< תהילים 57 >
למנצח אל-תשחת לדוד מכתם-- בברחו מפני-שאול במערה ב חנני אלהים חנני-- כי בך חסיה נפשי ובצל-כנפיך אחסה-- עד יעבר הוות | 1 |
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
אקרא לאלהים עליון לאל גמר עלי | 2 |
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
ישלח משמים ויושיעני-- חרף שאפי סלה ישלח אלהים חסדו ואמתו | 3 |
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
נפשי בתוך לבאם-- אשכבה להטים בני-אדם--שניהם חנית וחצים ולשונם חרב חדה | 4 |
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
רומה על-השמים אלהים על כל-הארץ כבודך | 5 |
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
רשת הכינו לפעמי-- כפף נפשי כרו לפני שיחה נפלו בתוכה סלה | 6 |
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
נכון לבי אלהים נכון לבי אשירה ואזמרה | 7 |
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
עורה כבודי--עורה הנבל וכנור אעירה שחר | 8 |
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
אודך בעמים אדני אזמרך בלאמים | 9 |
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
כי-גדל עד-שמים חסדך ועד-שחקים אמתך | 10 |
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
רומה על-שמים אלהים על כל-הארץ כבודך | 11 |
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.