka, kama mtoto aliye zaliwa kabla ya wakati ambaye hakuona jua.
בטרם יבינו סירתכם אטד כמו-חי כמו-חרון ישערנו 9
Kabla ya vyungu vyenu kupata joto la kuungua kwa miiba, yeye ataviondosha kwa upepo mkali, miiba ya kijani yote na ile inayoungua.
ישמח צדיק כי-חזה נקם פעמיו ירחץ בדם הרשע 10
Mwenye haki atafurahia atakapoona kisasi cha Mungu; ataiosha miguu yake kwenye damu ya waovu,
ויאמר אדם אך-פרי לצדיק אך יש-אלהים שפטים בארץ 11
hivyo watu watasema, “Hakika kuna tuzo kwa ajili ya mtu wenye haki; hakika kuna Mungu ahukumuye ulimwengu.”

< תהילים 58 >