< תהילים 58 >

למנצח אל-תשחת לדוד מכתם ב האמנם--אלם צדק תדברון מישרים תשפטו בני אדם 1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Enyi watawala, je, kweli mwanena kwa haki? Je, mnahukumu kwa unyofu miongoni mwa watu?
אף-בלב עולת תפעלון בארץ--חמס ידיכם תפלסון 2
La, mioyoni mwenu mnatunga udhalimu, na mikono yenu hupima jeuri duniani.
זרו רשעים מרחם תעו מבטן דברי כזב 3
Waovu ni wapotovu tangu kuzaliwa kwao, toka tumboni mwa mama zao ni wakaidi na husema uongo.
חמת-למו כדמות חמת-נחש כמו-פתן חרש יאטם אזנו 4
Sumu yao ni kama sumu ya nyoka, kama ile ya fira ambaye ameziba masikio yake,
אשר לא-ישמע לקול מלחשים חובר חברים מחכם 5
ambaye hatasikia sauti ya kutumbuiza ya mwaguzi, hata kama mganga angecheza kwa ustadi kiasi gani.
אלהים--הרס שנימו בפימו מלתעות כפירים נתץ יהוה 6
Ee Mungu, yavunje meno katika vinywa vyao; Ee Bwana, vunja meno makali ya hao simba!
ימאסו כמו-מים יתהלכו-למו ידרך חצו כמו יתמללו 7
Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi, wavutapo pinde zao, mishale yao na iwe butu.
כמו שבלול תמס יהלך נפל אשת בל-חזו שמש 8
Kama konokono ayeyukavyo akitembea, kama mtoto aliyezaliwa akiwa mfu, wasilione jua.
בטרם יבינו סירתכם אטד כמו-חי כמו-חרון ישערנו 9
Kabla vyungu vyenu havijapata moto wa kuni za miiba, zikiwa mbichi au kavu, waovu watakuwa wamefagiliwa mbali.
ישמח צדיק כי-חזה נקם פעמיו ירחץ בדם הרשע 10
Wenye haki watafurahi waonapo wakilipizwa kisasi, watakapochovya nyayo zao katika damu ya waovu.
ויאמר אדם אך-פרי לצדיק אך יש-אלהים שפטים בארץ 11
Ndipo wanadamu watasema, “Hakika utulivu wa wenye haki bado una thawabu, hakika kuna Mungu ahukumuye dunia.”

< תהילים 58 >